Machapisho

WABUNGE WA PIC WASHUHUDIA NHC ILIVYOTEKELEZA MIRADI SAMIA HOUSING, KAWE 711

Picha
- Waelezwa nyumba 560 zauzwa kabla ya kukamilika -NHC yaokoa Sh24 bilioni kwa kukopa Sh6 bilioni badala ya Sh30 bilioni  - Mradi wazalisha ajira 1,800,  uwanja wa michezo, soko kujengwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ukiangalia miradi ya Samia Housing Scheme Kawe na Kawe 711 inayotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC), utagundua kuwa haikuota kama uyoga, bali ni matokeo ya juhudi, nidhamu na usimamizi bora wa kazi zake, ambazo sasa zimeleta matokeo chanya. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah (aliyesimama mbele), akitoa maelezo kuhusu Mradi wa Samia Housing wa Kawe Dar es Salaam, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Serikali(PIC), iliyofanya ziara kwenye miradi ya NHC Machi 25,2026. Bila shaka, hali hiyo imempa nguvu na msukumo Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Hamad Abdallah, kuieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Serikali (PIC) kuwa jumla ya nyumba 560 zilizojengwa katika Mradi wa Samia Hou...

LUKUVI 'AKATISHA' ZIARA YA WABUNGE NHC

Picha
 - Mkurugenzi NHC asema alishiriki mradi uiotembelewa leo - Atajwa ni mbunge, waziri mkongwe zaidi -Ni mwalimu, kioo kwa wabunge na wanasiasa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Kifo cha Mkongwe wa siasa nchini ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge na Uratibu na Watu Wenye Ulemavu, William Lukuvi kimeilazimu Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), kukatisha ziara waliyoianza kwenye Mradi wa Samia Housing Scheme, Dar es Salaam inayotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Marehemu William Lukuvi Taarifa ya kifo cha Lukuvi imetolewa  leo, Machi 25, 2026  na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  ikieleza kuwa waziri huyo amefariki saa 1 asubuhi. Lukuvi anayetajwa kuwa mbunge aliyekaa bungeni kwa kipindi kirefu zaidi kati ya wabunge wa sasa hadi alipofariki, anaelezwa amekutwa na umauti wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma, baada ya kupatwa na mshituko wa moyo. Wakati taarifa ya kifo cha Luk...

TRC YAANZA KUUNGANISHA INJINI ZA TRENI RELI YA MGR

Picha
-Yaweka historia Afrika Mashariki Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza kuunganisha injini za treni za reli ya Meter Gauge Railway (MGR) ndani ya nchi, hatua inayofanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki kutekeleza mpango huo.  Hatua hiyo imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Wakati wa ziara ya ukaguzi wa mradi wa kuunganisha injini hizo katika Karakana ya Reli ya Pugu jijini Dar es Salaam leo Machi 14,2026, kamati hiyo imeishauri TRC kuendelea kuimarisha ujuzi wa vijana wa Kitanzania wanaoshiriki katika mradi huo kwa kuwapatia mafunzo ya juu ya kiufundi ndani na nje ya nchi. Mwenyekiti wa kamati hiyo,Selemani Kakoso, amesema kuwa uwekezaji katika kuendeleza taaluma za mafundi wazawa utasaidia kuongeza utaalamu wa kiufundi, ubunifu pamoja na ufanisi katika sekta ya reli nchini. Pia meiihimiza TRC kuweka kipaumbele katika kutoa ajira kwa vijana waliopata mafunzo hayo ili waendelee kuchangia maende...

ROSTAM AZIZ AINUNUA NMG YA KENYA INAYOZALISHA MAGAZETI YA DAILY NATION

Picha
- Arejea kwenye umiliki wa vyombo vya habari Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mfanyabishara bilionea wa Tanzania, Rostam Azizi amenunua asilimia 100 ya hisa za Shirika la Aga Khan Fund for Economic Development S.A ( AKFED ) ,  katika Kampuni ya Nation Media Group PLC ( NMG ), yenye makao makuu yake nchini Kenya, inayozalisha magazeti ya Daily Nation na kumiliki vituo mbalimbali vya redio na televisheni  ukanda wa Afrika Mashariki. Mtukufu Prince Rahim Aga Khan V (kulia) na mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Azizi. Picha kwa hisani ya Mtandao wa Daily Nation. Bila ya kutaja thamani ya hisa, taarifa iliyotolewa leo  Machi 10,2026 na AKFED imeeleza umiliki wake ul ikuwa  asilimia 54.08 ya hisa zote za NMG, ambazo sasa ni mali ya Rostam chini ya  Taarifa Ltd , kampuni inayomilikiwa na mfanyabiashara huyo wa Tanzania. . Uamuzi huo wa Rostam kununua NMG, unamrejesha mfanyabiashara huyo bilionea wa Tanzania katika biashara, umiliki na uendeshaji wa vy...

NHC: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UMILIKI MAKAZI YA KISASA SAMIA HOUSING KIJICHI

Picha
-NMB watembelea, wajionea fursa  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail Shirika la Nyumba la Taifa, National Housing Corporation (NHC), limeweka wazi kuwepo kwa fursa mpya za umiliki wa nyumba za kisasa kupitia Mradi wa Samia Housing Kijichi, wilayani Temeke Mkoa wa Dar es Salaam likiwataka wananchi wakiwemo watumishi wa Benki ya NMB Plc kuichangamkia. Kwa hatua hiyo, NHC limeendelea kufungua milango ya umiliki wa makazi ya kisasa kwa Watanzania kupitia utekelezaji wa mradi huo, unaolenga kutoa nyumba bora, salama na zenye miundombinu ya kisasa kwa wananchi wanaotamani kumiliki makazi yenye hadhi. Akitoa maelezo kuhusu mradi huo kwa maofisa wa NMB Bank Plc, Machi,7, 2026, Ofisa Masoko wa NHC, Thobiasi Kavishe, amesema mradi huo unatarajiwa kujumuisha takribani nyumba 260 zitakazojengwa katika majengo ya ghorofa aina ya G+4 . Kavishe amesema, nyumba hizo zimepangwa kwa kuzingatia mahitaji ya makundi tofauti ya wanunuzi. “Kutakuwepo na nyumba zenye chumba kimoja cha kulala, vyumba ...

BEI MPYA KIKOMO YA PETROLI MWEZI MACHI 2026 HII HAPA

Picha
-Dar yauzwa 2,864, Katoro 3,124 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa, zitakazoanza kutumika  leo Machi 4,2026 saa 6 siku, huku bei ya chini ya petroli ikiwa kwa Sh2,864 kwa lita na dizeli Sh2,858 jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Dk. James Mwainyekule Kwa mujibu EWURA, bei kikomo ya juu ya petroli ni Sh3,124 na dizeli Sh 3119 Katoro mkoani Kagera, ambapo bei ya juu zaidi ya mafuta ya taa ni Sh3,193 Katoro, huku bei ya chini ni Sh2,932 kwa lita moja. Zaidi soma jedwali la EWURA hapa chini kupata bei za mafuta kwa maeneo mengine nchini ; 

MAELEKEZO YA RAIS DK. SAMIA MRADI UJENZI MATENKI YA MAFUTA HAYA HAPA

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amezipa maelekezo maalum wizara na taasisi za Serikali akizitaka kuhakikisha Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam unatekelezwa kwa wakati na kukidhi viwango vya kimataifa. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, Machi 3, 2026. Ameiagiza pia Wizara ya Nishati, kuhakikisha inaimarisha miundombinu ya hifadhi ya mafuta na taifa linakuwa na akiba ya kutosha, ili kukabiliana na misukosuko ya bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia, huku akieleza kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani ni changamoto inayoongeza umuhimu wa kuwa na miundombinu madhubuti ya nishati. Rais Dk. Samia ametoa maelekezo hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati, Machi 3, 2026, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kwamba uwekezaji huo ni ha...