Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Wanaume asilimia 6 waugua saratani ya matiti

 -Ubalozi wa Sweden, SCF nguvu moja





Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com

Asilimia 6.5 ya wagonjwa wote wa saratani nchini wametajwa kuwa ni wanaume, ikielezwa kwamba idadi hiyo ni mara kumi zaidi inayoonekana nchi nyingi duniani.

Balozi wa Sweden nchini, Charlotta Ozaki amebainisha hayo katika mkutano wake na wanahabari katika ofisi za ubalozi huo Dar es Salaam Oktoba 13, 2023, ambapo pamoja na maadhimisho ya miaka 60 ya ubalozi huo nchini, alizungumzia ushiriki wao katika kampeni ya kupambana na saratani ya matiti nchini.

Balozi wa Sweden nchini Charlota Ozaki akiteta jambo na Mkurugenzi wa asasi ya Shujaa cancer Foundation (SCF) ya Dar es Salaa wakati wa mkutano na wanahabari kwenye ofisi za ubalozi wa Sweden kuhusu Madhimiso ya Miaka 60 ya Ubalozi wa Sweden nchini na Mwezi Oktoba wa Kampeni ya Saratani ya Matiti.  

“Tunataka kuongeza ufahamu kuhusu saratani ya matiti kwa wanaume hata wavulana na kuwasaidia wanawake. Tunataka watu wajifunze, saratani ya matiti sio ugonjwa wa wanawake tu, wanaume pia huathiriwa,” alibainisha Ozaki.

 Balozi huyo alisema: “ Ni muhimu kwetu kuwepo hapa, mwezi huu Oktoba ni mwezi wa saratani ya matiti. Tupo hapa ili kusisistiza umuhimu wa kuongeza uelewa kuhusu saratani ya matiti na aathari zake kwa jamii ya Watanzania.”

Kwa mujibu wa Balozi Ozaki mwezi huo wa Oktoba ni muhimu kwao  kwani kwa kushirikiana na taasisi ya Shujaa Cancer Foundation(SCF), Wizara tya Afya kampuni ya kiswidi ya ELEKTA, Taasisi ya Saratani Ocean Road(ORCI) na Shirika la Afya Duniani, wameandaa matembezi ya kilometa sita ili kukusanya fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya saratani ya matiti, yatakayofanyika oktoba 21 viwanja vya ORCI.

Amesema saratani ya matiti ndiyo chanzo kikuu cha vifo vinavyohusiana na saratani kwa wanawake duniani na kwamba wakati mwezi huo wa saratani ya matiti unapoadhimishwa  makadirio ya hivi karibuni yanaonyesha kuwapo kwa wagonjwa wapya takriban milioni mbili na laki moja kwa mwaka.

 “Zaidi ya vifo 600,000 vinaripotiwa kila mwaka, huku asilimia 80 ya wagonjwa wa saratani ya matiti nchini Tanzania wakigundulika wakati tayari wamefikia hatua ya tatu au nne, hali inayochangiwa na kukosekana kwa programu za uchunguzi, utambuzi na matibabu duni kama vile chemotherapy, upasuaji na tiba ya mionzi,” amesema.

Balozi huyo ambaye pia ni shujaa wa saratani ya matiti, amesema pia kwamba nchini Tanzania, saratani ya matiti imeripotiwa kwa kiasi kidogo katika miongo miwili iliyopita, huku kukiwa pia na tafiti chache.

Balozi huyo amesema iwapo hakutakuwa juhudi za dhati, ongezeko la visa vipya vya saratani Tanzania linakadiriwa kufikia asilimia 82 ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza matembezi hayo ya Oktoba 21,  Mkurugenzi Mtendaji wa SCF, Gloria Kida amesema yanalenga kukuza uelewa kuhusu umuhimu wa kupima saratani ya matiti na kujipima, pamoja na kusaidia walioathirika, umuhimu wa utafiti, kuzuia, matibabu na kupona.

Kida amesema, pamoja na maadamano hayo, wameandaa fulana maalum, zitakazouzwa katika vituo vitakavyokuwapo Dar Free Market na Shoppers Plaza akitaja mawasiliano ya namba za simu 0745 538079 kuwa yatasaidia anayehitaji kupata fulana hizo na fedha zitakazopatikana zitatumika kununulia vifaa vya mazoezi kwa wagonjwa wa saratani.

Amesema watajifunza pia kuhusu teknolojia ya kisasa zaidi katika uchaguzi wa saratani nchini iliyofadhiliwa na kampuni ya ELEKTA ya Sweden.

Amesema ni muhimu kila mmoja akaonyesha mshikamano na kusaidia wagonjwa na waathirika wa saratani ya matiti bila kuwasahau wahudumu wa saratani.

 

Chapisha Maoni

0 Maoni