Machapisho

Wananchi wahimizwa kulima mkonge wanufaike kiuchumi

Picha
Hellen Stanislaus, daimatznews@gmail.com JAMII imeshauriwa kujikita katika kilimo cha mkonge ili kiweze kuwanufaisha kiuchumi. Mkuu wa sehemu ya masoko wa Bodi ya mkonge Tanzania, David Maghali akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la  bodi hiyo katika viwanja vya Sabasaba Dar es Salam Wito huo umetolewa  Julai 10, 2025 jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Sehemu ya Masoko wa Bodi ya Mkonge Tanzania, David Maghali, alipokuwa akizungumza katika maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba. Amesema zao la mkonge lina faida kubwa  kutokana na kuzalisha bidhaa nyingi kwa uchumi wa mkulima taifa kwa ujumla hivyo wananchi hawana budi kukichangamkia. "Mkonge una faida kubwa kuanzia mbegu hadi mabaki yake na tuna soko la uhakika  istoshe nchi yetu imejaliwa kuwa na ardhi yenye rutuba. Wananchi wachangamkie fursa ili kujikwamua," alisema Maghali. Naye Ofisa Kilimo Mwandamizi wa bodi hiyo Emmanuel Lutego ametaja faida za mabaki ya mkonge kuwa ni nishati safi ya kupikia....

Maswi aipongeza Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali

Picha
Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali imepongezwa kwa kuendelea kusimamia kwa weledi mashauri ya madai na usuluhishi hatua ambayo imesaidia Serikali kuongeza kasi katika kuwaletea wananchi maendeleo. Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakimu Maswi akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Mashauri na Uthibiti Ubora wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Mercy Kyamba alipotembelea banda la Ofisi hiyo wakati wa Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakim Maswi alipotembelea banda la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya 49 ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam. Maswi alisema kuwa uwepo wa weledi na ufanisi katika uendeshaji wa mashauri ya madai, usuluhishi, Katiba, Haki za Binadamu na Uchaguzi katika Ofisi hiyo umeongeza kasi katika kupunguza na kutatua migogoro ya kisheria kwa njia ya majadil...

REA yajidhatiti kufikisha lengo kitaifa nishati safi ya kupikia

Picha
-Mkurugenzi Mkuu REA abainisha hatua zinazochukuliwa -Amshukuru Rais Samia kwa kuwezesha Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia. Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy, (kushoto),akipata maelezo kuhusu bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia zinazosambazwa na Kampuni ya Jucho Chanya kutoka kwa Ofisa Masoko wa kampuni hiyo, Ibrahim Kikoti katika Banda la REA kwenye Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa jijiniDar es SalaamJulai 7, 2025 Amebainisha hayo Julai 07, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA). “REA inalo jukumu la kuhakikisha maeneo yote ya vijijini yanapata aina zote za nishati s...

Wanyama 400 wauawa Mikumi

Picha
 -Kamera kunasa wahalifu Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Hifadhi ya Taifa Mikumi inajipanga ili kuweka  kamera zikazowekwa geti la kuingilia hifadhi hiyo eneo la Kijiji cha Doma, Mikumi Mjini inapoishia hifadhi kwenye barabara Kuu kwenda Iringa, inayopita hifadhini humo, ikielezwa kuwa wastani wa wanyama 400 hufa kwa kugonjwa na gari kila mwaka. Kamishna Augustine Masesa Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Kamishna Augustine Masesa amesema hayo Juni 28/2025 akieleza kuwa hatua hiyo inalenga  kuwanasa madereva watakaowagonga wanyama kwenye eneo la hifadhi na magari yanayovunja sheria kwa kutembea mwendo usioruhusiwa.  Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu hifadhi hiyo, ambapo amesema mradi huo unahitaji takriban shilingi bilioni 2. “Tayari upembuzi yakinifu umefanywa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa (UNDP), tunasubiri pesa tu ipatikane kutekeleza mradi huo kwenye eneo hilo la kilometa 50 inapokatiza b...

Mambo matano ya kipekee usiyoyajua Hifadhi ya Taifa Saadan

Picha
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Licha ya Tanzania kuwa na hifadhi 21 za Taifa zenye vivutio mbalimbali vya utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan imebahatika kuwa na vivutio vya kipekee barani Afrika, hivyo kuitofautisha na nyingine. Hifadhi ya Taifa ya Saadani inayopatikana eneo la mikoa ya Pwani   na Tanga ina mambo matano yanayoelezwa kuitofautisha na nyingine nchini, hata barani Afrika hivyo kuwa ya kipekee. Hifadhi hiyo iliyopo katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani   na wilaya za Handeni na Pangani Mkoa wa Tanga ina ukubwa wa takriban Kilomete za mraba 1,100   na ilianzishwa mwaka 2009. Ofisa Mhifadhi, Utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan, Daud Gordon Akizungumza na wanahabari ndani ya hifadhi hiyo, Ofisa Mhifadhi, anayeongoza kitengo cha utalii, Hifadhi ya Taifa Saadan, Daud Gordon ameyataja mambo hayo kuwa ni makutano ya Bahari ya Hindi na nyika, uwepo wa mlango bahari wa Mto Wami unaoingia Bahari ya Hindi na mazalia ya kasa wa kijani. Mengine ni wanyama na b...

SANAMU YA BIKIRA MARIA YAONEKANA HIFADHI YA TAIFA SAADAN

Picha
- Maajabu mapya ya kipekee Exuperius Kachenje Sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria (Mariam), anayetajwa na vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu na Qur’an Tukufu (Mariam), ndiye mama wa Yesu Kristo (Nabii Issa bin Mariam), imegundulika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani, ikitajwa kuwa ni maajabu mapya yasiyo ya kawaida kwa watalii ndani na nje ya Tanzania, inayoongeza upekee wa hifadhi hiyo kwa utalii. Mti wa mbuyu wenye sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadan. Picha na Exuperius Kachenje Ofisa Mhifadhi kitengo cha Utalii, Hifadhi ya Taifa Saadani (SANAPA) Daud Gordon amebainisha hayo Juni 26, 2025 akieleza kwamba kivutio hicho kipya ni nyenzo muhimu katika kukuza utalii wa kiimani, hata kuweza kuwa sehemu ya hija kwa waamini, hasa wanaoamini na kumheshimu mama huyo kadiri ya mapokeo ya imani zao,mfano ukiwa Kanisa Katoliki. Gordon amesema kuwa sanamu hiyo ya asili inaonekana katikati ya mti wa mbuyu, eneo la Buyuni  ndani ya hifadhi hiyo,...

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Picha
  -Maajabu mapya ya kipekee Exuperius Kachenje Sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria (Mariam), anayetajwa na vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu na Qur’an Tukufu (Mariam), ndiye mama wa Yesu Kristo (Nabii Issa bin Mariam), imegundulika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani, ikitajwa kuwa ni maajabu mapya yasiyo ya kawaida kwa watalii ndani na nje ya Tanzania, inayoongeza upekee wa hifadhi hiyo kwa utalii. Mti wa mbuyu wenye sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadan. Picha na Exuperius Kachenje Ofisa Mhifadhi kitengo cha uta;ii, Hifadhi ya Taifa Saadani (SANAPA) Daud Gordon amebainisha hayo Juni 26, 2025 akieleza kwamba kivutio hicho kipya ni nyenzo muhimu katika kukuza utalii wa kiimani, hata kuweza kuwa sehemu ya hija kwa waamini, hasa wanaoamini na kumheshimu mama huyo kadiri ya mapokeo ya imani zao,mfano ukiwa Kanisa Katoliki. Gordon amesema kuwa sanamu hiyo ya asili inaonekana katikati ya mti wa mbuyu, eneo la Buyuni  ndani ya h...