'Hatutawavumilia wanaokwamisha wawekezaji'

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango amesema Serikali haitasita kuchukua hatua kwa watumishi wataobainika kushiriki kukwamisha wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini, huku akitaja hatua nne walizochukua ili kuvutia wawekezaji. Dk. Mpango amesema hayo mkoani Dar es Salaam Machi 27, 2024 wakati akifunga la Kongamano la Uwekezaji kati ya China na Tanzania, lililokutanisha zaidi ya kampuni 300 za mataifa hayo, kujadili fursa mbalimbali za uwekezaji. Makamu wa Rais Dk. Phillip Mpango akifunga la Kongamano la Uwekezaji kati ya China na Tanzania, lililokutanisha zaidi ya kampuni 300 za mataifa hayo, kujadili fursa mbalimbali za uwekezaji. Makamu wa Rais amesema, kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya watumishi wa umma kukwamisha wawekezaji kwa kuendekeza urasimu na rushwa, jambo ambalo hawapo tayari kuvumilia. “Napenda kuchukua nafasi hii, kuwaagiza watumishi wa umma ambao mnashiriki mchakato wa uwekezaji na nitumie nafasi hii kuwaomba wawekezaji ambao watakuta...