Wananchi wahimizwa kulima mkonge wanufaike kiuchumi

Hellen Stanislaus, daimatznews@gmail.com JAMII imeshauriwa kujikita katika kilimo cha mkonge ili kiweze kuwanufaisha kiuchumi. Mkuu wa sehemu ya masoko wa Bodi ya mkonge Tanzania, David Maghali akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la bodi hiyo katika viwanja vya Sabasaba Dar es Salam Wito huo umetolewa Julai 10, 2025 jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Sehemu ya Masoko wa Bodi ya Mkonge Tanzania, David Maghali, alipokuwa akizungumza katika maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba. Amesema zao la mkonge lina faida kubwa kutokana na kuzalisha bidhaa nyingi kwa uchumi wa mkulima taifa kwa ujumla hivyo wananchi hawana budi kukichangamkia. "Mkonge una faida kubwa kuanzia mbegu hadi mabaki yake na tuna soko la uhakika istoshe nchi yetu imejaliwa kuwa na ardhi yenye rutuba. Wananchi wachangamkie fursa ili kujikwamua," alisema Maghali. Naye Ofisa Kilimo Mwandamizi wa bodi hiyo Emmanuel Lutego ametaja faida za mabaki ya mkonge kuwa ni nishati safi ya kupikia....