Hot Posts

6/recent/ticker-posts

EWURA yaweka hadharani bei mpya ya petroli

-Dar sasa bei  Sh3,261, Dodoma Sh3,320, Bukoba Sh3,476


Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com

Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo  ya mafuta ya petroli na bidhaa zake nchini kwa mwezi Juni, huku ikiainisha bei ya chini kuwa ni Sh 3,261 kwa lita moja ya petroli Dar es Salaam na bei ya juu ni Sh 3,476 mkoani Kagera.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dk. James Mwainyukule

Kwa mujibu wa EWURA, bei ya lita moja ya diseli kwa Dar es Salaam ni Sh3,112 huku wilayani Tanganyika ikiwa Sh 3,288 kwa lita moja na mafuta ya taa yakiwa bei sawa na petroli kwa maeneo hayo.

Taarifa ya EWURA iliyotolewa Juni 5, 2024 kupitia mkurugenzi wake mkuu, Dk. James Mwainyukule, imeeleza kuwa bei kikomo za rejareja kwa lita moja ya petroli kwa Bandari ya Dar es Salaam ni Sh 3,261 huku kwa Bandari ya Tanga ikiwa Sh3,263 kwa lita.

Katika jiji la Dodoma bei ya lita moja ya petroli ikiwa Sh3,320, dizeli Sh3,171 na mafuta ya taa yakiuzwa kwa Sh3,319 kwa lita, huku jijini Arusha, bei ya lita moja ya petroli ni Sh3,320,  dizeli Sh 3,178 na mafuta ya taa ni Sh3,345.

Katika jiji la Mwanza, bei ya lita moja ya petroli ni Sh 3,411 petroli, Sh3,262 dizeli na mafuta ya taa Sh 3,411.

Zaidi soma jedwali la bei mpya ya mafuta iliyotolewa na EWURA Juni 5, 2024





Chapisha Maoni

0 Maoni