TRC:USAFIRISHAJI MIZIGO SASA KWA CONTAINER CARRIERS SGR
-Mteja wa kwanza apata ofa Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza rasmi usafirishaji wa makasha kwa kutumia reli ya kisasa ya Standard Gauge (SGR) ikibeba makontena 100 kwa safari moja. Hatua hiyo inalenga kupanua wigo wa biashara nchini, kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na kurahisisha usafirishaji wa mizigo kwenda mikoa ya kati ya nchi. Kaimu Mkurugenzi wa Usafirishaji wa TRC, Focus Makoye Sahani, aliyezungumza wakati wa kuanza safari ya treni ya kwanza ya makasha kutoka Pugu Dar es Salaam kuelekea Ihumwa mkoani Dodoma, ameeleza kuwa treni hiyo inasafiri umbali wa takribani kilometa 420 kutoka Dar es Salaam. "Leo tumeongeza wigo wa biashara kwa kupakia makasha. Kama mnavyoona, treni yetu ya kwanza ya makasha kwenda Ihumwa, Dodoma, leo imeanza safari zake na tuna ofa ya kutosha kutoka kwa mteja wetu wa kwanza,” amesema Sahani. Amebainisha kwamba hatua hiyo ni mwanzo wa usafirishaji wa makasha baada ya TRC kuanza kusafirisha abiria pamo...