NHC: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UMILIKI MAKAZI YA KISASA SAMIA HOUSING KIJICHI
-NMB watembelea, wajionea fursa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail Shirika la Nyumba la Taifa, National Housing Corporation (NHC), limeweka wazi kuwepo kwa fursa mpya za umiliki wa nyumba za kisasa kupitia Mradi wa Samia Housing Kijichi, wilayani Temeke Mkoa wa Dar es Salaam wakiwataka wananchi wakiwemo watumishi wa Benki ya NMB Plc kuichangamkia. Kwa hatua hiyo, NHC limeendelea kufungua milango ya umiliki wa makazi ya kisasa kwa Watanzania kupitia utekelezaji wa mradi huo, unaolenga kutoa nyumba bora, salama na zenye miundombinu ya kisasa kwa wananchi wanaotamani kumiliki makazi yenye hadhi. Akitoa maelezo kuhusu mradi huo kwa maofisa wa NMB Bank Plc, kuhusu mradi huo Machi,7, 2026, Ofisa Masoko wa NHC, Thobiasi Kavishe, amesema mradi huo unatarajiwa kujumuisha takribani nyumba 260 zitakazojengwa katika majengo ya ghorofa aina ya G+4 . Kavishe amesema, nyumba hizo zimepangwa kwa kuzingatia mahitaji ya makundi tofauti ya wanunuzi. “Kutakuwepo na nyumba zenye chumba kimoja ch...