WABUNGE WA PIC WASHUHUDIA NHC ILIVYOTEKELEZA MIRADI SAMIA HOUSING, KAWE 711
- Waelezwa nyumba 560 zauzwa kabla ya kukamilika -NHC yaokoa Sh24 bilioni kwa kukopa Sh6 bilioni badala ya Sh30 bilioni - Mradi wazalisha ajira 1,800, uwanja wa michezo, soko kujengwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ukiangalia miradi ya Samia Housing Scheme Kawe na Kawe 711 inayotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC), utagundua kuwa haikuota kama uyoga, bali ni matokeo ya juhudi, nidhamu na usimamizi bora wa kazi zake, ambazo sasa zimeleta matokeo chanya. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah (aliyesimama mbele), akitoa maelezo kuhusu Mradi wa Samia Housing wa Kawe Dar es Salaam, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Serikali(PIC), iliyofanya ziara kwenye miradi ya NHC Machi 25,2026. Bila shaka, hali hiyo imempa nguvu na msukumo Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Hamad Abdallah, kuieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Serikali (PIC) kuwa jumla ya nyumba 560 zilizojengwa katika Mradi wa Samia Hou...