Mambo mapya saba, Sabasaba 2024
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Ni msimu wa Maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba, safari hii yakiwa ni ya 48 tangu kuanzishwa kwake, yakiendeshwa na kuratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), ambapo kwa mwaka huu ykuna mambo saba tofauti, mapya yanayobeba maonyesho hayo ikiwamo matumizi ya robot (akili bandia (IA). Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis Katika mahojiano, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis ameeleza kuwa maonyesho ya mwaka huu ni tofauti na miaka mingine, kutokana na ukweli kwamba yanabebwa na mambo saba tofauti. āMaonyesho ya mwaka huu yana sura ya kipekee, tuna bidhaa za kitanzania halisia, tuna nchi za kigeni zaidi ya 25 zinashiriki, tuna mabanda manne ya kimataifa, tuna nchi zaii ya sita zitahimisha siku za mataifa yao kwa mwaka 2024 kipindi cha maonyesho, tiketi za Sabasaba mwaka huu zipo kwa mtandao; Pia tutawadhamini wafanyabiashara wa Kariakoo ili waweze kuuza bidhaa za jumla kutoka kwa washi...