Machapisho

WAZIRI DK. AKWILAPO AWATANGAZIA 'VITA' WANAOHODHI ARDHI, AIPONGEZA NHC

Picha
-Atishia kutumia Sheria Namba 113 kunyang’anya waliokaa na viwanja bila kuviendeleza. -Ahimiza ujenzi wa nyumba nafuu kukabili upungufu wa nyumba milioni 3.8 Mwandhishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, ameanza kukunjua makucha, akieleza atawanyang’anya ardhi wote wanaohodhi bila kuziendeleza kwa muda mrefu, huku akilipongeza Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuendeleza maeneo inayomiliki kwa kujenga miradi mbalimbali, hata kuzalisha faida ya Sh bilioni 58 kwa mwaka uliopita 2025.   Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC unaofanyika kwa siku tano kuanzia leo, Februari 11, 2026 jijini Arusha, Dk. Akwilapo, amesema anafikiria kuchukua hatua hiyo kwa kuzingatia sheria zilizopo.   “Natafakari kutumia sheria yetu Namba 113 kifungu cha 49 kunyang’anya ardhi watu waliohodhi muda mrefu bila ya kuiendeleza. Maana sheria inataka mmiliki wa ardhi kuiendeleza sio kuihodhi. Wapo wanaohodh...

HINDU ANG’ARA NHC YAMTUZA KWA KUUZA NYUMBA NYINGI

Picha
- Mauzo ya nyumba 16 yambeba Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, amemtunuku cheti na tuzo ya Mfanyakazi Bora wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bi. Hindu Mwema kutoka Kurugenzi ya Uendelezaji Biashara NHC, kwa kutambua utendaji wake wa kipekee katika mauzo ya nyumba.   Akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NHC, Waziri alimpongeza Hindu kwa kuonesha kiwango cha juu cha uwajibikaji, ubunifu na ari binafsi, hatua iliyomwezesha kuuza nyumba 16, idadi inayozidi hata baadhi ya watendaji wa Idara ya Mauzo na Masoko.   “Mafanikio hayo ni ushahidi kuwa malengo ya NHC yanaweza kufikiwa pale ambapo mtumishi anafanya kazi kwa bidii na weledi,” amesema Dk. Akwilapo.   Amebainisha kuwa utambuzi wa watendaji bora ni mkakati wa kujenga ushindani chanya, kuongeza motisha na kuimarisha utamaduni wa uwajibikaji ndani ya taasisi za umma huku akiwataka wafanyakazi wengine kuiga mfano huo, il...

NHC YAELEKEZWA KUWEKEZA AFCON

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo(pichani), amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuwekeza jijini Arusha katika eneo la viwanja vitakavyotumika kwa Mashindano ya Kombe la Afrika(AFCON), mashindano yatakayofanyika mwakani 2027.   Mashindano hayo yatajumuisha uenyeji wan chi tatu ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda, ambapo Dk. Akwilapo amesema Serikali imeelekeza kila Wizara na taasisi za umma zifanye jambo kuwezesha ACON kuwa bora zaidi, ikiwezekana kuliko iliyofanyika Morocco na kumalizika mwaka huu 2026.   “Wizara ya Ardhi imepima maeneo kwenye eneo la AFCON, NHC iangalie namna ya kushiriki kwa kujenga na kuwekeza,”amesema Dk. Akwilapo na kuongeza: “Mimi napenda mambo ya   ‘Here and now’, (Hapa tulipo na sasa), natarajia NHC itafanya jambo kuwa na majengo yatakayofanikisha AFCON.”   Awali, akimkaribisha Waziri Dk. Akwilapo kuzungumza, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah,...

TAMICO YAPENDEKEZA MABORESHO HALI ZA WAFANYAKAZI NHC

Picha
  -Mkurugenzi Mkuu NHC ajibu unafanyiwa kazi ndani ya miezi 6 -Ataka TAMICO ichukue ya NHC kama mfano bora   Mwandishi Wetu, daimatzanews@gmail.com Chama cha Wafanyakazi wa Migodi, Nishati na Ujenzi (TAMICO), kimependekeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuufanyia maboresho Mkataba wa Hali Bora kwa Wafanyakazi wa shirika hilo uliopo kwa maslahi ya watumishi hao, huku Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah ikiahidi kufanyia kazi ndani ya miezi sita. Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa shirika hilo leo, Februari 11, 2026 jijini Arusha Ushauri huo umetolewa na Katibu Mkuu wa TAMICO Taifa, Partenus Rwechungura, alipokuwa akitoa salam za chama hicho cha wafanyakazi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC kwa mwaka 2026, unaofanyika jijini Arusha.   “Marejeo ya mkataba yanapaswa kuzingatia maboresho ya stahiki mbalimbali, ikiwemo posho za makazi (house allowance) na masuala mengine yanay...

Muhimbili yaitwa kuhudumia Jeshi Comoro

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika kile kinachoeweza kuelezwa kuendelea kupaa kwa ubora wa huduma za Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH), Jeshi la Comoro limeialika hospitali hiyo nchini humo na kuangalia uwezekano wa menejimenti na MNH kuanzisha huduma za kibingwa na bobezi nchini Comoro. Tayari uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umefanya ziara ya kikazi nchini Comoro kwa mwaliko wa jeshi hilo la Comoro, hatua inayotajwa ni maandalizi ya kuanzisha ushirikiano wa kimkakati kwenye huduma za Hospitali ya Jeshi na sekta ya afya kwa ujumla nchini Comoro. Mwaliko huo wa Jeshi la Comoro umeelezwa kuwa na lengo la kuanzisha ushirikiano utakaohusisha menejimenti ya hospitali, huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, uboreshaji wa vifaa tiba, tiba shirikishi, pamoja na maeneo mengine muhimu yatakayochangia kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma za afya kwa wanajeshi na raia wa Comoro. Kwenye ziara hiyo ujumbe wa MNH uliongozwa na Mkurugenzi wake Mtendaji wa Dk. Delilah Charles Ki...

Mkazi Kibangu 'amlilia' DC Ubungo utekeleaji amri ya mahakama

Picha
-Ni kuhusu mgogoro wa ardhi unaotishia mustakabali wake Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MKAZI wa Ubungo Kibangu, Monica Mujuni, ameiomba Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando(Pichani), kuhakikisha amri ya mahakama inaheshimiwa na mgogoro wa mipaka unaohusisha nyumba yake unatatuliwa haraka. Monica amesema anahitaji ufumbuzi wa dharura ili kurejesha sehemu ya ukuta wa nyumba yake uliobolewa na jirani yake, akisisitiza kuwa eneo hilo tayari lilishapimwa kisheria na ana hati halali ya umiliki. Akizungumza leo, Monica alisema mvutano huo ulianzia ngazi ya kata kabla ya kufika mahakamani, ambako alishinda kesi hiyo. Alieleza kuwa baada ya ushindi huo, maelekezo ya kupima eneo lake yalitekelezwa na ndipo alipopatiwa hati ya umiliki. “Eneo langu limepimwa, nina hati halali. Jirani yangu wa nyuma analazimisha kupita katika uwani kwangu. Usiku alibomoa sehemu ya ukuta wangu na akaweka geti upande wa kwake likielekea kwangu, katika sehemu aliyoharibu,” alisema Monica. Am...

Makamu wa Rais: Uhuru wa Mahakama ni dhamana ya haki, sio kinga ya uzembe

Picha
- Mahakama zageukia AI kuongeza ufanisi utoaji haki   Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua za makusudi katika kuimarisha uhuru wa Mahakama ili kuiwezesha kutekeleza wajibu wake kikamilifu na kuchochea ustawi na maendeleo ya Taifa ikitambua umuhimu wa Mahakama katika ujenzi wa Taifa. Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi Dk. Nchimbi pia ametoa rai kwa majaji na mahakimu akitaka uhuru wa Mahakama usitumike kama sehemu ya kuficha uzembe, upendeleo au vitendo visivyo vya haki na kwamba uhuru huo ni dhamana ya kutenda haki kwa uadilifu, uwazi na kwa kuzingatia Katiba na Sheria za nchi. Amesema hayo, alipomwakilisha Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, yaliyofanyika leo Februari 2,2026 Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tambukareli, Jijini Dodoma. “Serikali itaendelea kushirikiana na Mahakama katika ujenzi wa miundombinu ya Mahakama, kuimarisha rasili...