Machapisho

PADRI MACHIBYA AWAKUMBUSHA WAKATOLIKI THAMANI YA UHAI

Picha
 Mwandishi Wetu, Waumini wa Kanisa Katoliki nchini wamekumbushwa kuwa uhai huanza na pumzi ya Mungu, na kuwataka kuutumia wakati huu wa kwaresma kukumbuka kwamba kila uhai ni pumzi iliyotoka kwa Mungu. Rai hiyo imetolwa na P adri Vedastus Machibula wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza,(Pichani Juu),  ambaye kwa sasa yuko Masomoni nchini Hispania, katika Tafakari yake ya Kwaresma ambapo amesema Yesu  Kristo alimwaga damu yake kwa ajili ya uhai, ili wanadamu kukombolewa. Kupitia ujumbe huo, amewahimiza waamini wa Kanisa Katoliki kuitazama Kwaresma kama wakati wa kutafakari kwa kina juu ya thamani ya uhai akieleza kuwa uhai ni zawadi takatifu kutoka kwa Mungu, inayopaswa kulindwa na kuheshimiwa katika kila hatua ya maisha ya Mwanadamu. Kwa mujibu wa mafundisho ya Kanisa Katoliki, uhai ni kitu Kitakatifu ambacho asili yake ni Mungu pekee,  tangu kutungwa mimba hadi kifo cha kawaida. Damu ya Yesu Kristo msalabani ni ishara ya upendo na uthibitisho wa thamani ya kila uhai kwa mwan...

NHC YACHORA RAMANI MPYA YA UFANISI NA UWAJIBIKAJI 2026/2027

Picha
- Faida ya Sh58.86 bilioni yatoa msukumo wa mageuzi ya kimfumo, kiutendaji -Waziri ataka kasi ya nyumba nafuu na uwekezaji wa kimkakati kuelekea AFCON 2027 -Baraza la Wafanyakazi lapitisha maazimio mazito ya mapato, mifumo na huduma -Serikali yataka nyumba nafuu, uwekezaji wa kimkakati na uwajibikaji zaidi  Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) uliofanyika jijini Arusha umeweka msingi imara wa hatua mpya za kiutendaji, uwazi na ukuaji endelevu unaolenga kuleta tija zaidi kwa shirika hilo. Mkutano huo umeibuka na maazimio mazito 23 yanayolenga kuimarisha mapato, mifumo ya utendaji na ustawi wa NHC kwa ujumla. Badala ya kuwa mkutano wa kawaida wa tathmini, kikao hicho kimekuwa jukwaa la kuweka mikakati mipya itakayolifanya Shirika la Nyumba la Taifa liendelee kuwa mhimili wa makazi bora nchini. Maazimio ya mageuzi na uwajibikaji Katika kujenga msingi wa ufanisi wa ndani, Baraza lilipitisha hatua ka...

KARDINALI PENGO KUZIKWA PUGU FEBRUARI 28

Picha
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhasham Yuda Thadei Ruwa'ichi, ametangaza kwamba mazishi ya Askofu Mkuu Mstaafu wa jimbo hilo, hayati Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, yatafanyika Jumamosi ya Februari 28, mwaka 2026 katika makaburi ya Kituo cha Hija Pugu.  Ikumbukwe kuwa, enzi za uhai wake, hayati Kardinali Pengo alisema kuwa kaburi lake lipo Pugu na atafurahi tamanio lake hilo likitimizwa. Katika taarifa yake ya leo, Askofu Ruwa'ichi amesema siku ya Ijumaa Februari 27, saa 3 asbuhi, mwili wa hayati Kardinali Pengo utawasili viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ambapo heshima za mwisho zitatolewa. Ratiba hiyo inaonesha kuwa  siku hiyo saa 10 jioni itafanyika misa maalum ya kumuombea marehemu. Imeabinisha kwamba siku ya Jumamosi Februari 28 kianzia saa 1 kamili asubuhi hadi saa 3.45 heshima za mwisho zitatolewa kabla ya Ibada ya Mazishi kuanza saa 4 kamili asubuhi  kwenye Kituo cha Hija Pugu. Kwa mujibu wa Askofu Ruwai’ch...

Jamhuri 'yakwaa visiki' kesi ya kusafirisha 'unga'

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com UPANDE wa mashtaka katika kesi ya kusafirisha kilo 70.89 za 'unga' umekwaa kisiki, Mahakama imegoma kupokea notisi ya kuongeza vielelezo nane kwa sababu ina mapungufu. Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi mbele ya Jaji Godfrey Isaya imemtia uamuzi huo baada ya upande wa utetezi kuweka pingamizi maombi ya Jamhuri. Washtakiwa katika shauri hilo ni Sharifa Majani, Chigbo Innocent, Omari Omari na Mandela Masawe ambao wanashtakiwa kwa makosa manne. Shtaka la kwanza ilidaiwa kati ya Januari Mosi mwaka 2019 na Aprili 4,2023 maeneo ya Dar es Salaam, Pwani na Kilimanjaro waliandaa gengeni la uhalifu kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine. Shtaka la pili kwa mshtakiwa wa kwanza na wapili wanadaiwa Aprili 24,2023  maeneo ya Kiluvya wilayani Kisarawe walikutwa wakisafirisha kilo 25 za heroine. Shtaka la tatu kwa washtakiwa wote walidaiwa kati ya Aprili 20,2023 na Aprili 22, 2023 maeneo ya Kiluvya na Himo mkoani Kilimanjaro ...

DC ampa siku 7 Kamishna wa Ardhi

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MKUU wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando amempa siku saba Kamishna wa Ardhi Kanda ya Dar es Salaam kumaliza mgogoro wa mipaka katika hati tatu za viwanja zenye mkanganyiko alizowapa wananchi Ubungo Kibangu. DC Msando amesema hayo alipotembelea eneo lenye mgogoro wa mipaka Ubungo Kibangu na kukutana na wenye nyumba ambao wana hati halali za kumiliki maeneo hayo. Wananchi wanaobishania mipaka katika maeneo yao ni Edgar Rweyemamu ambaye alipata hati Novemba 18 mwaka 2023 inayoonesha eneo la njia. Mwingine Edward Mkina ambaye hati alipata Novemba 20 mwaka 2023 ikionyesha eneo la njia na Monica Mujungu ambaye hati alipata mwaka jana ikionyesha katika eneo lake hakuna njia inayokatiza. Akielezea Monica amesema Mahakama ilielekeza apimiwe eneo lake, eneo lilipimwa akapewa hati  akajenga ukuta katika eneo hilo. ""Nilijenga ukuta Edgar akaubomoa, hati niliyopewa hakuna njia katika eneo langu,"amesema na kuhoji kama ilikuwa halali jirani yake k...

KARDINALI PENGO-MWAMBA WA IMANI, MAADILI ULIOLALA

Picha
-Atajwa shuhuda wa majadiliano kidini, kisiasa na kitamaduni   Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mwamba wa imani na maadili umelala. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Thadei Ruwa’ichi kutangaza kifo cha mtangulizi wake, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, akieleza kuwa ametwaliwa na Mungu usiku wa saa 4, Februari 19, mwaka 2026. Kwa mujibu wa Askofu Ruwai’chi, Kardinali Pengo ametwaliwa wakati akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dar es Salaam. “Ninayo masikitiko makubwa kuwatangazieni kwamba, leo 19/02/2026, saa 04.00 usiku huu, mpendwa baba yetu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele, akiwa katika Taaisisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), jijini Dar es Salaam,” amesema Askofu Ruwa’ichi katika taarifa yake. Taarifa hiyo imetolewa Kwenda kwa Mwadhama Kardinali Protas Rugambwa, Maaskofu wakuu wote, ...

TRC:USAFIRISHAJI MIZIGO SASA KWA CONTAINER CARRIERS SGR

Picha
-Mteja wa kwanza apata ofa Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza rasmi usafirishaji wa makasha kwa kutumia reli ya kisasa ya Standard Gauge (SGR) ikibeba makontena 100 kwa safari moja. Hatua hiyo inalenga kupanua wigo wa biashara nchini, kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na kurahisisha usafirishaji wa mizigo kwenda mikoa ya kati ya nchi. Kaimu Mkurugenzi wa Usafirishaji wa TRC, Focus Makoye Sahani, aliyezungumza wakati wa kuanza safari ya treni ya kwanza ya makasha kutoka Pugu Dar es Salaam kuelekea Ihumwa mkoani Dodoma, ameeleza kuwa treni hiyo inasafiri umbali wa takribani kilometa 420 kutoka Dar es Salaam. "Leo tumeongeza wigo wa biashara kwa kupakia makasha. Kama mnavyoona, treni yetu ya kwanza ya makasha kwenda Ihumwa, Dodoma, leo imeanza safari zake na tuna ofa ya kutosha kutoka kwa mteja wetu wa kwanza,” amesema Sahani. Amebainisha kwamba hatua hiyo ni mwanzo wa usafirishaji wa makasha baada ya TRC kuanza kusafirisha abiria pamo...