TEC yajitenga waraka feki, yatoa taarifa kwa umma
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Baraza la Maaskofu Katolini Tanzania (TEC), limekanusha kuhusika na waraka uliokuwa ukizagaa mitandaoni Oktoba 13,2025 ukilihusisha Baraza hilo na waraka usio wake na kusema hiyo ni tabia mbaya kutumia TEC na kutaka ikomeshwe.
![]() |
| Katibu Mkuu wa TEC, Padri Charles Kitima |
Taarifa ya TEC iliyotiwa saini na Katibu wake Mkuu, Padri
Charles Kitima imeeleza kuwa waraka huo wenye Kichwa cha Habari; TAMKO LA
BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC) KUHUSU AMANI KWA TAIFA KUELEKEA SIKU
YA UCHAGUZI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UTAKAOFANYIKA TAREHE 29
OKTOBA 2025. "SAUTI YA WATU SAUTI YA MUNGU" ni 'Fake'.
Padri Kitima amesema wanawatangazia Waamini na Watanzania
wote kwa ujumla kuwa waraka huo haukutolewa na
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. “Baraza halihusiki na hayo maudhui
yaliyomo kwenye andiko hilo,” amesema.
TEC kupitia taarifa yake kwa umma yenye kumbukumbu namba TEC/GEN/1/2025 iliyobeba kichwa cha habari; YAH WARAKA "FAKE" ULIOSAMBAZWA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII, imesema; "Tabia hii mbaya ya kutumia Taasisi ya Maaskofu kupitisha ujumbe zisizotokana na Baraza ikomeshwe. Tunawataka wenye tabia hiyo waache…”


Maoni
Chapisha Maoni