Rostam Aziz ainunua NMG ya Kenya inayozalisha magazeti ya Daily Nation
- Arejea kwenye umiliki wa vyombo vya habari Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mfanyabishara bilionea wa Tanzania, Rostam Azizi amenunua asilimia 100 ya hisa za Shirika la Aga Khan Fund for Economic Development S.A ( AKFED ) , katika Kampuni ya Nation Media Group PLC ( NMG ), yenye makao makuu yake nchini Kenya, inayozalisha magazeti ya Daily Nation na kumiliki vituo mbalimbali vya redio na televisheni ukanda wa Afrika Mashariki. Mtukufu Prince Rahim Aga Khan V (kulia) na mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Azizi. Picha kwa hisani ya Mtandao wa Daily Nation. Bila ya kutaja thamani ya hisa, taarifa iliyotolewa leo Machi 10,2026 na AKFED imeeleza umiliki wake ul ikuwa asilimia 54.08 ya hisa zote za NMG, ambazo sasa ni mali ya Rostam chini ya Taarifa Ltd , kampuni inayomilikiwa na mfanyabiashara huyo wa Tanzania. . Uamuzi huo wa Rostam kununua NMG, unamrejesha mfanyabiashara huyo bilionea wa Tanzania katika biashara, umiliki na uendeshaji wa vy...