Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Mambo mapya saba, Sabasaba 2024

 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com

Ni msimu wa Maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba, safari hii yakiwa ni ya 48 tangu kuanzishwa kwake, yakiendeshwa na kuratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara  Tanzania (Tan Trade), ambapo kwa mwaka huu ykuna mambo saba tofauti, mapya yanayobeba maonyesho hayo ikiwamo matumizi ya robot (akili bandia (IA).

Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis

Katika mahojiano, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Latifa Khamis ameeleza kuwa maonyesho ya mwaka huu ni tofauti na miaka mingine, kutokana na ukweli kwamba yanabebwa na mambo saba tofauti.

“Maonyesho ya mwaka huu yana sura ya kipekee, tuna bidhaa za kitanzania halisia, tuna nchi za kigeni zaidi ya 25 zinashiriki, tuna mabanda manne ya kimataifa, tuna nchi zaii ya sita zitahimisha siku za mataifa yao kwa mwaka 2024 kipindi cha maonyesho, tiketi za Sabasaba mwaka huu zipo kwa mtandao;

Pia tutawadhamini wafanyabiashara wa Kariakoo ili waweze kuuza bidhaa za jumla kutoka kwa washiriki wa maonyesho kutoka nje ya nchi, lakini zaidi tutakuwa na roboti atakayetumika kukaribisha mgeni rasmi. Hii itaonyesha namna teknolojia ilivyokua na inavyoweza kutumika kuleta maendeleo,” amesema Latifa.

Kuhusu kuwadhamini wafanyabishara wa Dar es Salaam, Mkurugenzi huyo wa TanTrade amesema kuwa, watafanya hivyo kwa lengo la kundi hilo kuachiwa bidhaa na washiriki wa nje, ambao mara nyingi huondoka na bidhaa zao wakishamaliza maonyesho.

Kwa mujibu wa Latifa nchi zitakazoathimisha siku za mataifa yao kwenye maonyesho ya Sabasaba ni pamoja na China, Uturuki, Singapore, Pakistan, Ghana, Uturuki na Korea.

Amesema kwamba maonyesho hayo yanachangia pato la taifa kwa kuwa washiriki wa nje wanalipia ushiriki wao, lakini pia yanakuza diplomasia kati ya Tanzania nan chi washiriki.

Latifa ameeleza kuwa kwa mwaka huu 2024, nchi za China na Misri zinaongoza kwa kuleta washiriki wengi, China ikiwa na washiriki zaii ya 300 na Misri ikiwa na washiriki 35,

Kuhusu ushiriki wa Tanzania mkurugenzi huyo amesema, katika maonyesho hayo yaliyoanza leo yakitarajiwa kukamilika Julai 13, wizara na taasisi 2,979 zinashiriki huku kampuni zikiwa 223.

Latifa amesema katiuka maonyesho hayo Zanzibar ina washiriki zaidi ya 15, akieleza kuwa lengo la maonyesho hayo ni kuongeza ustawi wa jamii akibainisha wanafunzi na mama lishe nio walioongoza kwa kupata ajira.  

Amesema kupitia maonyesho hayo TanTrade inaendesha mpango maalum wa Urithi Wetu inayojumuisha watoto hasa wa vijijini ambao hupewa nafasi ya kutembelea maonyesho hayo kwa siku tatu nan je ya maonyesho hayo kujifunza masuala ,mbalimbali kwa lengo la kuwarithisha mema ya taifa.

“Kwa mwaka huu tuna Watoto kutoka Monduli mkoani Arusha, Kondoa Mkoa wa Dodoma, Kilosa mkoani Mrorogoro, pia kutoka Unguja na Pemba,” amesema Mkurugenzi huyo wa TanTrade.

 

Chapisha Maoni

0 Maoni