Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2023

Mkurugenzi Mkuu NHC alivyocheza nambari nane, tisa mikoani

Picha
 -Ni miezi minane tangu kuteuliwa -Atembelea mikoa tisa ya NHC Mwandishi Wetu, Bukoba Kwa wafuatiliaji wa mchezo wa mpira wa miguu yaani soka, anaelewa umuhimu wa namba nane na tisa kwenye mchezo huo, kwani anayecheza namba nane ndiye kiungo anayesukuma mpira kwa washambuliaji, huku namba tisa akisukuma mashambulizi na kufunga magoli. Hata hivyo, ingawa nafasi hizo za namba nane na tisa huchezwa na watu tofauti, lakini Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Hamad Abdallah ameweza kucheza nafasi hizo mbili peke yake katika kuhakikisha anatimiza majukumu yake ya kuliongoza shirika hilo la taifa. Mkurugenzi huyo amecheza nambari nane kwani Oktoba hii ametimiza miezi minane tangu alipoteuliwa na Rais Samia kuiongoza NHC   Februari 23, mwaka huu akichukua nafasi ya Nehemia Mchechu, ambaye ameteuliwa kuwa Msajili wa Hazina. Si hivyo tu, bali Hamad pia amehitimisha ziara ya mikoani ambapo ametoa maagizo na maelekezo nane yenye lengo la kulisukuma mbele shirika h...

Waziri Mkuu kwa Papa Francis

Vatican,  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea Vatican City, Makao Makuu ya Kanisa Katoliki duniani na kiongozi wa kanisa hilo, Papa Francis. Majaliwa na ujumbe wake, waliokuwa wakishiriki kwenye Mkutano wa Jukwaa la Kimataifa la Chakula Duniani, Maadhimisho ya Kumbukizi ya Miaka 78 tangu kuanzishwa kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) pamoja na Maadhimisho ya Siku ya 43 ya Chakula Duniani kwa Mwaka 2023. Mjini Vatican, Majaliwa na ujumbe alioongozana nao walitembelea Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican na kujionea Altare na Makaburi ya Mapapa wa Kanisa Katoliki.  Habari kutoka tovuti rasmi ya Vatican zinaeleza kuwa katika kanisa hilo, ndimo  Baba Mtakatifu huongoza Ibada mbalimbali kwa kipindi cha mwaka mzima.  Waziri Mkuu Majaliwa amefanya ziara hiyo Jumatano Oktoba 18, 2023, ambapo  alitembelea chini ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro,  mahali ambapo wamezikwa baadhi ya Mababa watakatifu. Akiwa eneo hilo, Waziri Mkuu aligu...

Birthday za wanawake zawadi kupima saratani

Picha
 - Waziri Ummy Mwalimu ashauri -Asema asilimia 50 saratani inatesa wanawake -Kila miaka 10 ongezeko asilimia 50 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amewataka wanawake wote wanaofikia umri wa miaka 30 kusherehekea siku zao za kuzaliwa kwa kujipa zawadi ya kupima saratani ya matiti na mlango wa kizazi. Akizungumza leo Oktoba 21,2023, alipokuwa mgeni rasmi kwenye matembezi ya   kuadhimisha Mwezi wa Kampeni ya Elimu Kuhusu Saratani ya Matiti, pamoja na miaka 60 ya uwepo wa Ubalozi wa Sweden nchini katika Viwanja vya Ocean Road, jijini Dar es Salaam, Waziri Ummy amesema takwimu zinaonyesha saratani inaongezeka kwa asilimia 50 kila baada ya miaka 10. ā€œKila mwanamke anayetimiza miaka 30 katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake, zawadi ya kwanza ujipe mwenyewe, uwe umepima saratani ya matiti na saratani ya mlango wa kizazi. Ukifikia miaka 40 walau upime saratani kila baada ya miaka miwili,ā€ amesema Ummy na kuongeza: ā€œTakwimu za Wizara ya Afy...

MO Dewji aongoza matajiri vijana Afrika

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu MO Dewji, ametajwa kinara kwa utajiri miongoni wafanyabiashara vijana barani Afrika, akiwa na utajiri unaofikia Dola za Marekani bilioni 1.5, sawa na takriban shilingi trilioni 3.75. Dewji pia anatajwa kuwa ndiye milionea kijana zaidi katika orodha hiyo ya matajiri kumi viana barani Afrika kufikia Oktoba 2023, akiwa na umri wa miaka 48. Anayemfuatia ana umri wa miaka 61 huku wa kumi akiwa na miaka 70. Kwa mujibu wa Mtandao wa Business Insider Africa,  utajiri wa Dewji, ambaye pia anamiliki asilimia 49 ya hisa katika Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, unatajwa kutokana na biashara mbalimbali anazozifanya ndani na nje ya Tanzania. Mfanyabiashara, Mohammed Dewji Ripoti hiyo inamtaja MO ambaye pia ni Mkurugenzi wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Limited (MeLT Group), anatajwa kushika nafasi ya 13 katika orodha ya matajiri wote barani Afrika. Mfanyabiashara maarufu hapa nchini Aliko Dangote(66) raia wa Nig...

'Maokoto' yapaa LATRA

 -Yafikia asilimia 32 Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), imefanikiwa kuongeza mapato (Maokoto), yake kwa asilimia 32 katika kipindi cha miaka mitatu kutoka shilingi bilioni 25.95 hadi Sh. bilioni 34.17. Akizungumza katika Mkutano na Wahariri wa Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam leo Oktoba 19, 2023, Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, CPA Habibu Suluo amebainisha hayo. "Katika kipindi cha miaka mitatu ya utekelezaji wa majukumu ya LATRA, mwaka wa fedha 2020/21 hadi 2022/23, mapato ya yameongezeka kutoka Sh. bilioni 25.95 hadi Sh. bilioni 34.17" amesema Suluo. Amefafanua kuwa mapato hayo ni kabla ya kukaguliwa na CAG ikiwa ni ongezeko la Sh. bilioni 8.22 sawa na ongezeko la asilimia 32.  Katika mkutano huo ulioratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina, bosi huyo wa LATRA amesema: "Kipindi cha mwaka wa fedha 2020/21 hadi 2021/22, mapato ya LATRA yaliongezeka kutoka Sh. bilioni 25.945 hadi Sh. bilioni 28.53 ikiwa ni ongezeko la Sh....

BOT yahadharisha Dola feki

-Yaeleza kukamatwa shehena kuja Afrika  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com  Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imetoa tahadhari kwa wamiliki wa maduka ya kubadilishia fedha na wafanyabiashara kuhusu kuwepo kwenye mzunguko kwa fedha za Marekani (Dola) zilizoisha muda wake. Kupitia barua yake kwenda kwa benki na maduka ya kubadilishia fedha iliyo na kumbukumbu namba FD.69/130/01//61 BOT imesema, ina taarifa ya kukamatwa kwa shehena ya kiasi kikubwa cha dola zilizoisha muda wa matumizi. Kwa mujibu wa BOT, fedha hizo zinatoka katika moja ya nchi ughaibuni, kuja Afrika. " Kutokana na jambo hilo, benki zote na maduka ya kubadilishia fedha yanatakiwa kuchukua tahadhari zote ikiwamo kuimarisha mifumo ya utambuzi noti bandia," imetahadharisha BOT na kuongeza: " Benki na maduka yote ya kubadilishia fedha, yanashauriwa kuendelea kuwaelimisha wateja kuhusu madhara ya kubadilisha fedha kwa kutumia mifumo isiyo rasmi ili kuepuka uwezekano wa kupewa dola feki." Onyo hilo la BOT limeku...

'Mafiga' manne yaikweza TIB

-Yanufaisha kampuni kubwa -Sekta binafsi yaongoza  Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Benki ya Maendeleo (TIB) imefanikiwa kutekeleza  majukumu yake manne ya msingi (mafiga), ambapo sasa imefikia uwekezaji wa shilingi bilioni 980. Akizungumza katika mkutano wake na wahahriri wa vyombo vya Habari chini ya usimamizi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Oktoba 16, 2023, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIB,  Lilian Mbassy amesema benki hiyo imetekeleza malengo hayo kwa ukamilifu hata kufikia uwekezaji huo wa shilingi bilioni 980.  Utekelezaji kikamilifu wa majukumu hayo sasa umeweza kuipaisha benki hiyo siyo tu kufikia uwekezaji wa shilingi bilioni 980, bali sekta binafsi kuongoza kufaidika. Katika mkutano huo, pamoja na mambo mengine, Mbassy ametaja 'mafiga' manne iliyopewa TIB kisheria kuwa ni pamoja na kuwezesha upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu na wa kati kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi, kutoa msaada wa kiufundi na ushauri kwa ajili ya kuwezesha maendeleo ya viwanda. ...

Hatari, pigo jipya kiafya

-Ni  Homa ya Moyo ya Rumatiki -Wataalam wasema un aongoza kwa vifo -Waitana Abu Dhabi kuujadili Exuperius Kachenje, daimanews@gmail.com NI pigo, ni hatari mpya kiafya. Ndivyo unavyoweza kusema kwa kifupi, baada ya wataalam wa afya kubainisha uwepo wa Ugonjwa wa Moyo wa Rumatiki nchini, unaotajwa kuongoza kwa kusababisha vifo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mahojiano maalum na DaimaTanzania mapema juma hili jijini Dar es Salaam, Profesa Pilly Chillo wa Kituo cha Umahiri cha Kufundishia na Kufanya Tafiti za Magonjwa ya Moyo cha Afrika  Mashariki na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dk.Samwel Rweyemamu wamebainisha tatizo hilo, wakieleza ni kubwa. Wataalam hao wamesema ugonjwa wa Moyo wa Rumatiki unaogoza kwa kusababisha vifo kutokana na matatizo ya moyo kushindwa kufanya kazi vizuri kitaalam 'Heart failure'. Mahojiano na wataalam hao yamefanyika kwa nyakati tofauti katika taasisi ya moyo JKCI na Hospitali ya Taifa Muhimb...

Wanaume asilimia 6 waugua saratani ya matiti

Picha
  -Ubalozi wa Sweden, SCF nguvu moja Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Asilimia 6.5 ya wagonjwa wote wa saratani nchini wametajwa kuwa ni wanaume, ikielezwa kwamba idadi hiyo ni mara kumi zaidi inayoonekana nchi nyingi duniani. Balozi wa Sweden nchini, Charlotta Ozaki amebainisha hayo katika mkutano wake na wanahabari katika ofisi za ubalozi huo Dar es Salaam Oktoba 13, 2023, ambapo pamoja na maadhimisho ya miaka 60 ya ubalozi huo nchini, alizungumzia ushiriki wao katika kampeni ya kupambana na saratani ya matiti nchini. Balozi wa Sweden nchini Charlota Ozaki akiteta jambo na Mkurugenzi wa asasi ya Shujaa cancer Foundation (SCF) ya Dar es Salaa wakati wa mkutano na wanahabari kwenye ofisi za ubalozi wa Sweden kuhusu Madhimiso ya Miaka 60 ya Ubalozi wa Sweden nchini na Mwezi Oktoba wa Kampeni ya Saratani ya Matiti.     ā€œTunataka kuongeza ufahamu kuhusu saratani ya matiti kwa wanaume hata wavulana na kuwasaidia wanawake. Tunataka watu wajifunze, saratani y...

ACT WAKAZIA MACHO UKATILI KWA MTOTO WA KIKE

Picha
Wataka uendeshaji kesi upunguzwe Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Chama cha ACT Wazalendo kimetoa wito kwa Serikali na vyombo vyake vya dola kupunguza muda wa uendeshaji wa kesi za ukatili dhidi ya watoto na wanawake. Kimependekeza muda wa uendeshwaji wa mashauri hayo usizidi miezi miwili hadi kumalizika kwake ili haki ionekane kutendeka. Ushauri huo umetolewa leo Oktoba 11, 2023 jijini Dar es Salaam na Waziri Kivuli wa Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto wa ACT, Janeth Rithe. "Ukatili dhidi ya watoto wa kike bado upo katika jamii, zinahitajika mbinu mbalimbali za kuukabili ikiwa ni pamoja na kesi zinazohusu vitendo hivyo kusikilizwa na kamilika katika muda mfupi tofauti na sasa ambapo zinachukua muda mrefu," ameema Rithe. Waziri Kivuli wa Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe.   Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa kike Duniani, ACT imetaja changamoto kubwa zinazowakabili...

Msemaji wa Serikali aikosoa Ifakara

Picha
 

Kumbe 15% ya Watanzania ni 'magolikipa'!?

 - 13% pekee wana uhakika wa kipato -Wewe upo kundi gani ? Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Asilimia 15 ya Watanzania, wanaishi kwa kutegemea pesa za kupewa kwa kutumiwa au kudakishwa kama magolikipa kutoka kwa ndugu, jamaa, au marafiki, ili kuendesha maisha yao ya kila siku, utafiti umebainisha. Taarifa ya utafiti unaojulikana kwa jina la Finscope Tanzania 2023, ambao umetolewa na Wizara ya Fedha hivi karibuni imebainisha hayo na kwamba fedha hizo hutumwa kupitia mifumo rasmi iliyopo. FinScope Tanzania ni utafiti wa kina wa mahitaji ya sekta ya fedha kwa watu wazima Tanzania, walio na umri wa kuanzia miaka 16 na kuendelea. Umeonyesha pia kwamba, asilimia 13 pekee ya Watanzania, ndio wenye vyanzo vya mapato vinavyowalipa kwa uhakika, mara kwa mara. Utafiti huo uliolenga kujua na kutoa taarifa za hali ya matumizi ya huduma za fedha nchini, unatajwa kuwa ni kipimo cha kuaminika kubaini mahitaji na matumizi ya huduma za fedha kwenye makundi mbalimbali ya watu. Matokeo ya utafiti ...

Serikali yasifu utendaji Kagera

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Serikali kupitia Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Toba Nguvila imeisifu Menejimenti  ya Hospiatali ya Rufaa ya Mkoa huo kwa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi. Nguvila ametoa sifa hizo Oktoba, 6 mwaka 2023, alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Bukoba (BRRH) na kuzungumza na watumishi wa hospitali hiyo kuhusu masuala mbalimbali ya utumishi na utendaji kazi.  Katibu Tawala Mkoa wa Kagera, Toba Nguvila akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa Bukoba. ā€œNawapongeza watumishi wote wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Bukoba hasa Mganga  Mfawidhi wa hospitali hii kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kunusuru maisha ya Watanzania. Binafsi nimekuja mara nyingi katika hospitali hii kupata huduma, lakini nimekuwa nikipokelewa vizuri na majibu ya vipimo yanatoka kwa wakati, hongereni sana,ā€amesema Nguvila. Ofisa Tawala huyo wa mkoa amesema kwa sasa hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa, Bukoba inaendelea kukua na kupanuka katika utoaji wa h...

TASAC yaja na 'Big3', fursa lukuki

Picha
-Victoria, Nyasa, Tanganyika kucheka  Exuperius Kachenje, daimatzanews@gmail.com  Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), limejipanga kupunguza na kuzuia athari za ajali majini, ikitangaza miradi mitatu mikubwa, ikiwamo wa ujenzi wa boti tano za uokoaji katika Ziwa Victoria,Tanganyika na Ziwa Nyasa.   Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TASAC, Nelson Mlali, (Aliyesimama kulia), akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari, kuhusu utendaji, mikakati mafanikio na changamoto za shirika hilo, jijini Dar es Salaam Oktoba 5, 2023. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TASAC, Nelson Mlali ameeleza hayo leo Oktoba 5,2023 wakati akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na utekelezaji wa miradi mitatu mikubwa (Big 3), alitaja pia fursa sita zilizopo katika sekta ya usafiri kwa njia maji Tanzania.  Kuhusu hatua ya TASAC kupunguza na kuzuia athari za ajali majini, Mlali amesema: "Shirika linaendelea na utekelezaji wa miradi mitatu mikuu ikiwamo ujenz...

Rais Dk. Samia afanya uteuzi tena

Picha

TEF wamshukuru Rais, wampongeza Mobhare

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Mobhare Matinyi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali. TEF pia imempongeza mteule huyo kwa kuaminiwa na Rais kushika wadhifa huo, ikieleza kuwa ina matarajio kwamba atakuwa kiunganishi kati ya vyombo vya Habari na Serikali. "TEF tunamshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanya uteuzi wa mtu sahihi kushika wadhifa huu, baada ya aliyekuwapo, ... Gerson Msigwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu,"imeeleza sehemu ya taarifa ya TEF iliyosainiwa na Mwenyekiti wake, Deodatus Balile Oktoba 2, 2023. Kupitia taarifa hiyo TEF iliongeza: "Msemaji Mkuu wa Serikali ndiye Mshauri Mkuu wa Masuala ya Habari serikalini. Tunaamini ataifanya kazi hii kwa ustadi wa hali ya juu na kwa ufasaha." Iliongeza kuwa pamoja na mambo mengine,kuna uundwaji wa vyombo vinavyoanzishwa kisheria kupitia Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 k...

Mobhere ateuliwa Msemaji Mkuu wa Serikali

Picha

CCM nao watua Mtambwe

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimetua katika Jimbo la Uchaguzi Mtambwe, Zanzibar kwa kumteua kada wake, Hamad Khamis Hamad kuwania kiti cha uwakilishi. Jimbo la Mtambwe linatarajiwa kufanya uchaguzi mdogo Oktoba 28 mwaka huu, kufuatia kifo cha aliyekuwa mwakilishi wake, Habib Mohammed Ali, aliyefariki mwezi Machi mwaka 2023. Taarifa ya uteuzi huo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM imetangazwa Oktoba Mosi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Sophia Mjema, kufuatia kikao chake maalum. Hamad anatarajiwa kupambana na wagombea kutoka vyama vingine ikiwamo Dk Mohammed Ali Suleiman wa ACT Wazalendo, kilicho na ushindani mkubwa na CCM visiwani Zanzibar.

ACT wateua mgombea Mtambwe

Picha
Chama cha ACT Wazalendo kimeanza safari kuliwania tena Jimbo la Uwakilishi Mtambwe, kwa kumteua Dk. Mohammed Ali Suleiman pichani chini, kuwa mgombea wa kiti hicho. Tayari Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imetangaza tarehe 28 Oktoba kuwa ndiyo siku ya uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwakilishi wake, Habib Mohammed Ali, Machi 3, mwaka huu.