Salum Mwalimu aja na kuwekezesha vijana kuanzisha kampuni za utalii, biashara

 Mgombea Urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, ameahidi kuanzisha mfuko maalumu wa kuwawezesha vijana kuwekeza katika sekta ya utalii, iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu, utakaofanyika Oktoba 29,2025.

Ametoa ahadi hiyo alipokuwa akiiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Arusha, ambapo amesema mpango huo utahusisha utoaji wa magari ya kuanzia, mitaji midogo na mafunzo maalum kwa vijana wenye ndoto ya kuingia kwenye biashara ya utalii.

"Mpango huo ni sehemu ya ajenda ya CHAUMMA ya kupanua wigo wa ajira kwa vijana," amesema Mwalimu.

Mgombea urais huyo wa CHAUMMA ameitaka jamii kuwa tayari kuunga mkono juhudi hizo kwa kushiriki kikamilifu kwenye mabadiliko ya kiuchumi kupitia sekta zenye fursa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi