Mtoto wa Mbowe hatarini kutupwa 'lupango'

-Yupo mikononi mwa Jaji -Ni kukaidi amri ya mahakama -Mishahara ya wanahabari yamponza Na Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe yupo hatarini kutupwa gerezani, baada ya maombi ya wanahabari 10 wanaomdai malimbikizo ya mishahara kufika mbele ya Jaji, Dk Modesta Opiyo, katika Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi. Dudley Mbowe Waandishi hao wamewasilisha ombi la kutaka Dudley ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti Mstaafu wa Chadema,Freeman Mbowe akamatwe na kutupwa gerezani baada ya Mkurugenzi huyo wa Gazeti Tanzania Daima kushindwa kuwalipa fedha hizo. Wadai ambao ni Maregesi Paul na wenzake 9 waliwasilisha maombi mahakamani hapo ya kumkamata Dudley na kumtupa gerezani kama mfungwa wa kiraia baada ya kushinda tuzo ambayo Dudley hakuitekeleza. Januari 14 mwaka huu mahakama hiyo ilimuonya Dudley mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio akielezwa hajawahi kufika mahakama licha ya kuahidi kufanya hivyo, huku akiamriwa kufika m...