Machapisho

Muhimbili yaitwa kuhudumia Jeshi Comoro

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katika kile kinachoeweza kuelezwa kuendelea kupaa kwa ubora wa huduma za Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH), Jeshi la Comoro limeialika hospitali hiyo nchini humo na kuangalia uwezekano wa menejimenti na MNH kuanzisha huduma za kibingwa na bobezi nchini Comoro. Tayari uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umefanya ziara ya kikazi nchini Comoro kwa mwaliko wa jeshi hilo la Comoro, hatua inayotajwa ni maandalizi ya kuanzisha ushirikiano wa kimkakati kwenye huduma za Hospitali ya Jeshi na sekta ya afya kwa ujumla nchini Comoro. Mwaliko huo wa Jeshi la Comoro umeelezwa kuwa na lengo la kuanzisha ushirikiano utakaohusisha menejimenti ya hospitali, huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, uboreshaji wa vifaa tiba, tiba shirikishi, pamoja na maeneo mengine muhimu yatakayochangia kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma za afya kwa wanajeshi na raia wa Comoro. Kwenye ziara hiyo ujumbe wa MNH uliongozwa na Mkurugenzi wake Mtendaji wa Dk. Delilah Charles Ki...

Mkazi Kibangu 'amlilia' DC Ubungo utekeleaji amri ya mahakama

Picha
-Ni kuhusu mgogoro wa ardhi unaotishia mustakabali wake Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MKAZI wa Ubungo Kibangu, Monica Mujuni, ameiomba Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando(Pichani), kuhakikisha amri ya mahakama inaheshimiwa na mgogoro wa mipaka unaohusisha nyumba yake unatatuliwa haraka. Monica amesema anahitaji ufumbuzi wa dharura ili kurejesha sehemu ya ukuta wa nyumba yake uliobolewa na jirani yake, akisisitiza kuwa eneo hilo tayari lilishapimwa kisheria na ana hati halali ya umiliki. Akizungumza leo, Monica alisema mvutano huo ulianzia ngazi ya kata kabla ya kufika mahakamani, ambako alishinda kesi hiyo. Alieleza kuwa baada ya ushindi huo, maelekezo ya kupima eneo lake yalitekelezwa na ndipo alipopatiwa hati ya umiliki. “Eneo langu limepimwa, nina hati halali. Jirani yangu wa nyuma analazimisha kupita katika uwani kwangu. Usiku alibomoa sehemu ya ukuta wangu na akaweka geti upande wa kwake likielekea kwangu, katika sehemu aliyoharibu,” alisema Monica. Am...

Makamu wa Rais: Uhuru wa Mahakama ni dhamana ya haki, sio kinga ya uzembe

Picha
- Mahakama zageukia AI kuongeza ufanisi utoaji haki   Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua za makusudi katika kuimarisha uhuru wa Mahakama ili kuiwezesha kutekeleza wajibu wake kikamilifu na kuchochea ustawi na maendeleo ya Taifa ikitambua umuhimu wa Mahakama katika ujenzi wa Taifa. Makamu wa Rais Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi Dk. Nchimbi pia ametoa rai kwa majaji na mahakimu akitaka uhuru wa Mahakama usitumike kama sehemu ya kuficha uzembe, upendeleo au vitendo visivyo vya haki na kwamba uhuru huo ni dhamana ya kutenda haki kwa uadilifu, uwazi na kwa kuzingatia Katiba na Sheria za nchi. Amesema hayo, alipomwakilisha Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, yaliyofanyika leo Februari 2,2026 Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tambukareli, Jijini Dodoma. “Serikali itaendelea kushirikiana na Mahakama katika ujenzi wa miundombinu ya Mahakama, kuimarisha rasili...

Nyenzo Kuu 3 Dira 2050 kuanza kuwasilishwa bungeni kesho

Picha
-Bunge kuzijadili kwa wiki nzima Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Taifa ya Mipango inatarajia kuwasilisha Nyenzo Kuu Tatu za kuanza utekelezaji wa Dira 2050, bungeni mjini Dodoma kesho Februari 2, 2026. Katibu Mtendaji wa NPC, Dk. Fred Msemwa Baada ya kuwasilishwa na kupokelewa, Bunge litazijadili kwa muda wa wiki moja kabla ya kutoa uamuzi wake kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Februari Mosi, 2026 Katibu Mtendaji wa NPC, Dk. Fred Msemwa ameeleza hayo akizitaja nyenzo hizo kuwa ni pamoja na Mpango Elekezi wa Muda Mrefu ambao ni wa miaka 25 kuanzia mwaka 2026/2027 hadi mwaka 20250/2051, Mpango Elekezi wa Miaka Mitano w mwaka 2026/2027-2030/2031 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2026/2027. “Nyenzo hizo zitawasilishwa bungeni na Serikali kupitia Waziri wa Nchi (Mipango na Uwekezaji) Profesa Kitila Mkumbo,” amesema Msemwa aliyekuwa akitoa taarifa kwa umma kuhusu maandalizi ya kuanza kwa u...

Matokeo Kidato cha nne 2025, haya hapa

Picha
  Mwandishi Wetu Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), limetangaza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne wa mwaka 2025, uliofanyika Novemba mwaka jana. Kwa matokeo ya kijana wako, binti yako, jamaa au wewe mwenyewe, fuata kiunganishi hapa chini;    https://matokeo.necta.go.tz/results/2025/csee/results/s4213.htm

Ndoto mabasi ya umeme Z'bar yatimia

Picha
 Ndoto imetimia, ndivyo unavyoweza kueleza, baada ya awamu ya kwanza ya mabasi ya Mradi wa Mabasi Yanayotumia Umeme (Zan Bus) kuwasili katika Bandari ya Malindi, Zanzibar. Kuwasil kwa mabasi hayo ya mradi unaoratibiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) na utasimamiwa na Kampuni ya Usafirishaji ya Unitrans kutoka Afrika Kusini ni kutimia kwa ndoto ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kupunguza taabu ya usafiri kwa wananchi. Mabasi hayo 10 yamawasili Januari 26, 2026  na kuelekea katika maegesho ya Stendi Mpya ya Kijangwani, Mkoa wa Mjini Magharibi  yakitarajiwa kuanza kutoa huduma rasmi za usafiri wa abiria mwezi ujao Februari. Hatua hiyo pia inalenga kupunguza msongamano wa magari barabarani pamoja na kuboresha usafiri rafiki wa mazingira Zanzibar. Mradi huo wa Zan Bus unaotarajiwa kuendelea kutekelezwa hatua kwa hatua  ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Nane ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein ...

NHC yaendelea kugusa maisha ya jamii: Wajasiriamali Kinondoni wapapatiwa mashine za uzalishaji

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeendelea kudhihirisha kwa vitendo dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kwa kukabidhi mashine ya kisasa ya kukamulia juisi kwa vikundi vya wajasiriamali wasioona katika wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam—hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuongeza thamani ya shughuli zao za uzalishaji. Watumishi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakishusha mashine ya kutengenezea juisi ya miwa kisha kuikabidhi kwa kikundi cha wajasiriamali wenye ulemavu wa macho Kinondoni, Dar es Salaam. Mashine hiyo imetolewa na NHC kuwasaidia wajasiriamali hao waweze kujikimu kimaisha. Akizungumza kwa niaba ya vikundi hivyo, Katibu Mkuu wa Chama cha Wasioona Kinondoni, Vitalis Mdoe, ameishukuru NHC kwa kuitikia ombi lao na kutoa msaada huo muhimu, akisema mashine hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa vikundi vinavyojihusisha na utengenezaji wa juisi kuongeza uzalishaji, ubora wa bidhaa na hatimaye kipato. "Tumesh...