Muhimbili yaitwa kuhudumia Jeshi Comoro
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika kile kinachoeweza kuelezwa kuendelea kupaa kwa ubora wa huduma za Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH), Jeshi la Comoro limeialika hospitali hiyo nchini humo na kuangalia uwezekano wa menejimenti na MNH kuanzisha huduma za kibingwa na bobezi nchini Comoro. Tayari uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umefanya ziara ya kikazi nchini Comoro kwa mwaliko wa jeshi hilo la Comoro, hatua inayotajwa ni maandalizi ya kuanzisha ushirikiano wa kimkakati kwenye huduma za Hospitali ya Jeshi na sekta ya afya kwa ujumla nchini Comoro. Mwaliko huo wa Jeshi la Comoro umeelezwa kuwa na lengo la kuanzisha ushirikiano utakaohusisha menejimenti ya hospitali, huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, uboreshaji wa vifaa tiba, tiba shirikishi, pamoja na maeneo mengine muhimu yatakayochangia kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma za afya kwa wanajeshi na raia wa Comoro. Kwenye ziara hiyo ujumbe wa MNH uliongozwa na Mkurugenzi wake Mtendaji wa Dk. Delilah Charles Ki...