Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Rais Samia azindua hoteli ya bil 109 Kisiwa cha Bawe

-Dk. Mwinyi akunjua makucha wawekezaji ‘uchwara’
 -Rais Samia aunga mkono wanyang'anywe visiwa
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Zanzibar; Rais Samia Suluhu Hassan amezindua hoteli kubwa ya kitalii Bawe Island the Cocoon Collection iliyopo katika Kisiwa cha Bawe Januari 7,2025, huku Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi akitoa siku 90 kwa wawekezaji walioshindwa kuendeleza visiwa walivyovikodi kuvirejesha serikalini.
Rais Samia Suluhu Hassan (Wa pili kulia), akisisitiza jambo, wakati alipotembelea kujionea vyumba vya kulala wageni katika Hoteli ya Bawe, kisiwani Bawe aliyoizindua Januari 7,2024 mjini Zanzibar.Wa nne kulia ni Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, aliyesimama mbele ni mwekezaji wa mradi huo.

Katika tukio hilo la kihistoria, ambalo ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12 mwaka 1964, Rais Samia amezindua hoteli hiyo akiwa na mwenyeji wake Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Uzinduzi wa hoteli hiyo ni sehemu ya mikakati ya Dk.Mwinyi kuinua Uchumi wa Zanzibar kwa kuvutia wawekezaji, ambapo uwekezaji wa Bawe Hotel umefanyika chini ya mpango ukodishwaji ardhi ya visiwa vidogo chini ya Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) na tayari visiwa16 kati ya 50 vimewekezwa.

Akiungumza katika hafla hiyo kwenye kisiwa hicho kilichopo umbali wa kilometa kumi kutoka Mji Mkongwe, Rais Samia amesema Dk. Mwinyi aliona mbali kwa kufikiria na kutekeleza ukodishaji wa visiwa vidogo.

“Dk Mwinyi aliona mbali kukoisha visiwa, waswahili husema,uchumi tuliukalia, leo ajira zaidi ya 400 zimezalishwa. Ujenzi na uwekezaji katika visiwa vidogo utakuza jina la Zanzibar, kila jambo lina mambo yake,” amesema Dk Samia na kuongeza: 

“Uwekezaji huu hapa Bawe wa zaidi ya Dola za Marekani 42 milioni (Shilingi bilioni 109.2) ni ishara ya wawekezaji kuridhika na mazingira pia utawala.” 

Rais Samia amesema lengo na dhamira ya mapinduzi ni kuwaletea neema wananchi wa Zanzibar na kwamba hata Ilani ya Uchaguzi wa CCM imeeleza, yapo mambo mengi ya kufanya, ikiwamo Uchumi wa Zanibar kuwa endelevu.

“Mawapongeza ZIPA kusimamia uwekezaji, msiingizwe mtegoni, kazi iendelee, yajayo yanafurahisha. Serikali imedhamiria kuongeza uwekezaji bandarini katika Bandari ya Malindi, Maruhubi, Fumba, Mkoani, Manga Pwani na Mpigaduri,pia ujenzi wa Bandari Wete na kubwa zaidi Kizimkazi; 

Hapa Dk.Mwinyi umemaliza, ntakupa kila ushirikiano, Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume unaendelea kuboreshwa, Pemba sasa ndege zinarukahata usiku, ila tutafanya makubwa zaidi. 

Naipongeza ZIPA kwa usimamizi madhubuti, tuendelee kuelimisha wananchi uwekezaji katika visiwa kwani ni jambo jipya kwao.” 

Rais Samia amesema jeuri ya leo ya Zanzibar katika maeneleo inatokana na mchango wa Serikali ya Mapinduzi awamu zote,akihimiza wananchi kuendelea kuyaenzi mapinduzi.

Awali, akimkaribisha Rais Samia, Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi amesema:

“ …Leo niseme hadharani kwamba Rais Samia amekuwa msaada mkubwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika mambo yetu yote. Namshukuru na kumpongeza kwa dhati na kwa kweli tupo pamoja naye katika kuijenga nchi yetu kwa pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
Leo ni historia ya pekee, tumeonyesha faida ya maeneo ya visiwa, awali yalisemwa mengi.” 

Dk. Mwinyi amesema Serikali yake kupitia ZIPA imeshatoa visiwa 16 kwa wawekezaji ili viwekezwe na kwamba Bawe ndio mradi wa kwanza kuzinduliwa ikiwa na kiwango cha kimataifa, akiwashukuru wawekezaji kwa kutimiza waliloahidi ikiwamo kuwasaidia wavuvi waliokuwa wakitumia kisiwa hicho kwa kuwajengea jiko la kisasa na kununua samaki wote wanaowavua. 

Amewaonya wawekezaji waliokodishwa visiwa bila kuviendeleza kwa muda mrefu kuwa vitarejeshwa serikalini wsipofanya lolote ndani ya siku 90. 

“…Nataka leo nitoe tamko kwa wale wote ambao tumewakodisha visiwa, muda umekuwa mrefu, hawajaanza kujenga, Serikali inawapa miezi mitatu kuanzia sasa. Hapo tutakapoona hawaendelezi tutavirudisha serikalini,” amesema.
Rais Samia Suluhu Hassan katika hotuba yake ya ufunguzi wa hoteli hiyo ameunga mkono kauli ya Dk,Mwinyi kuhusu kuwanyang’anya wawekezaji wasiondeleza visiwa hivyo akisema; 
“Nami naungana na Rais wa Zanzibar kwamba wale wote waliopewa visiwa nahawajafanya kazi, basi miezi mitatu,baada yah apo Mheshimiwa Rais usirudi nyuma.”

Akizungumzia CCM, Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi amesema Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho ya mwaka 2020 iliwataka kuongeza vitanda kwenye hoteli za kitalii kutoka 10,000 hadi 15,000, lakini hadi 2024, mwaka mmoja kabla muda wa utekelezaji kuisha wameshaongeza kufikia 15,132. 

Dk. Mwinyi ametaja faida kubwa tatu za uwekeaji ikiwamo kukukua kwa soko la bidhaa za wazanzibari, kuongezeka watalii na ajira, akiwataka Wazanzibar kuwa na weledi na kusoma ili waweze kufanya kazi kwenye hoteli hizo za kitalii. 

Amedokeza kuwa nchi ya Italia kupitia balozi wake nchini imeeleza kutenga kiasi cha Euro 5000 kwa ajili ya kuwajengea uwezo Wazanzibar waweze kuajiriwa kwenye hoteli hizo, akiishukuru Italia kwa msaada huo.

Chapisha Maoni

0 Maoni