TRC yaanza kuunganisha injini za treni za reli ya MGR
-Yaweka historia Afrika Mashariki Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza kuunganisha injini za treni za reli ya Meter Gauge Railway (MGR) ndani ya nchi, hatua inayofanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki kutekeleza mpango huo. Hatua hiyo imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Wakati wa ziara ya ukaguzi wa mradi wa kuunganisha injini hizo katika Karakana ya Reli ya Pugu jijini Dar es Salaam leo Machi 14,2026, kamati hiyo imeishauri TRC kuendelea kuimarisha ujuzi wa vijana wa Kitanzania wanaoshiriki katika mradi huo kwa kuwapatia mafunzo ya juu ya kiufundi ndani na nje ya nchi. Mwenyekiti wa kamati hiyo,Selemani Kakoso, amesema kuwa uwekezaji katika kuendeleza taaluma za mafundi wazawa utasaidia kuongeza utaalamu wa kiufundi, ubunifu pamoja na ufanisi katika sekta ya reli nchini. Pia meiihimiza TRC kuweka kipaumbele katika kutoa ajira kwa vijana waliopata mafunzo hayo ili waendelee kuchangia maende...