SIKU 100 ZA RAIS DK. SAMIA, NHC YAANDIKA HISTORIA MPYA
- Ahadi zageuka vitendo, NHC ikiimarisha sekta ya makazi -Mapato ya Bilioni 137.12, miradi yakamilika kwa kasi -Ubunifu wa kifedha, kidijitali waongeza ufanisi wa Serikali Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika uongozi wa kisiasa wa sasa, kipimo cha thamani ya Serikali si wingi wa ahadi kwa wananchi, bali ni uzito wa matokeo ya utekelezaji wake. Serikali hupimwa kwa vitendo vinavyoonekana na vinavyogusa maisha ya watu wake ndani ya muda husika. Ndani ya msingi huo ndipo unapopimwa pia utekelezaji wa ahadi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika siku 100 tangu kuanza kwa muhula wa pili wa Serikali ya Awamu ya Sita, mwaka 2025. Katika kipindi hicho kifupi, utekelezaji wa ahadi umejidhihirisha kama kioo kinachoakisi dira ya taifa, uongozi wenye uthubutu, maamuzi ya haraka na matokeo yanayoonekana wazi kwa Watanzania. Haikuwa hadithi ya takwimu pekee, bali simulizi ya uwajibikaji, ufanisi na matumaini mapya. Moja ya vielelezo vya mafanikio hayo ni sekt...