Machapisho

TRC yaanza kuunganisha injini za treni za reli ya MGR

Picha
-Yaweka historia Afrika Mashariki Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza kuunganisha injini za treni za reli ya Meter Gauge Railway (MGR) ndani ya nchi, hatua inayofanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki kutekeleza mpango huo.  Hatua hiyo imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Wakati wa ziara ya ukaguzi wa mradi wa kuunganisha injini hizo katika Karakana ya Reli ya Pugu jijini Dar es Salaam leo Machi 14,2026, kamati hiyo imeishauri TRC kuendelea kuimarisha ujuzi wa vijana wa Kitanzania wanaoshiriki katika mradi huo kwa kuwapatia mafunzo ya juu ya kiufundi ndani na nje ya nchi. Mwenyekiti wa kamati hiyo,Selemani Kakoso, amesema kuwa uwekezaji katika kuendeleza taaluma za mafundi wazawa utasaidia kuongeza utaalamu wa kiufundi, ubunifu pamoja na ufanisi katika sekta ya reli nchini. Pia meiihimiza TRC kuweka kipaumbele katika kutoa ajira kwa vijana waliopata mafunzo hayo ili waendelee kuchangia maende...

Rostam Aziz ainunua NMG ya Kenya inayozalisha magazeti ya Daily Nation

Picha
- Arejea kwenye umiliki wa vyombo vya habari Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mfanyabishara bilionea wa Tanzania, Rostam Azizi amenunua asilimia 100 ya hisa za Shirika la Aga Khan Fund for Economic Development S.A ( AKFED ) ,  katika Kampuni ya Nation Media Group PLC ( NMG ), yenye makao makuu yake nchini Kenya, inayozalisha magazeti ya Daily Nation na kumiliki vituo mbalimbali vya redio na televisheni  ukanda wa Afrika Mashariki. Mtukufu Prince Rahim Aga Khan V (kulia) na mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Azizi. Picha kwa hisani ya Mtandao wa Daily Nation. Bila ya kutaja thamani ya hisa, taarifa iliyotolewa leo  Machi 10,2026 na AKFED imeeleza umiliki wake ul ikuwa  asilimia 54.08 ya hisa zote za NMG, ambazo sasa ni mali ya Rostam chini ya  Taarifa Ltd , kampuni inayomilikiwa na mfanyabiashara huyo wa Tanzania. . Uamuzi huo wa Rostam kununua NMG, unamrejesha mfanyabiashara huyo bilionea wa Tanzania katika biashara, umiliki na uendeshaji wa vy...

NHC: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UMILIKI MAKAZI YA KISASA SAMIA HOUSING KIJICHI

Picha
-NMB watembelea, wajionea fursa  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail Shirika la Nyumba la Taifa, National Housing Corporation (NHC), limeweka wazi kuwepo kwa fursa mpya za umiliki wa nyumba za kisasa kupitia Mradi wa Samia Housing Kijichi, wilayani Temeke Mkoa wa Dar es Salaam likiwataka wananchi wakiwemo watumishi wa Benki ya NMB Plc kuichangamkia. Kwa hatua hiyo, NHC limeendelea kufungua milango ya umiliki wa makazi ya kisasa kwa Watanzania kupitia utekelezaji wa mradi huo, unaolenga kutoa nyumba bora, salama na zenye miundombinu ya kisasa kwa wananchi wanaotamani kumiliki makazi yenye hadhi. Akitoa maelezo kuhusu mradi huo kwa maofisa wa NMB Bank Plc, Machi,7, 2026, Ofisa Masoko wa NHC, Thobiasi Kavishe, amesema mradi huo unatarajiwa kujumuisha takribani nyumba 260 zitakazojengwa katika majengo ya ghorofa aina ya G+4 . Kavishe amesema, nyumba hizo zimepangwa kwa kuzingatia mahitaji ya makundi tofauti ya wanunuzi. “Kutakuwepo na nyumba zenye chumba kimoja cha kulala, vyumba ...

BEI MPYA KIKOMO YA PETROLI MWEZI MACHI 2026 HII HAPA

Picha
-Dar yauzwa 2,864, Katoro 3,124 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa, zitakazoanza kutumika  leo Machi 4,2026 saa 6 siku, huku bei ya chini ya petroli ikiwa kwa Sh2,864 kwa lita na dizeli Sh2,858 jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Dk. James Mwainyekule Kwa mujibu EWURA, bei kikomo ya juu ya petroli ni Sh3,124 na dizeli Sh 3119 Katoro mkoani Kagera, ambapo bei ya juu zaidi ya mafuta ya taa ni Sh3,193 Katoro, huku bei ya chini ni Sh2,932 kwa lita moja. Zaidi soma jedwali la EWURA hapa chini kupata bei za mafuta kwa maeneo mengine nchini ; 

MAELEKEZO YA RAIS DK. SAMIA MRADI UJENZI MATENKI YA MAFUTA HAYA HAPA

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amezipa maelekezo maalum wizara na taasisi za Serikali akizitaka kuhakikisha Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam unatekelezwa kwa wakati na kukidhi viwango vya kimataifa. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, Machi 3, 2026. Ameiagiza pia Wizara ya Nishati, kuhakikisha inaimarisha miundombinu ya hifadhi ya mafuta na taifa linakuwa na akiba ya kutosha, ili kukabiliana na misukosuko ya bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia, huku akieleza kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani ni changamoto inayoongeza umuhimu wa kuwa na miundombinu madhubuti ya nishati. Rais Dk. Samia ametoa maelekezo hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati, Machi 3, 2026, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kwamba uwekezaji huo ni ha...

TAWA KANDA MAALUM DAR YAHIMIZA UHIFADHI WALIO HATARINI KUTOWEKA

Picha
-Yaadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani -Yaita wananchi kujionea vivutio vya mjini  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Uhifadhi Wanyamapori nchini (TAWA), Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo Machi 3, 2026, imeungana na wadau wengine wa sekta hiyo katika kuadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani, inayoadhimishwa Machi 3 kila mwaka, ikihimiza jamii kushiriki katika kulinda wanyama walio katika hatari ya kutoweka   kwa faida ya taifa leo na vizazi vijavyo. Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy  Kamanda wa Uhifadhi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy ametoa wito huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Machi 3, 2026   alipokuwa akizungumzia maadhimisho hayo yaliyobeba Kauli mbiu isemayo; ‘Mimea dawa, manukato, uhifadhi urithi na kuboresha maisha.’ Amesema kauli mbiu hiyo inahamasisha wananchi kutunza hifadhi wanyama pori na mimea, lakini pia TAWA imetumia siku hiyo kuwapa elimu na kuwahamasisha wananchi k...

PADRI MACHIBYA AWAKUMBUSHA WAKATOLIKI THAMANI YA UHAI

Picha
 Mwandishi Wetu, Waumini wa Kanisa Katoliki nchini wamekumbushwa kuwa uhai huanza na pumzi ya Mungu, na kuwataka kuutumia wakati huu wa kwaresma kukumbuka kwamba kila uhai ni pumzi iliyotoka kwa Mungu. Rai hiyo imetolwa na P adri Vedastus Machibula wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza,(Pichani Juu),  ambaye kwa sasa yuko Masomoni nchini Hispania, katika Tafakari yake ya Kwaresma ambapo amesema Yesu  Kristo alimwaga damu yake kwa ajili ya uhai, ili wanadamu kukombolewa. Kupitia ujumbe huo, amewahimiza waamini wa Kanisa Katoliki kuitazama Kwaresma kama wakati wa kutafakari kwa kina juu ya thamani ya uhai akieleza kuwa uhai ni zawadi takatifu kutoka kwa Mungu, inayopaswa kulindwa na kuheshimiwa katika kila hatua ya maisha ya Mwanadamu. Kwa mujibu wa mafundisho ya Kanisa Katoliki, uhai ni kitu Kitakatifu ambacho asili yake ni Mungu pekee,  tangu kutungwa mimba hadi kifo cha kawaida. Damu ya Yesu Kristo msalabani ni ishara ya upendo na uthibitisho wa thamani ya kila uhai kwa mwan...