Exuperius Kachenje,daimatznews@gmail.com
Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, ametaja shabaha saba za uchumi kwa jumla katika bajeti yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025.
![]() |
Begi la Bajeti ya Serikali mwaka 2024/2025 |
Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2024/25, bungeni mjini Dodoma leo Juni 13, 2024, Dk. Mwigulu amesema shabaha hizo zimetokana na nyaraka na miongozo iliyozingayowa katika uandaaji bajeti hiyo.
"Shabaha za uchumi jumla ni saba kama ifuatavyo; Kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa kufikia asilimia 5.4 mwaka 2024 kutoka ukuaji wa asilimia 5.1 mwaka 2023; Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0 - 5.0 katika muda wa kati," amesema Dk Mwigulu.
Nyingine ni mapato ya ndani kufikia asilimia 15.8 ya Pato la Taifa mwaka 2024/25 ikilinganishwa na matarajio ya asilimia 15.4 mwaka 2023/24; Mapato ya kodi kufikia asilimia 12.9 ya Pato la Taifa mwaka 2024/25 kutoka matarajio ya asilimia 12.6 mwaka 2023/24 na kuwa na nakisi ya bajeti ikijumuisha misaada isiyozidi asilimia 3.0 ya Pato la Taifa.
![]() |
Wabunge wakifuatilia hotuba ya bajeti ikisomwa bungeni mjini Dodoma, Juni 13,2024. |
Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Fedha, shabaha nyingine ni kuwa na akiba ya fedha za kigeni kwa kiwango cha kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje kwa kipindi kisichopungua miezi minne.
Bajeti hiyo inawasilishwa na Waziri wa Fedha kwa mujibu wa Ibara ya 137 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na Kifungu cha 23 (3) cha Sheria ya Bajeti, Sura 439 na Kifungu cha 124 (4) cha Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Februari 2023.
Katika hotuba yake Dk. Mwigulu aliomba Bunge lipokee, lijadili na kukubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2024/25 yanayofikia Sh
0 Maoni