Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2025

Mtoto wa Mbowe hatarini kutupwa 'lupango'

Picha
-Yupo mikononi mwa Jaji -Ni kukaidi amri ya mahakama -Mishahara ya wanahabari yamponza Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe yupo hatarini kutupwa gerezani, baada ya maombi ya wanahabari 10 wanaomdai malimbikizo ya mishahara kufika mbele ya Jaji, Dk Modesta Opiyo, katika Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi. Dudley Mbowe Waandishi hao wamewasilisha ombi la kutaka Dudley ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti Mstaafu wa Chadema,Freeman Mbowe akamatwe na kutupwa gerezani baada ya Mkurugenzi huyo wa Gazeti Tanzania Daima kushindwa kuwalipa fedha hizo.  Wadai ambao ni Maregesi Paul na wenzake 9 waliwasilisha maombi mahakamani hapo ya kumkamata Dudley na kumtupa gerezani kama mfungwa wa kiraia baada ya kushinda tuzo ambayo Dudley hakuitekeleza.  Januari 14 mwaka huu mahakama hiyo ilimuonya Dudley mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio akielezwa hajawahi kufika mahakama licha ya kuahidi kufanya hivyo, huku akiamriwa kufika m...

Miaka minne ya Rais Samia madarakani ilivyoifungua NHC

Picha
- Mapato yaongezeka hadi Sh. bilioni 9.4   - Thamani yapaa kufikia Sh. trilioni 5.47 - Miradi, ndoto makazi bora vyatekelezwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Samia Suluhu Hassan akiapa kuiongoza Tanzania, Machi 19,2021. Kiongozi huyo atatimiza miaka minne madarakani Machi 19, mwaka huu .     Unapozungumzia mageuzi katika sekta ya nyumba Tanzania, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), litakuwa la kwanza kulitaja. Hii inatokana na ukweli usiopingika kwamba NHC ndiyo chachu ya mageuzi hayo makubwa nchini. Hakuna kificho kwamba jukumu pekee na kubwa la NHC tangu kuundwa kwake muda mfupi baada ya Uhuru wa Tanzania Bara mwaka 1961 ni kuwawezesha Watanzania kupata makazi bora. Ikumbukwe kuwa Shirika la Nyumba la Taifa, limeanzishwa mwaka 1962 chini ya Sheria ya Bunge Na. 45 na tangu wakati huo, limekuwa likitimiza jukumu lake hilo la kipekee kwa Watanzania kuwapatia makazi bora.  Hayo ndio maono ya NHC, iliyoyaakisi kutoka kwa muasisi wake, Rais wa Kwanza wa Tan...

'Fuatilieni vitambulisho vyenu vya taifa'

Picha
  Hussein Ndubikile,daimatznews@gmail.com  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo amewahimiza wananchi  kufuatilia vitambulisho vyao vya Taifa mara baada ya kujisajili ili kuepuka changamoto zinazojitokeza wanapohitaji huduma muhimu za kijamii. Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), James Kaji ,akizungumza mbele ya wanahabari. Sillo amezungumza hayo baada ya kutembelea Ofisi za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na kuzungumza na watumishi wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam,Januari 13,2025. Naibu Waziri Sillo, ameeleza kuwa vitambulisho zaidi ya milioni 20 tayari vimetengenezwa na kupelekwa Ofisi husika lakini bado kuna changamoto ya baadhi ya watu kushindwa kufuatilia vitambulisho hivyo kwa wakati Kadhalika Naibu Waziri alimpongeza Mkurugenzi wa NIDA na watumishi hao kwa kazi kubwa wanayoifanya  kuhakikisha huduma ya vitambulisho inawafikia wananchi pamoja na ongezeko la uzalishaji wa vitambulisho hivyo. Kwa upande wake...

Jamii ishirikiane kukomesha haya-ACT

Picha
 Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Mwenyekiti  wa Ngome ya Vijana ya Chama cha ACT Wazalendo, Abdul Nondo amesema  ni muhimu jamii kushirikiana bila kujali itikadi zao    ili kukomesha vitendo vya utekaji vilivyoshamiri nchini. Abdul Nondo Nondo amesema ili kukomesha vitendo vya utekaji ni vyema pia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, likafanya mabadiliko ya sheria kwa Askari wa Jeshi la Polisi, kuvaa sare anapokwenda kumkamata mtuhumiwa ili kuondoa taharuki. "Tofauti na hilo ni vema sheria nayo ikasema kwamba sheria ikasema askari anatakiwa ajitambulishe na kueleza kosa la mtuhumiwa kabla ya kumkamata na aeleze anampeleka kituo gani cha Polisi ili kuwapa urahisi ndugu, jamaa kuweza kumfuatilia. Ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam Januari 13,2025 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu mazingira ya kutekwa kwake na hofu aliyonayo baada ya kuvunja masharti aliyopewa  na waliomteka wakati wakimwachia, akiamini kwamba wanaweza kumteka tena na peng...

Mahakama yamwonya mtoto wa Mbowe kwa kutofika kortini

Picha
-Yamtaka kulipa madai ya wanahabari Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAHAKAMA Kuu Divisheni ya Kazi imemuonya Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe kwa kutofika mahakamani tangu shauri la madai ya malimbikizo ya misharaha ya waandishi wa habari 10 lilipofunguliwa mwanzoni mwa mwaka jana na kumuamuru kulipa fedha hizo. Dudley Mbowe, Mkurugenzi wa Tanzania Daima Dudley ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amepewa amri hiyo leo Januari 14,2025 mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio wakati shauri hilo la madai lilipokuwa likitajwa,ambapo ametakiwa kulipa kabla ya Januari 31,2025. Msajili Mrio amesema shauri hilo limwtajwa leo kwa ajili ya kuangalia maombi ya waandishi wa habari ya kumkamata Dudley na kumtupa gerezani kama mfungwa wa kiraia kwa kushindwa kulipa malimbikizo ya mishahara yao baada ya kushinda tuzo mahakamani. Hata hivyo, Mrio amesema maombi hayo hayajawasilishwa ambapo amemuru yawasilishwe mahakamani ndani ya siku saba kwa aj...

'NHC yaokoa bilioni 24'

Picha
  - DC aipongeza NHC  - Ni baada ya ku tembelaea Samia Housing Scheme  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, amefanya ziara katika mradi wa kihistoria wa Samia Housing Scheme, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Kawe, jijini Dar es Salaam na kupongeza jitihada za shirika hilo kuendeleza makazi bora nchini.  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, Wa pili  kushoto, akiwa katika ziara kwenye mradi wa kihistoria wa Samia Housing Scheme, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Kawe, jijini Dar es Salaam, Januari 8, 2025. Wengine pichani ni watendaji wa NHC na kutoka ofisi ya Mkuu huyo wa Wilaya . Akizungumza katika ziara hiyo,  Mtambule amesema kuwa iwapo mradi huo ungejengwa na mkandarasi wa nje, gharama zingefikia shilingi bilioni 72, hivyo ufanisi wa NHC ni jambo la kujivunia. “Hivyo tunaweza kueleza kuwa, hapa NHC imeokoa takriban Shilingi bilioni 24, ambazo sasa zinatumika kwa sh...

'NHC yaokoa bilioni 24'

Picha
- DC aipongeza NHC  - Ni baada ya ku tembelaea Samia Housing Scheme  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, amefanya ziara katika mradi wa kihistoria wa Samia Housing Scheme, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Kawe, jijini Dar es Salaam na kupongeza jitihada za shirika hilo kuendeleza makazi bora nchini.  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, Wa pili  kushoto, akiwa katika ziara kwenye mradi wa kihistoria wa Samia Housing Scheme, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Kawe, jijini Dar es Salaam, Januari 8, 2025. Wengine pichani ni watendaji wa NHC na kutoka ofisi ya Mkuu huyo wa Wilaya . Akizungumza katika ziara hiyo,  Mtambule amesema kuwa iwapo mradi huo ungejengwa na mkandarasi wa nje, gharama zingefikia shilingi bilioni 72, hivyo ufanisi wa NHC ni jambo la kujivunia. “Hivyo tunaweza kueleza kuwa, hapa NHC imeokoa takriban Shilingi bilioni 24, ambazo sasa zinatumika kwa shughuli ...

Baraza Kivuli ACT, lajipanga kusimamia uwajibikaji wa Serikali

Picha
Hussein  Ndubikile, daimatznews@gmail.com Waziri Mkuu Kivuli wa Chama cha ACT Wazalendo, Isihaki Rashidi Mchinjita, amesema kuwa Baraza la Mawaziri Kivuli la chama hicho litautumia mwaka 2025 kwa kusimamia haki za wananchi, uwajibikaji wa Serikali na kupigania mageuzi ya kweli ya kidemokrasia. Waziri Mkuu Kivuli wa Chama cha ACT Wazalendo,   Isihaki Rashidi Mchinjita akizungumza na wanahabari Januari 8,2025 Makao Makuu ya ACT, Magomeni Dar es Salaam, Mchinjita amesema mwaka 2024 ulikuwa wa changamoto nyingi ikiwamo migogoro ya ardhi,  hali ya kiuchumi isiyorihisha, kuongezeka kwa matukio ya utekaji na mauaji, maafa ya mvua za Elnino na wananchi kukosa huduma bora akieleza kwamba mwaka 2025 haupaswi kuendelea na taswira ya mwaka jana.. Katika kusisitiza msimamo huo, amesema kuwa Watanzania wanapaswa kushirikiana na ACT Wazalendo kufanya maamuzi yatakayoleta mabadiliko katika kuimarisha maisha yao na kujenga taifa la wote. Kauli hiyo ameitoa Januari 8, 2025 alipozungum...

DC Kinondoni ‘amteta’ Rais Samia NHC

Picha
         Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Ahmad Abdallah - Aipongeza NHC kwa ubunifu Morocco Square - Atamani ‘Morocco Square’ nyingine Mabwepande   Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule, amefanya ziara katika Mradi wa Morocco Square, unaotekelezwa na NHC 'akimteta’ Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumpongeza kutokana na kuongoza juhudi za kukwamua miradi mikubwa ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), iliyokuwa imekwama.   Msimamizi wa Mradi wa Morocco Square kutoka NHC, Stanley Msofe akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni. Saad Mtambulike(aliyevaa suti), sehemu ya jengo hilo, wakati kiongozi huyo alipotembelea na kukagua jengo hilo. Wengine pichani ni Meneja Habari na Uhusiano waNHC, Muungano Saguya (wa pilikulia) na mtumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya  Kinondoni. Mtambule pia amelipongeza shirika hilo kwa ubunifu ujenzi wa Morocco Square akisema anatamani ubunifu aliouona kwenye ujenzi wa jengo hilo upelekwe ...

Rais Samia azindua hoteli ya bil 109 Kisiwa cha Bawe

Picha
-Dk. Mwinyi akunjua makucha wawekezaji ‘uchwara’  -Rais Samia aunga mkono wanyang'anywe visiwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Zanzibar; Rais Samia Suluhu Hassan amezindua hoteli kubwa ya kitalii Bawe Island the Cocoon Collection iliyopo katika Kisiwa cha Bawe Januari 7,2025, huku Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi akitoa siku 90 kwa wawekezaji walioshindwa kuendeleza visiwa walivyovikodi kuvirejesha serikalini. Rais Samia Suluhu Hassan (Wa pili kulia), akisisitiza jambo, wakati alipotembelea kujionea vyumba vya kulala wageni katika Hoteli ya Bawe, kisiwani Bawe aliyoizindua Januari 7,2024 mjini Zanzibar.Wa nne kulia ni Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, aliyesimama mbele ni mwekezaji wa mradi huo. Katika tukio hilo la kihistoria, ambalo ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12 mwaka 1964, Rais Samia amezindua hoteli hiyo akiwa na mwenyeji wake Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwiny...