Ada Cottrell yawasaidia watoto wenye mahitaji Zanzibar

 Mwandishi Wetu, Zanzibar

Taasisi ya Ada Cottrell Foundation kwa kushirikiana na Taasisi ya Labayka Development Foundation (LDF), imetoa msaada kwa watoto wanaoishi kwenye mazingila magumu ili kuwawezesha kujikimu kwa mahitaji yao.

Baadhi ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu eneo la Nungwi Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa msaada kutoka taasisi ya Ada Cottrell Foundation ya Marekani kwa kushirikiana na Taasisi ya Labayka Development Foundation (LDF) ikiwa ni sehemu ya kumuenzi marehemu Robert Cottrell.

Msaada huo umetolewa kwa Watoto hao walio katika Kata ya Nungwi, Kijiji cha Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A na Mkoa wa Kaskazini Unguja, visiwani  Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi msaada huo, Mkurungezi Muwakilishi wa taasisi ya Ada Cottrell Foundation, Shedrack Gabriel Albert amesema hatua hiyo ni mwendelezo wa utaratibu unaofanywa kila mwaka na taasisi hiyo, ikiwa ni kumbukizi ya Marehemu Robert Cottrell, raia ya Marekani kila ifikapo Agosti kwa kuwa ndio mwezi aliofariki.

Robart ambaye alikua ni Daktari nchini Marekani alifariki dunia Agosti 2018 kwa ugonjwa wa saratani na ameacha mke, Joyce  Cottrell na mtoto wa kike, Ada Cottrell ambaye ndiye msimamizi wa taasisi ya Ada Cottrell Foundation ya Marekani na tawi lake kwa sasa lipo nchini Tanzania.

Hata hivyo, Shedrack amesema pamoja na msaada ukliotolewa na taasisi yake, visiwa vya Unguja bado vinakabiliwa na changamoto ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, hivyo bado wanahitaji msaada zaidi.

Akizungumza  baada ya Watoto hao kukabidhiwa msaada huo, mwenyeji wa Taasisi ya Ada Cottrell, Khamis Juma Mtwana kutoka taasisi   ya Labayka Development Foundation(LDF), iliyopo Nungwi ameahidi kushirikiana vyema kuhakikisha wanapunguza tatizo la watoto wenye uhitaji mjini humo.

Watoto wanaoishi katika mazingira magumi Nungwi mjini Zanzibar, wakiwa katika pia ya pamoja na watendaji wa taasisi za Ada Cottrell Foundation ya Marekani kwa kushirikiana na Taasisi ya Labayka Development Foundation (LDF) ambao walitoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto hao.

Pamoja na ugawaji wa mahitaji hayo pia ilifanyika dua maalum ya kumuombea Robart Cottrell ikiwa sehemu ya kumbukumbu yake, iliyoongozwa na Sheikh Apite Haji Ali, Jinala.

 

 

 

  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi