Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2024

Mambo mapya saba, Sabasaba 2024

Picha
  Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Ni msimu wa Maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba, safari hii yakiwa ni ya 48 tangu kuanzishwa kwake, yakiendeshwa na kuratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara  Tanzania  (Tan Trade), ambapo kwa mwaka huu ykuna mambo saba tofauti, mapya yanayobeba maonyesho hayo ikiwamo matumizi ya robot (akili bandia (IA). Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis Katika mahojiano, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis ameeleza kuwa maonyesho ya mwaka huu ni tofauti na miaka mingine, kutokana na ukweli kwamba yanabebwa na mambo saba tofauti. ā€œMaonyesho ya mwaka huu yana sura ya kipekee, tuna bidhaa za kitanzania halisia, tuna nchi za kigeni zaidi ya 25 zinashiriki, tuna mabanda manne ya kimataifa, tuna nchi zaii ya sita zitahimisha siku za mataifa yao kwa mwaka 2024 kipindi cha maonyesho, tiketi za Sabasaba mwaka huu zipo kwa mtandao; Pia tutawadhamini wafanyabiashara wa Kariakoo ili waweze kuuza bidhaa za jumla kutoka kwa washi...

Nape: Wadau naomba tuaminiane

Picha
Selemani Msuya, daimatznews@gmail.com WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amewaomba wadau wa sekta ya habari kuwa na imani naye kuhusu vifungu 12 vinavyolalamikiwa katika Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016. Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye Kauli hiyo ya Waziri Nape imetokana na maazimio sita yaliyosomwa na Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Thobias Makoba, ambapo moja ya azimio lilikuwa ni vifungu 12 vya Sheria ya Huduma ya Habari ambavyo vinalalamikiwa na wadau wa sekta hiyo. Nape ametoa kauli hiyo wakati akifunga Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari lilifoanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam kwa siku mbili na kushirikisha wadau zaidi 1,200 kutoka sekta umma na binafsi kwenye tasnia ya habari. "Nitatoa mfano, hoja ya umiliki wa vyombo vya habari, ipo kwenye Sera ya Vyombo vya Habari ya mwaka 2003, mimi sikuwepo, nilikuwa ndio naanza kazi CCM. Jamani nao...

Msikiti 'mikononi' mwa RITA Arusha

Mwandishi Wetu, Arusha WAKALA wa Usajili Ufilisi na Udhamini nchini (RITA), umeunda kamati ya muda itakayochukua majukumu  ya Bodi ya Udhamini iliyomaliza muda wake ya Taasisi ya Arusha Muslim. Sanjari na hatua hiyo, RITA imeunda Kamati ya Maalumu ya Uchunguzi itakayofuatilia malalamiko ya wanachama, kuwatuhumu viongozi wa msikiti huo kuhujumu mali za  taasisi hiyo. Akizitambulisha kamati hizo katika kikao kilichojumuisha uongozi wa RITA, viongozi wa Serikali ya Wilaya ya  Arusha, viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA ), viongozi wa Arusha Muslim pamoja na wanachama wa msikiti huo, Kabidhi Wasii  Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Frank Kanyusi ameziagiza kamati hizo kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu.  ā€œNimeiagiza Bodi iliyomaliza muda wake kuwasilisha RITA taarifa ya mapato na matumizi,ā€ amesema Kanyusi na kuiagiza kamati ya mpito kuhakikisha inafanya marekebisho ya katiba na uchaguzi unafanyika ndani ya siku 60, ili kupata viongoz...

INEC: Wanasiasa someni Sheria ya Uchaguzi msipotoshe wananchi

Na Selemani Msuya  WAKATI vyama vya siasa vikiitaka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), isimamie uchaguzi wa serikali za mitaa, tume hiyo imevishauri vyama hivyo vikasome Kifungu cha 10 (1) (C) cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, ili viache kupotosha wananchi. Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa INEC, Ramadhan Kailima wakati akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya kwanza kwa waandishi wa habari 250 leo Juni 13, jijini Dar es Salaam. Kailima amesema kumekuwa na muendelezo wa viongozi wa vyama vya siasa kuitaka INEC isimamie uchaguzi wa serikali za mitaa, kwa hoja kwamba Sheria ya Tume ya Huru ya Taifa ya Uchaguzi inataka hivyo, jambo ambalo sio kweli. "Waandishi wa habari nyie ni watu muhimu sana kwenye mchakato wote wa uchaguzi, sisi INEC, wanasiasa na wananchi wanawategemea mtoe bahari zenye usahihi, naomba hili la wanasiasa kutaka sisi tusimamie uchaguzi mliandike kwa usahihi kwani kwa sheria iliyopo sasa hatuna...

Dar mpaka Moro moto SGR abiria kuanza safari kesho

Picha
  Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Dar mpaka Moro, hayawi, hayawi, sasa yamekuwa. Tanzania inaandika historia mpya katika nyanja ya usafiri na usafirishaji Saa12 kamili ya Juni 14, 2024, ambapo Treni ya Mwendokasi (SGR) inayotumia umeme, ikianza safari zake kwa kubeba abiria kibiashara. Treni ya Umeme ya SGR Treni hiyo itaanza safari zake, kabla ya muda uliopangwa wa Julai mwaka huu kufika, ambapo itaanza kwa safari za Dar es Salaam kwenda Morogoro. Nauli kwa abiria mmoja kwa kila safari ni Sh13,000 mtu mzima huku watoto wenye umri zaidi ya miaka minne wakitakiwa kulipa nusu ya nauli ya mtu mzima. Daima Tanzania blog, ilikuwepo kwenye kituo kikuu cha treni hiyo maeneo ya Steshen", ambapo ilishuhudia maandalizi ya mwisho yakiendelea, huku wananchi waliojaa bashasha, wakiingia na kuulizia upatikanaji wa tiketi. Hata hivyo, walielezwa kuwa wanaweza kupata titeki hizo kupitia mtandao wa TRC au wawahi kufika kituoni hapo kabla ya muda wa safari. Ratiba iliyotolewa na S...

VAR kutumika Ligi Kuu msimu ujao

Picha
 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, amelifahamisha Bunge la Jamhuri ya Muungano kuwa msimu ujao Ligi Kuu Tanzania, itaanza kutumia VAR. Mashine ya VAR VAR ni mfumo wa usaidizi kwa waamuzi wanapochezesha soka uwanjani kutumia 'video'. Dk. Nchemba ametoa maelezo hayo wakati akiwasilisha hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2024/2025 bungeni, mjini Dodoma leo, ambapo amesema lengo la kutumia mfumo huo ni kuhakikisha matokeo yanayopatikana yanakuwa ya haki. "Msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania, tutaanza kutumia ''VAR'' ili kuhakikisha matokeo yanayopatikana uwanjani yanakuwa ya haki ,"amesema Dk.Mwigulu na kuongeza: "Maana kuna timu zimezidi - msimu mmoja penati 10, halafu zikifungwa zenyewe magoli yanakataliwa." Waziri wa Fedha, amesema kuwa ili kuwepo na ''VAR'' za kutosha katika viwanja vyote, anapendekeza  Bunge litoe msamaha kwenye uingizaji wa mashine hizo na vifaa vyake. ...

Bajeti; Malengo yake saba kiuchumi ni haya

Picha
 Exuperius Kachenje,daimatznews@gmail.com Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, ametaja shabaha saba za uchumi kwa jumla katika bajeti yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025. Begi la Bajeti ya Serikali mwaka 2024/2025 Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2024/25, bungeni mjini Dodoma leo Juni 13, 2024, Dk. Mwigulu amesema shabaha hizo zimetokana na nyaraka na miongozo iliyozingayowa katika uandaaji bajeti hiyo.  "Shabaha za uchumi jumla ni saba kama ifuatavyo; Kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa kufikia asilimia 5.4 mwaka 2024 kutoka ukuaji wa asilimia 5.1 mwaka 2023; Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0 - 5.0 katika muda wa kati," amesema Dk Mwigulu. Nyingine ni mapato ya ndani kufikia asilimia 15.8 ya Pato la Taifa mwaka 2024/25 ikilinganishwa na matarajio ya asilimia 15.4 mwaka 2023/24; Mapato ya kodi kufikia asilimia 12.9 ya Pato la Taifa mwaka 2...

Kikokotoo sasa asilimia 40, Rais awapoza wastaafu

Picha
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Serikali imesikia kilio cha wastaafu kuhusu kikotoo, ikitangaza kwamba malipo ya mkupuo sasa yatakuwa ni asilimia 40 kutoka 33 ya awali kuanzia mwaka ujao wa fedha. Uamuzi huo wa Serikali umetangazwa bungeni mjini Dodoma leo Juni 13, 2024 na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba (pichani juu) , alipokuwa akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025. ā€œSerikali imesikia kilio cha watumishi na kufanyia kazi suala la masilahi..., Rais Samia ameelekeza kuongezeka kwa malipo ya mkupuo....;  "Wastaafu waliokuwa wakipokea asilimia 25 hadi 33 kwa malipo ya mkupuo, sasa watapandishwa hadi asilimia 35 na walioathirika na mabadiliko yaliyojitokeza watakuwa sehemu ya mabadiliko hayo," amesema Mwigulu na kuongeza: ā€œSerikali itaendelea kuliangalia kwa karibu suala la masilahi ya wastaafu kwa kuzingatia tathmini ya uhai na uendelevu wa mifuko yetu.ā€  Hatua hiyo ya Serikali inagusa watumishi walioshushiwa malipo ya mkupuo kutoka asi...

Serikali yatoa msimamo Sekta ya Posta Afrika

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha Serikali ya Tanzania imeuhakikishia Umoja wa Posta Afrika (PAPU), msimamo wake usioyumba kwamba, itaendelea kuunga mkono na kusaidia mikakati ya umoja huo kwa maendeleo ya Sekta ya Posta Afrika. Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), akihutubia Mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la PAPU, makao makuu ya umoja huo jijini Arusha, leo Juni 11,2024. Msimamo huo wa Serikali umetolewa leo Juni 11, 2024 na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), wakati akihutubia Mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la PAPU, unaofanyika makao makuu ya umoja huo jijini Arusha. "Kwa heshima kubwa, napenda kuthibitisha msimamo usioyumba wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kusaidia mipango mbalimbali ya PAPU," amesema Mhandisi Mahundi aliyekuwa mgeni rasmi wa mkutano huo. Mhandisi Mahundi ameutaka mkutano huo wa PAPU, kutafakari njia zitakazowe...

Nauli Dar-Dodoma treni ya mwendokasi Sh 31,000

Picha
  -Kuumiza kichwa wenye mabasi Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imeutangazia umma wa Watanzania nauli  kwa safari ya treni za Mwendokasi, maarufu SGR, kuwa ni Sh  69.51 kwa kilomita,huku watoto  kuanzia kuanzia miaka 4 hadi 12 wakitakiwa kulipia Sh34.76 kwa kilomita. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwaaga viongozi wa dini 104 waliokuwa wakielekea Dodoma kwa Treni ya Mwendokasi (SGR), Jumatatu, Aprili 22, 2024. Picha ya Mtandao. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, nauli kwa safari ya  Dar es Salaam hadi Dodoma iliyo na umbali wa kilometa 444.0 itakuwa Sh31,000, huku safari ya Dar hadi Moro ya umbali wa kilometa 192.0 ikiwa Sh13,000 kwa watu wazima . Nauli za watoto kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma itakuwa Sh15,500 na kwa safari za Dar kwenda Moro ni Sh 6,500 huku  ikielezwa watoto mwenye umri chini ya miaka minne (4) hawatalipa nauli . Nauli hizo za Treni ya Mwendokasi (SGR), zinaelezwa kuwa zitaongeza tija k...

RC Nawanda 'aliwa kichwa' mchana kweupe

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk. Yahya Nawanda, 'ameliwa kichwa' mchana kweupe. Ndivyo unavyoweza kueleza baada ya uteuzi wake kutenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan leo Juni 11, 2024, huku Kenan Kihongosi aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba, akiteuliwa kuwa mkuu mpya wa mkoa huo. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan Kutenguliwa kwa uteuzi wa Nawanda, kumeandamana na maelezo, pia tuhuma mbalimbali zilizozagaa mitandaoni zikimtaja kwa jina kiongozi huyo kudaiwa kuhusika nazo, maeneo mbalimbali alipohudumu kama kiongozi. Dk. Yahya Nawanda Taarifa ya Ikulu, iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Sharifa Nyanga, imeleeza kuwa mbali na Rais Samia kutengua uteuzi wa Dk. Nawanda na kuteua mbadala wake, pia amefanya uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya  Momba ambaye sasa ni Elias Mwandobo akichukua nafasi ya Kihongosi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Kabla ya uteuzi huo, Mwandobo alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais, Ikulu. Zaidi soma taarifa ya Iku...

Naibu Waziri Mahundi kufungua Baraza la 42 PAPU kesho

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha  Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika (PAPU), Juni 11, 2024 Makao Makuu ya Ofisi za Umoja huo jijini Arusha. Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb). Mkutano huo utakaofanyika kwa siku 2 kuanzia  Juni 11 hadi 12,unatarajiwa kujadili maazimio na taarifa za vikao vya Kamati za Wataalam wa Masuala ya Posta vilivyoanza jijini humo Juni 03, 2024, ambavyo vilijadili masuala mbalimbali yanayohusu fedha na utawala, mikakati, sera na kanuni pamoja na uendeshaji na teknolojia. Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 45 wanachama wa PAPU pamoja na wadau mbalimbali wa Sekta ya Posta kutoka barani Afrika na wajumbe wa Sekretarieti ya Umoja wa Posta Duniani. Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika ni jukwaa muhimu kwa maende...

Wafanyabiashara wa ng'ombe wamuunga mkono Rais Samia

Picha
-Kufanya maonyesho Juni 14 Chalinze Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  CHAMA cha Wafanyabiashra wa Ng'ombe Tanzania (TCCS), kimesema kinaendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha sekta ufugaji nchini inazidi kuboreshwa kufikia ufugaji wa kisasa. Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji wa Kibiashara wa Ng'ombe(TCCS), Naweed Mulla (aliyevaa kofia),wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya mifugo na mnada, unaotarajiwa kufanyika Juni 14 -15, 2024 maeneo ya Ubena Estate Chalinze. Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji wa Kibiashara wa Ng'ombe nchini ( TCCS ), Naweed Mulla ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, kuhusu maonesho ya mifugo na mnada unaotarajiwa kufanyika Juni 14 -15, 2024 maeneo ya Ubena Estate Chalinze. "Lengo la kuanzisha programu hizo ni kusaidia wakulima na wafugaji kujikwamua kiuchumi wao wenyewe na kuongeza  Pato la Taifa kupitia ufugaji," amesema Mulla. Amebainisha kuwa takribani w...

Wafungisha ndoa wapewa siku 4 kujisajili e-RITA

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com KABIDHI Wasii Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Frank Kanyusi amewataka wafungishaji ndoa wote nchini kuhakikisha wamejisajili  kwenye mfumo wa kidijitali wa e-RITA ifikapo Juni 10, 2024. Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), Bw Frank Kanyusi  akisisitiza jambo kwa Waandishi wa habari  kuhusu umuhimu kwa wafungishaji ndoa wote nchini kujisajili kwenye mfumo wa kidijitali wa e-RITA. Agizo hilo hilo limetolewa na Kabidhi Wasii Mkuu Juni 6,2024, Dar es Salaam, ikiwa ni siku nne, kabla ya siku ya mwisho kujisajili, sawa na saa 96 za utekelezaji kwa walengwa. ā€œMfumo huu wa kidijitali utawazeshesha wahusika kutambulika katika kanzidata ya Msajili Mkuu wa Ndoa na Talaka, pia kupata leseni mpya za kidijitali za kufungisha ndoa,ā€ amesema Kanyusi na kuongeza; "Mfumo huo utaongeza ufanisi na kuongeza udhibiti wa usajili wa ndoa." Kanyusi amewataja wa...

Hamad Rashid kuachia kiti ADC, Doyo akiwania

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Katibu Mkuu wa Chama Cha Alliance for Democrac Change (ADC) Taifa, Doyo Hassan Doyo ametangaza nia ya kugombea nafasi ya Uenyekiti Taifa  wa chama hicho, baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Alliance for Democrac Change (ADC) Taifa, Doyo Hassan Doyo (Katikati) akitangaza nia ya kugombea nafasi ya Uenyekiti Taifa  wa chama hicho mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam, Juni 6, 2024. mwenyekiti wa sasa Hamad Rashid Mohamed kumaliza muda wake kikatiba. Akitangaza nia yake leo Juni 6, 2024 jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari, amesema ameona kuwa anaamimi ana uwezo wa kukitumikia chama hicho katika kutekeleza matakwa ya Katiba. "Kutokana na uzoefu wa miaka 10 nilioupata kutoka kwa Mwenyekiti aliiyemaliza muda wake naahidi kuyaendeleza mazuri yote hususani kuilinda Katiba ya chama. "Mwenyekiti Hamad ametufunza jambo katika chama kwani ameonyesha kufuata matakwa ya Katiba kwa kuachia ngazi baada ya kumaliza muda wake na kuwapa...

Majengo, eneo Urafiki yauzwa kwa NHC

Picha
-NHC yalipa mabilioni: Ni kupitia mnada wa wazi,   -Thamani ya NHC kuongezeka: Sasa kuboresha mandhari Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limenunua rasmi eneo la Urafiki na majengo yaliyokuwa chini ya Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD).  Sehemu ya majengo ya kilichokuwa la Kiwanda cha Urafiki, ambayo sasa yanamilikiwa na NHC. Hatua hiyo, itaongeza ukubwa wa mtaji na thamani ya shirika hilo la nyumba, linalotajwa kuongoza kwa ukubwa wa mtaji na uwekezaji barani Afrika, huku NHC likitajwa pia kuidhinisha na kusaini mikataba ya miradi 21 ya ubia yenye thamani ya Sh.bilioni 271  kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya ameyasema hayo leo wakati wa ziara ya kukagua maeneo mbalimbali, ambayo sasa yatakuwa chini ya miliki ya NHC na kufafanua kuwa eneo hilo linajumuisha nyumba, maghala, viwanja vya wazi, viwanda na mali nyin...

HESLB: 'Elimu ya Juu sasa njooni mkope'

Picha
 Sh bilioni 787 zasubiri wanafunzi 250,000 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com   Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB), imetangaza kufunguliwa dirisha la kuomba mkopo kwa wanafunzi katika mwaka wa masomo 2024/2025, huku waombaji wakitakiwa kusoma mwongozo uliopo kabla ya kuomba mkopo. Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6, 2024 Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk. Bill Kiwia, (pichani juu), amesema baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda kuzindua miongozo Mei 27, 2024, waliiweka miongozo hiyo kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo ambayo ni; Www.heslb.go tz . "Kwa mwaka wa masomo 2024/2025 dirisha la kuomba mkopo kwa njia ya mtandao lipo wazi kwa siku 90, kuanzia Juni 1 hadi Agosti 31, 2024," amesema Dk Kiwia. Hata hivyo, Dk. Kiwia amesema muda wa siku tisini unatosha kwa waombaji na wanatakiwa kuandaa nyaraka muhimu, na itachukua dakika 40 kukamilisha maombi yake kwa njia ya Mtandao. "Tunasisitiza waomba...

Taka za plastiki zawapeleka wanafunzi Ustawi 'Hult Prize' Kenya

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wanafunzi watatu kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii ni miongoni mwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali duniani wanaokutana jijini Nairobi nchini Kenya na kuchuana kuwania Tuzo ya 'Hult' kupitia mawazo yao ya kibiashara na ubunifu. Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii,  Dk. Joyce Nyoni, (wa tatu kushoto), akisalimiana na mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho watakaoshiriki kuwania tuzo ya  Hult Prize jijini Nairobi, linaloendeshwa kwa ushirikiano kati ya  Umoja wa Mataifa(UN), na timu za wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali duniani. Wengine pichani ni wanafunzi kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, watakaoshiriki kuwania tuzo hiyo mwaka huu 2024.  Wanafunzi hao kutoka Tanzania ni pamoja na Hellena Sailas,  Maria Daudi, na Method Dallu ambao wamechaguliwa kuwania tuzo hiyo kupitia wazo lao la kibishara na ubunifu linalohusu utengenezaji na uzalishaji wa matofali kwa kutumia taka za plastiki. Tuzo ya Hult Prize ni shindano kubwa zaidi la ujasiriama...

Msimamo wa Tanzania PAPU huu hapa

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha Wakati vikao vya Kamati za Ufundi vya Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika (PAPU), vikiendelea kwa siku ya tatu  jijini Arusha, Tanzania imetoa msimamo wake baada ya kuwasilisha hoja zake ikiwemo inayopendekeza kuwa na mwakilishi kiongozi katika nafasi ya juu ya uongozi wa umoja huo. Baadhi ya wawakilishi wa Tanzania kwenye mkutano wa Kamati za Ufundi vya Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika (PAPU), vinavyoendelea kwa siku ya tatu  jijini Arusha. Wawakilishi wa Tanzania wametoa msimamo huo wakizingatia kwamba kwa mujibu wa mkataba wa PAPU, nchi mwenyeji ambayo kwa sasa ni Tanzania inalazimika kuchangia asilimia 50 ya bajeti ya uendeshaji ya umoja huo kila mwanzo wa mwaka wa fedha, iwapo nchi wanachama hazijachangia kwa wakati, fedha ambazo baadaye hurejeshwa. "Katika hoja zetu, tumesisitiza Tanzania kupatiwa nafasi hiyo ili kuhakikisha usimamizi imara wa fedha zinazotolewa, ambazo Tanzania imekuwa ikilipa kama nchi mwenyeji, pia kusima...

EWURA yaweka hadharani bei mpya ya petroli

Picha
-Dar sasa bei  Sh3,261, Dodoma Sh3,320, Bukoba Sh3,476 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo  ya mafuta ya petroli na bidhaa zake nchini kwa mwezi Juni, huku ikiainisha bei ya chini kuwa ni Sh 3,261 kwa lita moja ya petroli Dar es Salaam na bei ya juu ni Sh 3,476 mkoani Kagera. Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dk. James Mwainyukule Kwa mujibu wa EWURA, bei ya lita moja ya diseli kwa Dar es Salaam ni Sh3,112 huku wilayani Tanganyika ikiwa Sh 3,288 kwa lita moja na mafuta ya taa yakiwa bei sawa na petroli kwa maeneo hayo. Taarifa ya EWURA iliyotolewa Juni 5, 2024 kupitia mkurugenzi wake mkuu, Dk. James Mwainyukule, imeeleza kuwa bei kikomo za rejareja kwa lita moja ya petroli kwa Bandari ya Dar es Salaam ni Sh 3,261 huku kwa Bandari ya Tanga ikiwa Sh3,263 kwa lita. Katika jiji la Dodoma bei ya lita moja ya petroli ikiwa Sh3,320, dizeli Sh3,171 na mafuta ya taa yakiuzwa kwa Sh3,319 kwa lita, huku jijini Aru...

'Wataalam Posta tumieni maendeleo teknolojia kufungua fursa za kiuchumi'

Picha
 MWANDISHI WETU, WHMTH, Arusha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Dk. Mzee Suleiman Mndewa, amewataka wataalamu wa masuala ya Posta Afrika, kutumia vyema maendeleo ya teknolojia katika kuwezesha sekta hiyo kufungua fursa za kiuchumi na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi katika nchi hizo. Washiriki wa vikao vya Kamati za Wataalamu wa Masuala ya Posta kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU0, uliofanyika jijini  Arusha, Juni 3, 2024. vikao hivyo ni vya utangulizi kabla ya Mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la PAPU litakalofanyika Juni 11 hadi 12 jijini humo.  Dk. Mndewa amesema hayo Juni 03, 2024 mkoani Arusha wakati akifungua Vikao vya Kamati za wataalamu wa masuala ya posta kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU), ikiwa ni vikao vya utangulizi kabla ya Mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la PAPU litakalofanyika Juni 11 hadi 12 jijini humo. Amesema kuwa ili nchi za Afrika ziweze kufanikiwa zaidi katika masuala ya ...