Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2025

Naibu Spika Zungu meza kwa meza kusaka kura

Picha
  Naibu Spika Mussa Azzan Zungu, akipita kwa wafanyabiashara, meza kwa meza Mtaa wa Mkwepu, jimboni Ilala, kusaka kura za Mgombea Urais wa CCM, Dk.Samia Suluhu Hassan, Mbunge, yeye Zungu, na madiwani wa CCM, muda huu, Oktoba 15,2025

Raila Odinga afariki dunia

Picha
 Nairobi,Kenya. Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, (Pichani chini),amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80. Chanzo kutoka ofisi ya Odinga, kimeliambia Shirika la Habari la Reuters Jumatano, bila kufafanua. Awali, Gazeti la India la Mathrubhumi liliripoti kuwa Odinga, ambaye alikuwa akipata matibabu mjini Kochi, Kusini mwa India, alipatwa na shambulio la moyo Jumatano na alihamishiwa hospitalini ambapo baadae alitangazwa amefariki.   Enzi za uhai wake akiwa kiongozi wa upinzani, Odinga aligombea urais wa Kenya mara tano bila mafanikio, mbili kati ya hizo zilisababisha machafuko makubwa, umwagaji damu na malalamiko miaka kumi mfululizo.   Hata hivyo ushiriki wake katika harakati za kidemokrasia kwa miaka mingi, ziliisaidia kuimarisha mageuzi mawili makubwa nchini Kenya, moja likiwa demokrasia ya vyama vingi mwaka wa 1991 na pili ni Katiba Mpya nchini humo mwaka wa 2010.   Odinga aliongoza maandamano baada ya uchaguzi wa 2007 uliozua mzozo mk...

TEC yajitenga waraka feki, yatoa taarifa kwa umma

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Baraza la Maaskofu Katolini Tanzania (TEC), limekanusha kuhusika na waraka uliokuwa ukizagaa mitandaoni Oktoba 13,2025 ukilihusisha Baraza hilo na waraka usio wake na kusema hiyo ni tabia mbaya kutumia TEC na kutaka ikomeshwe. Katibu Mkuu wa TEC, Padri Charles Kitima  Taarifa ya TEC iliyotiwa saini na Katibu wake Mkuu, Padri Charles Kitima imeeleza kuwa waraka huo wenye Kichwa cha Habari; TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC) KUHUSU AMANI KWA TAIFA KUELEKEA SIKU YA UCHAGUZI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UTAKAOFANYIKA TAREHE 29 OKTOBA 2025. "SAUTI YA WATU SAUTI YA MUNGU"   ni 'Fake'. Padri Kitima amesema wanawatangazia Waamini na Watanzania wote kwa ujumla kuwa waraka huo haukutolewa na   Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. “Baraza halihusiki na hayo maudhui yaliyomo kwenye andiko hilo,” amesema. TEC kupitia taarifa yake kwa umma yenye kumbukumbu namba TEC/GEN/1/2025 iliyobeba kichwa cha habari; YAH ...

Makamu wa Rais ashiriki Misa kumuombea Nyerere

Picha
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Philip Mpango ameungana na viongozi, Waumini pamoja na wananchi mbalimbali katika Ibada ya kumuombea Baba wa Taifa Hayati Mwalimu. Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Francisko wa Asizi, Mwanjelwa Mkoani Mbeya leo tarehe 14 Oktoba 2025. Ibada hiyo imeongozwa na Akofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbeya Mhashamu Gervas Nyaisonga. Viongozi wengine wa kitaifa walioshiriki adhimisho hilo ni pamoja na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson.

Uhamiaji yatimua wawili nchini

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Idara ya Uhamiaji nchini imewafukuza nchini raia wawili wa kigeni, Mmarekani mmoja na Mjerumani mmoja, ikieleza hatua hiyo imetoka na wawili hao kukiuka masharti ya viza zao za matembezi. Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Anna Makakala Taarifa iliyotolewa leo na Uhamiaji imewataja raia hao kuwa ni Dk. Brinkel Stefanie mwenye hati ya kusafiria ya Ujerumani na Catherine Janel Amquist Kinokfu, mwenye hati ya kusafiria ya Marekani. Uhamiaji imewataka raia wote wa kigeni wanaoingia nchini kwa madhumuni mbalimbali, kuzingatia matakwa yanayoainishwa katika viza au vibali vyao kuingia nchini.  

NHC na urithi wa Mwalimu Nyerere: Miaka 26 ya kuendeleza ndoto makazi bora kwa kila Mtanzania

Picha
- NHC chini ya Rais Dk. Samia imefufua falsafa ya utu ya Mwalimu Nyerere - Miaka 26 tangu kifo cha Baba wa Taifa, NHC inaendelea kuwa nguzo ya heshima, maendeleo na utu kwa Watanzania wote Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Kila inapowadia tarehe 14 Oktoba, Watanzania hukusanyika kwa heshima na kumbukizi ya maisha na kazi za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere Ikumbukwe kuwa Mwalimu Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999 katika Hospitali ya St. Thomas Jijini London Ni siku inayobeba hisia nzito, si tu kwa sababu aliongoza harakati za ukombozi, bali pia kwa sababu alisimamia maono ya kujenga taifa lenye utu, heshima na usawa. Miongoni mwa mambo yaliyokuwa karibu sana na moyo wake ni suala la makazi bora aliamini kwamba mtu hawezi kuishi kwa heshima bila nyumba salama na yenye hadhi. Kutokana na falsafa hiyo, mwaka 1962 Nyerere akiwa kiongozi wa Serikali ya Tanganyika (baadaye Tanzania) alianzisha Shirika la Nyumba...

ABSA, NHC waandika historia mpya ya makazi Tanzania

Picha
  - Benki ya ABSA yatembelea miradi ya kisasa ya NHC Dar es Salaam   - NHC yajengea wataalam ABSA uelewa, kuwezesha umiliki nyumba bora   - Ushirikiano sekta ya fedha, ujenzi matumaini mapya ya makazi endelevu Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ni asubuhi tulivu ya Ijumaa Oktoba 10, mwaka 2025. Magari kadhaa yenye nembo ya Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) na Benki ya ABSA Tanzania, yakipenya barabara za Jiji la Dar es Salaam, kuelekea kwenye miradi miwili mikubwa ya makazi inayotekelezwa na NHC, ambayo ni Samia Housing Scheme eneo la Kijichi na Kawe 711 Housing Project. Lengo la safari hiyo limewekwa wazi kuwa ni kujifunza, kushirikiana, na kujenga daraja kati ya sekta ya fedha ikiongozwa na ABSA kwa upande mmoja na NHC upande wa sekta ya ujenzi. Timu ya wataalamu wa ABSA imefanya ziara hiyo ili kujionea kwa macho ubora wa kazi ya NHC, kubaini fursa za biashara, lakini   zaidi ya yote, kufahamu jinsi mikopo ya nyumba inavyoweza kumsaidia Mtanzania wa ...

TEF: Tutamkumbuka marehemu Mbega kwa mchango wake kukuza tasnia

Picha
Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF) linasikitika kufangaza kifo cha Mwanachama wake Daniele Mbega, kilichotokea leo Oktoba 10,2025 alfajiri katika Hospitali ya Temeke alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuzidiwa. Marehemu Daniel Mbega Taarifa ya TEF iliyosainiwa na Mwenyekiti wake, Deodatus Balile, imeeleza kuwa mwili wa Mbega ambaye atakubukwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza tasnia ya habari nchini, utaagwa kesho Hospitali ya Temeke, dar es Salaam, kabla ya kusafirishwa kwenda Chigwingwili, Kongwa mkoani Dodoma kwa mazishi. Kwa taarifa zaidi soma taarifa ya TEF chini...  

Trump atimua kazi maelfu ya watumishi wa umma

Picha
Washington, Marekani. Serikali ya Rais Donald Trump nchini Marekani, imetangaza kuwaachisha kazi maelfu ya wafanyakazi ikiwa ni sehemu ya mpango wake mkubwa wa kupunguza wafanyakazi, unaohusiana na kufungwa kwa taasisi za Serikali. Rais Donald Trump wa Marekani Ofisi ya Usimamizi na Bajeti ya nchi hiyo (OMB) imeeleza katika hati za mahakama kuwa notisi ya kuachishwa kazi zimetumwa kwa takribani wafanyakazi 4,200 katika wizara na taasisi za serikali nane. Kwa mujibu wa Mtandao wa Forbs leo, hatua hiyo iliyoanza jana Oktoba 9-2025, inafuatia kesi iliyofunguliwa na Shirikisho la Wafanyakazi wa Serikali ya Marekani (AFGE), chama kikubwa zaidi cha wafanyakazi wa Serikali kinachowakilisha wafanyakazi 800,000 kufungua kesi ikipinga wafanyakazi hao kuachishwa kazi. Kwa mujibu wa OMB, karibu wafanyakazi 1,500 wa Wizara ya Fedha ya Marekani wameachishwa kazi, wakiwemo takribani wafanyakazi 1,300 kutoka Mamlaka ya Mapato ya Marekani (IRS), kama ilivyoripotiwa na Bloomberg. Wizara ya Afya na...

Papa Leo XIV: Uhuru wa kidini ni nguzo ya amani duniani

Picha
  -Alipongeza Shirika la Misaada kwa Kanisa kwa Kutetea Uhuru wa Kidini Roma, Italia.  Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Leo XIV amesema vitendo vya uhasama na vurugu dhidi ya watu wanaoshikilia imani na mitazamo tofauti, wakiwemo Wakristo vinaongezeka duniani na kwamba hakutakuwa na amani bila uhuru wa dini. Papa Leo wa XIV akibariki msalaba wakati wa mkutano na shirika la Aid to the Church in Need (CAN)Oktoba 10, 2025 . Baba Mtakatifu Leo XIV ametoa kauli hiyo katika hotuba yake alipokutana na wanachama wa shirika la kipapa Aid to the Church in Need International (CAN), ambao umefanyika Oktoba 9-2025, siku chache kabla ya kuchapishwa kwa Ripoti ya Uhuru wa Kidini Duniani itakayozinduliwa rasmi Oktoba 21 mwaka huu. Akinukuu maneno ya Papa Francis, Papa Leo amesema, “Hakutakuwa na amani bila uhuru wa dini, uhuru wa kufikiri, uhuru wa kujieleza, na heshima kwa maoni ya wengine.” Alisisitiza kuwa Kanisa Katoliki linatetea uhuru wa kidini kwa w...

Majaliwa: Bila walimu hakuna wataalam, hakuna viongozi wa kesho

Picha
  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa walimu ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote hapa duniani kwani ndio wanaotoa rasilimali watu yenye elimu ambayo ni muhimu zaidi kwa Taifa. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Amesema hayo  Oktoba 03, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani, yaliyofanyika Bukombe mkoani Geita kwenye U wanja wa Shule ya Sekondari ya Ushirombo. Majaliwa amesema kwamba mafanikio ya kielimu, kijamii na kiuchumi hutokana na juhudi za walimu kwa kuwa walimu ni fahari ya familia, jamii na taifa na kupitia mikono yao vijana wa kitanzania wanajengewa maarifa, stadi na maadili ya uzalendo. “Kila hatua ya ustawi wa kijamii na kiuchumi huanzia darasani, kupitia juhudi na maarifa ya walimu. Bila walimu, hakuna taaluma, hakuna viongozi wa kesho na hakuna Taifa linaloweza kusimama imara, walimu ndio chimbuko la uvumbuzi na ubunifu wa kizazi kipya,” amesema Majaliwa. Amesema kwa kutambua umuhimu wa kada ya ualimu nchini, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa...

NHC yazindua nyumba za kifahari Dar,Tanga, Tabora

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limezindua rasmi mauzo ya nyumba katika miradi mikubwa ya kisasa jijini Dar es Salaam na mikoa ya Tanga na Tabora. Uzinduzi huo umefanyika Makao Makuu ya NHC, Kambarage House, ukiongozwa na Meneja Mauzo na Masoko, Deogratius Batakanwa (pichani juu) , ambaye amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora, ya kisasa na yenye thamani ya kudumu. Katika Mkoa wa Dar es Salaam, NHC imezindua Boulevard Residence yenye nyumba za chumba kimoja (37.7 sqm), vyumba viwili (103.5 sqm) na vyumba vitatu (124.2 sqm).  Upo pia mradi wa Samia Housing Kijichi Residence ulio na nyumba za chumba kimoja (32.02 sqm), vyumba viwili (62.70 sqm) na vyumba vitatu (95.30 sqm). Kwa Mkoa wa Tanga, NHC inatangaza mauzo ya nyumba kwenye mradi wake wa Mkwakwani Plaza wenye nyumba za vyumba viwili (80 sqm) na vitatu (108 sqm), huku mkoani Tabora ikijenga Tabora Plaza yenye vyumba viwili (95 sqm) na vitatu (124 sqm)....

NHC yawapa siku 14 wapangaji waliokimbia na madeni kuyalipa, vinginevyo...

Picha
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), limetoa siku 14 kwa waliokuwa wapangaji wa nyumba za shirika hilo na kuhama huku wakiacha madeni, kulipa malimbikizo hayo kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria. Zaidi soma taarifa ya NHC hapa chini...  

Safari ya Mradi wa 2H wa NHC Morogoro

Picha
  -Kutoka mchanga hadi mnara wa matumaini katikati ya Moro -NHC yawekeza bil 2.5, yapandisha hadhi Mji kasoro bahari -Ni jengo linalobadilisha sura ya Morogoro Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Hakika sasa Morogoro ni mjini kasoro bahari, kwani katikati ya mji huo uliobeba historia ya kusifika ya milima inayotiririsha maji, utawala wa Chifu Kingalu wa Waluguru, wasanii wakongwe wa muziki nchini hata chimbuko la vipaji vya mpira nchini imesimikw alama mpya ya matumaini na maendeleo. Ukitaja historia ya Morogoro, huwezi kuwaweka kando wasanii maarufu wa muziki kuwataja wachache kama marehemu Mbaraka Mwishehe na Moro Jazz, lakini pia huiweki kando Cuban Marimba Band na marehemu Juma Kilaza. Lakini kwa mpira wa miguu huwezi kuwaacha Gibson Sembuli (marehemu), Husein Ngulungu(marehemu), Hamisi Gaga(marehemu) na Zamoyoni Mogella, tukiwataja kwa uchahe. Jengo hilo linaloongeza thamani ya Morogogro linajengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia Mradi wa 2H-Morogoro,...

FCC, ZFCC 'zafunga ndoa' kulinda haki za mlaji

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Ushindani Tanzania Bara -FCC na Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar -ZFCC, zimeingia mkataba wa makubaliano ambayo pamoja na mambo mengine, zinalenga kujielekeza katika kumlinda mlaji dhidi ya bidhaa feki. Makubaliano hayo yametiwa saini Jijini Dar es Salaam,  ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dk. Hashil Abdallah aliyeshuhudia tukio hilo, amezielekeza FCC na ZFCC kufanyia kazi mambo yote yaliyokusudiwa ili ziweze kuongeza ufanisi kwa maslahi mapana ya Tanzania. Amesema makubaliano hayo yanapaswa kujikita katika kutatua changamoto za ushindani ikiwemo kwenye sekta ya biashara na viwanda lengo ni kuleta uhimilivu toshelezi wa uchumi. “ Kwanza, FCC na ZFCC zinapaswa kuteua watu au timu maalum kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa makubaliano haya. Pia, ndani ya kipindi cha miezi mitatu—au hata chini ya mwezi mmoja—ni muhimu kutengeneza nyaraka kama ‘roadmap’ au ‘plan of action’ zitakazotuongoza katika ut...