-Maajabu mapya ya kipekee Exuperius Kachenje Sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria (Mariam), anayetajwa na vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu na Qur’an Tukufu (Mariam), ndiye mama wa Yesu Kristo (Nabii Issa bin Mariam), imegundulika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Saadani, ikitajwa kuwa ni maajabu mapya yasiyo ya kawaida kwa watalii ndani na nje ya Tanzania, inayoongeza upekee wa hifadhi hiyo kwa utalii. Mti wa mbuyu wenye sanamu yenye mwonekano wa Bikira Maria uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadan. Picha na Exuperius Kachenje Ofisa Mhifadhi kitengo cha uta;ii, Hifadhi ya Taifa Saadani (SANAPA) Daud Gordon amebainisha hayo Juni 26, 2025 akieleza kwamba kivutio hicho kipya ni nyenzo muhimu katika kukuza utalii wa kiimani, hata kuweza kuwa sehemu ya hija kwa waamini, hasa wanaoamini na kumheshimu mama huyo kadiri ya mapokeo ya imani zao,mfano ukiwa Kanisa Katoliki. Gordon amesema kuwa sanamu hiyo ya asili inaonekana katikati ya mti wa mbuyu, eneo la Buyuni ndani ya h...
- Aichagua JKCI kupata huduma za kibingwa - Burkina Faso yasaini makubaliano na JKCI Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais wa Burkina Faso,Kapteni Ibrahim Traore amefuata huduma bora za afya zinazotolewa nchini, hasa za magonjwa ya moyo. Rais wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traore Ndivyo unavyoweza kueleza, baada kiongozi huyo maarufu duniani,kutuma mwakilishi wake wa masuala ya afya Burkina Faso nchini kuzungumza na kutiliana saini hati ya makubaliano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), katika kutoa huduma bobezi ya matibabu ya magonjwa ya moyo. Kwa mujibu wa JKCI, hati hizo zimesainiwa kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dk. Peter Kisenge na Mshauri wa Rais wa Burkina Faso na Mratibu wa Kitaifa wa Mpango wa Afya wa Rais, Drissa Traore, jana jijini Dar es Salaam. Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo, Dk. Kisenge amesema makubaliano hayo yataimarisha utoaji wa huduma za matibab...
Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Tanzania imepiga hatua isiyosahaulika katika historia ya maendeleo yake, baada ya kikosi cha wawekezaji wa ngazi ya juu kutoka Ufalme wa Oman, kufanya ziara nchini na kukutana na uongozi wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), wakifungua fursa kubwa za mabadiliko makubwa katika sekta ya nyumba na maendeleo ya miji nchini. Ujumbe wa Wawekezaji kutoka Oman(kulia) ukiwa katika mkutano na uongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), (kushoto), makao makuu ya shirika hilo jijini Dar es Salaam Mei 20,2024. Ujumbe huo uliongozwa na Balozi wa Oman nchini Tanzania, Saud Al Shidha, ulikuwa na malengo kadhaa ya kukuza ushirikiano wa kiuchumi ikiwamo kuanzisha mabadiliko ya kimkakati, yatakayochochea ukuaji wa sekta ya makazi kwa njia ya ubia wa kimataifa. Katika kikao cha kihistoria kilichofanyika Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) – Kambarage House, ujumbe wa Oman ulipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, pamoja na viongozi waandamizi w...
Maoni
Chapisha Maoni