Machapisho

Makamu wa Rais: Uhuru wa Mahakama ni dhamana ya haki, sio kinga ya uzembe

Picha
- Mahakama zageukia AI kuongeza ufanisi utoaji haki   Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua za makusudi katika kuimarisha uhuru wa Mahakama ili kuiwezesha kutekeleza wajibu wake kikamilifu na kuchochea ustawi na maendeleo ya Taifa ikitambua umuhimu wa Mahakama katika ujenzi wa Taifa. Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi Dk. Nchimbi pia ametoa rai kwa majaji na mahakimu akitaka uhuru wa Mahakama usitumike kama sehemu ya kuficha uzembe, upendeleo au vitendo visivyo vya haki na kwamba uhuru huo ni dhamana ya kutenda haki kwa uadilifu, uwazi na kwa kuzingatia Katiba na Sheria za nchi. Amesema hayo, alipomwakilisha Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, yaliyofanyika leo Februari 2,2026 Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tambukareli, Jijini Dodoma. “Serikali itaendelea kushirikiana na Mahakama katika ujenzi wa miundombinu ya Mahakama, kuimarisha rasili...

Nyenzo Kuu 3 Dira 2050 kuanza kuwasilishwa bungeni kesho

Picha
-Bunge kuzijadili kwa wiki nzima Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Taifa ya Mipango inatarajia kuwasilisha Nyenzo Kuu Tatu za kuanza utekelezaji wa Dira 2050, bungeni mjini Dodoma kesho Februari 2, 2026. Katibu Mtendaji wa NPC, Dk. Fred Msemwa Baada ya kuwasilishwa na kupokelewa, Bunge litazijadili kwa muda wa wiki moja kabla ya kutoa uamuzi wake kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Februari Mosi, 2026 Katibu Mtendaji wa NPC, Dk. Fred Msemwa ameeleza hayo akizitaja nyenzo hizo kuwa ni pamoja na Mpango Elekezi wa Muda Mrefu ambao ni wa miaka 25 kuanzia mwaka 2026/2027 hadi mwaka 20250/2051, Mpango Elekezi wa Miaka Mitano w mwaka 2026/2027-2030/2031 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2026/2027. “Nyenzo hizo zitawasilishwa bungeni na Serikali kupitia Waziri wa Nchi (Mipango na Uwekezaji) Profesa Kitila Mkumbo,” amesema Msemwa aliyekuwa akitoa taarifa kwa umma kuhusu maandalizi ya kuanza kwa u...

Matokeo Kidato cha nne 2025, haya hapa

Picha
  Mwandishi Wetu Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), limetangaza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne wa mwaka 2025, uliofanyika Novemba mwaka jana. Kwa matokeo ya kijana wako, binti yako, jamaa au wewe mwenyewe, fuata kiunganishi hapa chini;    https://matokeo.necta.go.tz/results/2025/csee/results/s4213.htm

Ndoto mabasi ya umeme Z'bar yatimia

Picha
 Ndoto imetimia, ndivyo unavyoweza kueleza, baada ya awamu ya kwanza ya mabasi ya Mradi wa Mabasi Yanayotumia Umeme (Zan Bus) kuwasili katika Bandari ya Malindi, Zanzibar. Kuwasil kwa mabasi hayo ya mradi unaoratibiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) na utasimamiwa na Kampuni ya Usafirishaji ya Unitrans kutoka Afrika Kusini ni kutimia kwa ndoto ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kupunguza taabu ya usafiri kwa wananchi. Mabasi hayo 10 yamawasili Januari 26, 2026  na kuelekea katika maegesho ya Stendi Mpya ya Kijangwani, Mkoa wa Mjini Magharibi  yakitarajiwa kuanza kutoa huduma rasmi za usafiri wa abiria mwezi ujao Februari. Hatua hiyo pia inalenga kupunguza msongamano wa magari barabarani pamoja na kuboresha usafiri rafiki wa mazingira Zanzibar. Mradi huo wa Zan Bus unaotarajiwa kuendelea kutekelezwa hatua kwa hatua  ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Nane ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein ...

NHC yaendelea kugusa maisha ya jamii: Wajasiriamali Kinondoni wapapatiwa mashine za uzalishaji

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeendelea kudhihirisha kwa vitendo dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kwa kukabidhi mashine ya kisasa ya kukamulia juisi kwa vikundi vya wajasiriamali wasioona katika wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam—hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuongeza thamani ya shughuli zao za uzalishaji. Watumishi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakishusha mashine ya kutengenezea juisi ya miwa kisha kuikabidhi kwa kikundi cha wajasiriamali wenye ulemavu wa macho Kinondoni, Dar es Salaam. Mashine hiyo imetolewa na NHC kuwasaidia wajasiriamali hao waweze kujikimu kimaisha. Akizungumza kwa niaba ya vikundi hivyo, Katibu Mkuu wa Chama cha Wasioona Kinondoni, Vitalis Mdoe, ameishukuru NHC kwa kuitikia ombi lao na kutoa msaada huo muhimu, akisema mashine hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa vikundi vinavyojihusisha na utengenezaji wa juisi kuongeza uzalishaji, ubora wa bidhaa na hatimaye kipato. "Tumesh...

NHC YAFIKISHA BUNGENI DIRA YA MAGEUZI, TEKNOLOJIA YA MAKAZI BORA

Picha
  - Utafiti na nyumba nafuu zatajwa suluhisho la baadaye - Kamati ya Bunge yataka utafiti kwa vifaa, teknolojia za kisasa kupunguza gharama za ujenzi - Enzi za Mwalimu Nyerere hadi Dira ya 2050, NHC yathibitisha uwezo wa taasisi za umma kujitegemea na kuleta tija. Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), limeweka wazi mkakati wake wa muda mfupi, wa kati na mrefu wa kuboresha upatikanaji wa makazi bora na ya gharama nafuu nchini mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, likisisitiza matumizi ya teknolojia za kisasa za ujenzi, utafiti wa kina wa vifaa mbadala pamoja na uendeshaji wa miradi kwa ufanisi wa kibiashara, unaolinda dhamira ya kijamii. Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, amebainisha hatua hizo wakati akiwasilisha taarifa ya Shirika hilo mbele ya Kamati ya Bunge, Januari 15, 2026 ambapo ameeleza kuwa NHC imejipanga kikamilifu kuendana na mahitaji ya sasa na ya baadaye ya Watanzania, kufuatana na Dira ya Taifa...

MBUNGE AFARIKI DUNIA, KUZIKWA LEO DAR

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mbunge wa Viti Maalum,Halima Idd Nassar amefariki dunia leo Jumapili Januari 18,2026 katika Hospitali ya Moyo ya Jakaya  Kikwete (JKCI), alipokuwa akipatiwa matibabu.  Marehemu Halima Idd Nassar Taarifa ya Bunge imemnukuu Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu akitangaza kifo hicho na kutoa pole kwa familia ya marehemu, wabunge, ndugu, jamaa na marafiki. Taarifa hiyo, imeeleza kuwa Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia, inaratibu mipango ya mazishi. Katika hatua nyingine, Ofisi ya Bunge imetoa tangazo linaloeleza kuwa marehemu Halima Idd Nassar atazikwa leo  saa 10 jioni katika makaburi ya Kibada kwa Dole Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Marehemu Halima, aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum akiwakilisha wafanyakazi, alikuwa mkazi wa Kigamboni, alizaliwa tarehe 12, Machi, mwaka 1980. Taarifa rasmi ya Ofisi ya Bunge soma hapa chini;