WAZIRI DK. AKWILAPO AWATANGAZIA 'VITA' WANAOHODHI ARDHI, AIPONGEZA NHC
-Atishia kutumia Sheria Namba 113 kunyang’anya waliokaa na viwanja bila kuviendeleza. -Ahimiza ujenzi wa nyumba nafuu kukabili upungufu wa nyumba milioni 3.8 Mwandhishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, ameanza kukunjua makucha, akieleza atawanyang’anya ardhi wote wanaohodhi bila kuziendeleza kwa muda mrefu, huku akilipongeza Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuendeleza maeneo inayomiliki kwa kujenga miradi mbalimbali, hata kuzalisha faida ya Sh bilioni 58 kwa mwaka uliopita 2025. Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC unaofanyika kwa siku tano kuanzia leo, Februari 11, 2026 jijini Arusha, Dk. Akwilapo, amesema anafikiria kuchukua hatua hiyo kwa kuzingatia sheria zilizopo. “Natafakari kutumia sheria yetu Namba 113 kifungu cha 49 kunyang’anya ardhi watu waliohodhi muda mrefu bila ya kuiendeleza. Maana sheria inataka mmiliki wa ardhi kuiendeleza sio kuihodhi. Wapo wanaohodh...