Uhamiaji yatimua wawili nchini

 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Idara ya Uhamiaji nchini imewafukuza nchini raia wawili wa kigeni, Mmarekani mmoja na Mjerumani mmoja, ikieleza hatua hiyo imetoka na wawili hao kukiuka masharti ya viza zao za matembezi.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Anna Makakala

Taarifa iliyotolewa leo na Uhamiaji imewataja raia hao kuwa ni Dk. Brinkel Stefanie mwenye hati ya kusafiria ya Ujerumani na Catherine Janel Amquist Kinokfu, mwenye hati ya kusafiria ya Marekani.

Uhamiaji imewataka raia wote wa kigeni wanaoingia nchini kwa madhumuni mbalimbali, kuzingatia matakwa yanayoainishwa katika viza au vibali vyao kuingia nchini.


 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi