Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Dar mpaka Moro moto SGR abiria kuanza safari kesho

 

Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com

Dar mpaka Moro, hayawi, hayawi, sasa yamekuwa. Tanzania inaandika historia mpya katika nyanja ya usafiri na usafirishaji Saa12 kamili ya Juni 14, 2024, ambapo Treni ya Mwendokasi (SGR) inayotumia umeme, ikianza safari zake kwa kubeba abiria kibiashara.

Treni ya Umeme ya SGR

Treni hiyo itaanza safari zake, kabla ya muda uliopangwa wa Julai mwaka huu kufika, ambapo itaanza kwa safari za Dar es Salaam kwenda Morogoro.

Nauli kwa abiria mmoja kwa kila safari ni Sh13,000 mtu mzima huku watoto wenye umri zaidi ya miaka minne wakitakiwa kulipa nusu ya nauli ya mtu mzima.

Daima Tanzania blog, ilikuwepo kwenye kituo kikuu cha treni hiyo maeneo ya Steshen", ambapo ilishuhudia maandalizi ya mwisho yakiendelea, huku wananchi waliojaa bashasha, wakiingia na kuulizia upatikanaji wa tiketi.

Hata hivyo, walielezwa kuwa wanaweza kupata titeki hizo kupitia mtandao wa TRC au wawahi kufika kituoni hapo kabla ya muda wa safari.

Ratiba iliyotolewa na Shirika la Reli Tanzania (TRC), inaonyesha kwamba treni ya kwanza ya Dar mpaka Moro, itaanza safari saa 12 kamili asubuni ambapo itasafiri kwa takriban dakika 109 kukamilisha safari yake.

Dakika hizo 109 ni sawa na saa 1 na dakika 49, ikimaanisha kwamba kwa mara ya kwanza abiria wa SGR, watafikishwa mjini Morogoro saa 1 na dakika 49.

Treni ya kwanza ya SGR kutoka Moro itaanza safari yake saa2:50 asubuhi na kuwasili Dar saa 4:39, huku treni ya pili kwenda Moro ikitoka Dar saa10 kamili jioni na itafika Moro saa 11:49.

Safari ya nne na ya mwisho kila siku katika ratiba ya safari hizo, itakuwa ikianzaia Moro kwenda dar, ambapo itaondoka saa 1:30 usiku na kuwasili Dar saa 3:19 usiku.

Kwa mujibu wa TRC, safari za treni hiyo zitafanyika kila siku, kuanzia Jumatatu hadi Jumapili.

Chapisha Maoni

0 Maoni