Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2025

NHC yawapa siku 14 wapangaji waliokimbia na madeni kuyalipa, vinginevyo...

Picha
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), limetoa siku 14 kwa waliokuwa wapangaji wa nyumba za shirika hilo na kuhama huku wakiacha madeni, kulipa malimbikizo hayo kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria. Zaidi soma taarifa ya NHC hapa chini...  

Safari ya Mradi wa 2H wa NHC Morogoro

Picha
  -Kutoka mchanga hadi mnara wa matumaini katikati ya Moro -NHC yawekeza bil 2.5, yapandisha hadhi Mji kasoro bahari -Ni jengo linalobadilisha sura ya Morogoro Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Hakika sasa Morogoro ni mjini kasoro bahari, kwani katikati ya mji huo uliobeba historia ya kusifika ya milima inayotiririsha maji, utawala wa Chifu Kingalu wa Waluguru, wasanii wakongwe wa muziki nchini hata chimbuko la vipaji vya mpira nchini imesimikw alama mpya ya matumaini na maendeleo. Ukitaja historia ya Morogoro, huwezi kuwaweka kando wasanii maarufu wa muziki kuwataja wachache kama marehemu Mbaraka Mwishehe na Moro Jazz, lakini pia huiweki kando Cuban Marimba Band na marehemu Juma Kilaza. Lakini kwa mpira wa miguu huwezi kuwaacha Gibson Sembuli (marehemu), Husein Ngulungu(marehemu), Hamisi Gaga(marehemu) na Zamoyoni Mogella, tukiwataja kwa uchahe. Jengo hilo linaloongeza thamani ya Morogogro linajengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia Mradi wa 2H-Morogoro,...

FCC, ZFCC 'zafunga ndoa' kulinda haki za mlaji

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Ushindani Tanzania Bara -FCC na Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar -ZFCC, zimeingia mkataba wa makubaliano ambayo pamoja na mambo mengine, zinalenga kujielekeza katika kumlinda mlaji dhidi ya bidhaa feki. Makubaliano hayo yametiwa saini Jijini Dar es Salaam,  ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dk. Hashil Abdallah aliyeshuhudia tukio hilo, amezielekeza FCC na ZFCC kufanyia kazi mambo yote yaliyokusudiwa ili ziweze kuongeza ufanisi kwa maslahi mapana ya Tanzania. Amesema makubaliano hayo yanapaswa kujikita katika kutatua changamoto za ushindani ikiwemo kwenye sekta ya biashara na viwanda lengo ni kuleta uhimilivu toshelezi wa uchumi. “ Kwanza, FCC na ZFCC zinapaswa kuteua watu au timu maalum kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa makubaliano haya. Pia, ndani ya kipindi cha miezi mitatu—au hata chini ya mwezi mmoja—ni muhimu kutengeneza nyaraka kama ‘roadmap’ au ‘plan of action’ zitakazotuongoza katika ut...

Hospitali ya Shifaa yawshukuru wananchi

Picha
    - Yasema haibagui ipo kwa ajili ya Watanzania wote Mwandishi Wetu,  daimatznews@gmail.com Uongozi wa Hospitali ya Shifaa ya Dar es Salaam umewashukuru wananchi wanaofika hapo kupata huduma za afya, tiba na ushauri katika miaka miwili tangu kuanzishwa kwake, ikieleza kwamba inaunga mkono juhudi za Serikali kuboresha huduma za afya kwa watanzania wote wenye changamoto za kiafya na maradhi mbalimbali, ikiwamo wanaojigharamia kwa fedha taslimu hata walio na bima mbalimbali za afya ikiwamo ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Sehemu ya Jengo la Hospitali ya Shifaa iliyopo Kinondoni, Dar es Salaam linavyoonekana. Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Bashir Haroun ameeleza katika miaka miwili tangu kuanza kazi kwa hospitali hiyo bado msimamo wao ni kushikamana na malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kuwahudumia wnanchi wote bila kubagua. Hospitali hiyo ya kisasa ya Shirika ...