M-PESA SASA MIAKA 18; SHUJAA ANAYEWAKOMBOA WATANZANIA
- Vodacom Tanzania yaimarisha ukuaji M-Pesa sasa yawekeza Dola milioni 28 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Kwa kawaida mtoto anapotimiza umri wa miaka 18 hutazamwa kwa matumaini mapya, makubwa zaidi ya kuivusha familia au jamii husika kutoka ilipokuwa awali kwenda juu zaidi katika kufanikiwa kimaendeleo. Hali hiyo huwezi kuitenganisha, bali kuifananisha na huduma ya M-Pesa, inayotolewa na Kampuni ya Vodacom Tanzania, ambayo inatimiza miaka 18 ya huduma zake nchini, Aprili hii 2026, ikiwa na nguvu zaidi na nafasi kubwa zaidi ya kuchagiza maendeleo ya Watanzania, wanaotumia huduma ya M-Pesa kupitisha miamala ya fedha kwa madhumuni mbalimbali. Hakika katika miaka 18 ya M-Pesa kuhudumia Watanzania, Vodacom Tanzania inaonesha ukomavu wake, ambapo sasa imeingia hatua mpya kwa kufanya uwekezaji mkubwa wa Dola za Marekani milioni 28 takriban Sh75.6 bilioni. Uwekezaji huo unalenga kuimarisha zaidi jukwaa hilo la kidijitali na kuhakikisha linaendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidiji...