Machapisho

BEI MPYA KIKOMO YA PETROLI MWEZI MACHI 2026 HII HAPA

Picha
-Dar yauzwa 2,864, Katoro 3,124 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa, zitakazoanza kutumika  leo Machi 4,2026 saa 6 siku, huku bei ya chini ya petroli ikiwa kwa Sh2,864 kwa lita na dizeli Sh2,858 jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Dk. James Mwainyekule Kwa mujibu EWURA, bei kikomo ya juu ya petroli ni Sh3,124 na dizeli Sh 3119 Katoro mkoani Kagera, ambapo bei ya juu zaidi ya mafuta ya taa ni Sh3,193 Katoro, huku bei ya chini ni Sh2,932 kwa lita moja. Zaidi soma jedwali la EWURA hapa chini kupata bei za mafuta kwa maeneo mengine nchini ; 

MAELEKEZO YA RAIS DK. SAMIA MRADI UJENZI MATENKI YA MAFUTA HAYA HAPA

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amezipa maelekezo maalum wizara na taasisi za Serikali akizitaka kuhakikisha Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam unatekelezwa kwa wakati na kukidhi viwango vya kimataifa. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa Matanki ya Kupokelea na Kuhifadhi Mafuta eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, Machi 3, 2026. Ameiagiza pia Wizara ya Nishati, kuhakikisha inaimarisha miundombinu ya hifadhi ya mafuta na taifa linakuwa na akiba ya kutosha, ili kukabiliana na misukosuko ya bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia, huku akieleza kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani ni changamoto inayoongeza umuhimu wa kuwa na miundombinu madhubuti ya nishati. Rais Dk. Samia ametoa maelekezo hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati, Machi 3, 2026, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kwamba uwekezaji huo ni ha...

TAWA KANDA MAALUM DAR YAHIMIZA UHIFADHI WALIO HATARINI KUTOWEKA

Picha
-Yaadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani -Yaita wananchi kujionea vivutio vya mjini  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Uhifadhi Wanyamapori nchini (TAWA), Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo Machi 3, 2026, imeungana na wadau wengine wa sekta hiyo katika kuadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani, inayoadhimishwa Machi 3 kila mwaka, ikihimiza jamii kushiriki katika kulinda wanyama walio katika hatari ya kutoweka   kwa faida ya taifa leo na vizazi vijavyo. Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy  Kamanda wa Uhifadhi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Sylvester Mushy ametoa wito huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Machi 3, 2026   alipokuwa akizungumzia maadhimisho hayo yaliyobeba Kauli mbiu isemayo; ‘Mimea dawa, manukato, uhifadhi urithi na kuboresha maisha.’ Amesema kauli mbiu hiyo inahamasisha wananchi kutunza hifadhi wanyama pori na mimea, lakini pia TAWA imetumia siku hiyo kuwapa elimu na kuwahamasisha wananchi k...

PADRI MACHIBYA AWAKUMBUSHA WAKATOLIKI THAMANI YA UHAI

Picha
 Mwandishi Wetu, Waumini wa Kanisa Katoliki nchini wamekumbushwa kuwa uhai huanza na pumzi ya Mungu, na kuwataka kuutumia wakati huu wa kwaresma kukumbuka kwamba kila uhai ni pumzi iliyotoka kwa Mungu. Rai hiyo imetolwa na P adri Vedastus Machibula wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza,(Pichani Juu),  ambaye kwa sasa yuko Masomoni nchini Hispania, katika Tafakari yake ya Kwaresma ambapo amesema Yesu  Kristo alimwaga damu yake kwa ajili ya uhai, ili wanadamu kukombolewa. Kupitia ujumbe huo, amewahimiza waamini wa Kanisa Katoliki kuitazama Kwaresma kama wakati wa kutafakari kwa kina juu ya thamani ya uhai akieleza kuwa uhai ni zawadi takatifu kutoka kwa Mungu, inayopaswa kulindwa na kuheshimiwa katika kila hatua ya maisha ya Mwanadamu. Kwa mujibu wa mafundisho ya Kanisa Katoliki, uhai ni kitu Kitakatifu ambacho asili yake ni Mungu pekee,  tangu kutungwa mimba hadi kifo cha kawaida. Damu ya Yesu Kristo msalabani ni ishara ya upendo na uthibitisho wa thamani ya kila uhai kwa mwan...

NHC YACHORA RAMANI MPYA YA UFANISI NA UWAJIBIKAJI 2026/2027

Picha
- Faida ya Sh58.86 bilioni yatoa msukumo wa mageuzi ya kimfumo, kiutendaji -Waziri ataka kasi ya nyumba nafuu na uwekezaji wa kimkakati kuelekea AFCON 2027 -Baraza la Wafanyakazi lapitisha maazimio mazito ya mapato, mifumo na huduma -Serikali yataka nyumba nafuu, uwekezaji wa kimkakati na uwajibikaji zaidi  Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) uliofanyika jijini Arusha umeweka msingi imara wa hatua mpya za kiutendaji, uwazi na ukuaji endelevu unaolenga kuleta tija zaidi kwa shirika hilo. Mkutano huo wa mwanzoni mwa Februari 2026, umeibuka na maazimio mazito 23 yanayolenga kuimarisha mapato, mifumo ya utendaji na ustawi wa NHC kwa ujumla. Badala ya kuwa mkutano wa kawaida wa tathmini, kikao hicho kimekuwa jukwaa la kuweka mikakati mipya itakayolifanya Shirika la Nyumba la Taifa liendelee kuwa mhimili wa makazi bora nchini. Maazimio ya mageuzi na uwajibikaji Katika kujenga msingi wa ufanisi wa nda...

KARDINALI PENGO KUZIKWA PUGU FEBRUARI 28

Picha
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhasham Yuda Thadei Ruwa'ichi, ametangaza kwamba mazishi ya Askofu Mkuu Mstaafu wa jimbo hilo, hayati Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, yatafanyika Jumamosi ya Februari 28, mwaka 2026 katika makaburi ya Kituo cha Hija Pugu.  Ikumbukwe kuwa, enzi za uhai wake, hayati Kardinali Pengo alisema kuwa kaburi lake lipo Pugu na atafurahi tamanio lake hilo likitimizwa. Katika taarifa yake ya leo, Askofu Ruwa'ichi amesema siku ya Ijumaa Februari 27, saa 3 asbuhi, mwili wa hayati Kardinali Pengo utawasili viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ambapo heshima za mwisho zitatolewa. Ratiba hiyo inaonesha kuwa  siku hiyo saa 10 jioni itafanyika misa maalum ya kumuombea marehemu. Imeabinisha kwamba siku ya Jumamosi Februari 28 kianzia saa 1 kamili asubuhi hadi saa 3.45 heshima za mwisho zitatolewa kabla ya Ibada ya Mazishi kuanza saa 4 kamili asubuhi  kwenye Kituo cha Hija Pugu. Kwa mujibu wa Askofu Ruwai’ch...

Jamhuri 'yakwaa visiki' kesi ya kusafirisha 'unga'

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com UPANDE wa mashtaka katika kesi ya kusafirisha kilo 70.89 za 'unga' umekwaa kisiki, Mahakama imegoma kupokea notisi ya kuongeza vielelezo nane kwa sababu ina mapungufu. Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya imemtia uamuzi huo baada ya upande wa utetezi kuweka pingamizi maombi ya Jamhuri. Washtakiwa katika shauri hilo ni Sharifa Majani, Chigbo Innocent, Omari Omari na Mandela Masawe ambao wanashtakiwa kwa makosa manne. Shtaka la kwanza ilidaiwa kati ya Januari Mosi mwaka 2019 na Aprili 4,2023 maeneo ya Dar es Salaam, Pwani na Kilimanjaro waliandaa gengeni la uhalifu kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine. Shtaka la pili kwa mshtakiwa wa kwanza na wapili wanadaiwa Aprili 24,2023  maeneo ya Kiluvya wilayani Kisarawe walikutwa wakisafirisha kilo 25 za heroine. Shtaka la tatu kwa washtakiwa wote walidaiwa kati ya Aprili 20,2023 na Aprili 22, 2023 maeneo ya Kiluvya na Himo mkoani Kilimanjaro ...