Sh bilioni 787 zasubiri wanafunzi 250,000
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB), imetangaza kufunguliwa dirisha la kuomba mkopo kwa wanafunzi katika mwaka wa masomo 2024/2025, huku waombaji wakitakiwa kusoma mwongozo uliopo kabla ya kuomba mkopo.
![]() |
"Kwa mwaka wa masomo 2024/2025 dirisha la kuomba mkopo kwa njia ya mtandao lipo wazi kwa siku 90, kuanzia Juni 1 hadi Agosti 31, 2024," amesema Dk Kiwia.
Hata hivyo, Dk. Kiwia amesema muda wa siku tisini unatosha kwa waombaji na wanatakiwa kuandaa nyaraka muhimu, na itachukua dakika 40 kukamilisha maombi yake kwa njia ya Mtandao.
"Tunasisitiza waombaji kuzingatia muda uliotolewa kwa kuwa hatutarajii kuongezwa baada ya Agosti 31, 2024," amesema.
Amebainisha kuwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imetenga Sh. Bilioni 787 kwa ajili ya mikopo na ruzuku kwa jumla ya wanafunzi 250,000 ambapo idadi hiyo imeongezeka kutoka wanafunzi 224,056 mwaka 2023/2024 ambapo ni ongezeko la jumla wanafunzi 25,944.
0 Maoni