Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2024

'Hatutawavumilia wanaokwamisha wawekezaji'

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango amesema Serikali haitasita kuchukua hatua kwa watumishi wataobainika kushiriki kukwamisha wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini, huku akitaja hatua nne walizochukua ili kuvutia wawekezaji. Dk. Mpango amesema hayo mkoani Dar es Salaam Machi 27, 2024 wakati akifunga la Kongamano la Uwekezaji kati ya China na Tanzania, lililokutanisha zaidi ya kampuni 300 za mataifa hayo, kujadili fursa mbalimbali za uwekezaji. Makamu wa Rais Dk. Phillip Mpango  akifunga la Kongamano la Uwekezaji kati ya China na Tanzania, lililokutanisha zaidi ya kampuni 300 za mataifa hayo, kujadili fursa mbalimbali za uwekezaji. Makamu wa Rais amesema, kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya watumishi wa umma kukwamisha wawekezaji kwa kuendekeza urasimu na rushwa, jambo ambalo hawapo tayari kuvumilia. “Napenda kuchukua nafasi hii, kuwaagiza watumishi wa umma ambao mnashiriki mchakato wa uwekezaji na nitumie nafasi hii kuwaomba wawekezaji ambao watakuta...

Wachambua miaka 3 ya Dk. Samia, waishauri

Picha
  Hellen Ngoromera, daimatznews@gmail.com Miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan madakani imetajwa kuimarisha na kukuza demokrasia nchini, huku wasomi wakiishauri Serikali kuboresha maisha ya wananchi kiuchumi. Rais Samia ametimiza miaka mitatu madarakani tangu alipotwaa madaraka ya kuiongoza Tanzania Machi 19, 2021, kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Rais John Magufuli Machi 17,2021. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana Machi  26 katika mjadala wa uchambuzi wa miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia madarakani ulioandaliwa na Kampuni ya Mchambuzi Media, Mchambuzi wa masuala ya kisiasa Dk. Denis Muchunguzi na Profesa Samuel Wangwe wameeleza hayo. "Napongeza miaka mitatu ya  Dk. Samia kwani amefanya makubwa... tumeshuhudia mikutano ya kisiasa ikiruhusiwa, maandamano ya Chadema kwenda Umoja wa Ulaya yalifanyika bila bugudha," amesema Dk. Muchunguzi. Ameongeza kuwa katika miaka mitatu hiyo hata baadhi ya watu wakiwemo wanasiasa waliohama nchini ...

Wanaumee, hii hatari

-Takwimu zawataja kujamiiana zaidi Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Karibu nusu ya wanaume Tanzania, wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 49, walifanya mapenzi na mwanamke zaidi ya mmoja ndani ya miezi 12, wakati asilimia nne pekee ya wanawake wenye umri kama huo, walifanya mapenzi na wanaume tofauti kwa kipindi hicho. Matokeo ya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 inayopatikana Ofisi ya Taifa ya Takwimu, yamebainisha hayo yakieleza kwamba, asilimia 21 ya wanawake walijamiiana na watu ambao ama walikuwa w waume zao au waliishi nao.   “Kati ya wanawake hao, asilimia 22 walitumia kondom mara ya mwisho walipojamiiana na wenza wao hao,” ripoti hiyo inaweka wazi.   Kwa mujibu wa ripoti hiyi ya utafiti, asilimia 38 ya wanaume walijamiiana na watu ambao ama ni wake zao au waliowahi kuishi nao, huku asilimia 43 ya wanaume hao wakitumia kondom mara ya mwisho walipojamiiana na wenza wao.   Kuhusu kupima Virusi vya Ukimwi (HIV),...

Anne Makinda: Sensa ni kiboko kwa wanasiasa

Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Makinda amewataka wanasiasa kutofurahia tu matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, badala yake watambue kuwa inaweza kuwa kiboko kwao. Makinda ambaye pia ni Kamisaa wa Sensa nxhini, ametoa kauli hiyo leo Machi13,2024 jijini Dar es Salaam alipokuwa mgeni rasmi katika mafunzo ya waandishi wa habari, kuhusu matumizi ya takwimu za sensa ikiwa ni sehemu ya awamu ya tatu ya utekelezaji Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022. "Tumewaambia wanasiasa wenzagu, sensa hii imefanikiwa. Lakini, kwenu ni kiboko, shangilieni lakini watu watakuwa wanauliza maswali kutokana na takwimu na maelezo yaliyomo kwenye matokeo ya sensa. Sisi tunafundisha mpaka chini kwa wananchi," amesema Makinda. Spika mstaafu huyo, ametoa onyo hilo kwa wanasiasa wakati ambapo taifa linatarajia kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu 2024 na Uchaguzi Mkuu mwakani 2025. Amebainisha kuwa kutokana na wananchi kupata uelewa kuhusu mat...

Waandishi wa habari wambwaga Mbowe kortini

 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, amebwagwa kortini na waandishi wa habari 10, wanaomdai mtoto wake katika kesi aliyofungua kutaka wamlipe gharama kwa kukamata nyumba yake. Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi leo Machi 13 2024 mbele ya Naibu Msajili Mary Mrio kufuatia  maombi ya Mbowe, yaliyowasilishwa kwa hati ya dharura chini ya kiapo cha Mbowe, aliyewakilishwa na Wakili John Mallya. Uamuzi huo wa Mahakama umetolewa baada ya kupitiwa hoja zote za mleta maombi. Hoja hizo za Mbowe ziliwasilishwa na Mbowe kupitia Wakili wake John Mallya, ambapo Mrio amesema mahakama iliona hakuna ubishi katika maombi ya kuiachia nyumba na kwamba kinachobishaniwa ni mleta maombi (Mbowe), kulipwa gharama za kesi na wajibu maombi, ambao ni waandishi wa habari 10 na dalali wa mahakama. Mrio amesema: "Mahakama iliangalia katika kesi hii kama gharama zilipwe au zisilipwe. Nimepitia Gazeti la Serikali (GN) namba 106 la mwaka 200...

Jafo: Miradi huchochea uwezo wa wananchi

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Selemani Jafo amesema miradi mbalimbali ya mazingira imechangia kuwajengea wananchi uwezo katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Selemani Jafo  akiwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya Urejeshwaji wa Mazingira, Bayoanuai Tanzania na Hifadhi Endelevu ya Ardhi katika Bonde la Ziwa Nyasa mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Machi 12, 2024 jijini Dodoma. Ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Urejeshwaji wa Mazingira na Hifadhi ya Bayoanuai Tanzania (SLR) unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Pia aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Hifadhi Endelevu ya Ardhi katika Bonde la Ziwa Nyasa (SLM-Nyasa) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira katika kikao kilichofanyika Machi 12, 2024 jijini Dodoma. Dk. J...

Mfuko wa Self wakopesha bil 324 wananchi 300,000

Selemani Msuya, daimatznews@gmail.com MFUKO wa Self umetoa mikopo ya zaidi ya Sh bilioni 324 kwa wananchi 314,055 wa mikoa 30 nchini huku ukijipanga kupanua wigo siku zijazo. Mfuko pia umesema katika mikopo iliyotoa kiwango cha mikopo chechefu ni chini ya asilimia 10, huku wakijipanga kukabiliana na changamoto ya mikopo kaushadamu. Hayo yamesemwa Machi 12,2024 na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Self, Mudith Cheyo alipozungumza kwenye mkutano wa 53 wa ya taasisi hiyo na wahariri wa vyombo vya habari Dar es Salaam, kupitia uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina. Cheyo amebainisha kwamba, hadi Desemba 31 mwaka jana, mfuko huo unaotarajia kuwezesha wananchi wengi kwa mikopo, ulifikia zaidi ya wananchi 300,000; wanawake 166,449 sawa na asilimia 53 na wanaume 147,606 sawa na asilimia 47. Ameongeza kuwa Self pia umekopesha na kuzijengea uwezo taasisi ndogo 200 za fedha na kutengeneza ajira 37,024 kwa mwaka jana na kutoa elimu kwa wakopaji 1,519. Ofisa Mtendaji huyo amesema katika kipindi cha m...

Rais Samia aigusa CCM

Picha
 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi akikigusa Chama Cha Mapinduzi(CCM), kwa kumteua Naibu Katibu Mkuu wake, Anamringi Macha, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Kwa hatua hiyo, kuna uwezekano kwa CCM kumteua na kumpitisha mtu mwingine kushika nafasi ya unaibu katibu mkuu, badala ya Anamringi. Anamringi anachukua nafasi ya Christina Mndema, ambaye ameteuliwa na Rais kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus leo Machi 12,2024, imeeleza kuwa mbali na uteuzi wa wawili hao, Rais Samia pia amefanya uteuzi na uhamisho wa watendaji mbalimbali, wakiwamo wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji wa halmashauri na makatibu tawala wa wilaya. Taarifa hiyo ya Ikulu, imeeleza kuwa uapisho wa wakuu wa mikoa na naibu katibu mkuu, utafanyika kesho saa 4 asubuhi Ikulu Dar es Salaam. Habari zaidi soma orodha ya watbyeule na nafasi zao katika kiambatanis...

Kesi ya Jalakhan yapigwa kalenda Nzega

 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com MAHAKAMA ya Mwanzo Nzega imeendelea kulipiga kalenda shauri la  Mirathi ya Zena Jalakhan lenye mvutano wa ndugu katika kusimamia mirathi hiyo. Shauri hilo lipo mbele ya Hakimu Mfawidhi, Abunas Sonyo, ambapo jana liliahirishwa kwa mara nyingine hadi Aprili 23 kwa ajili ya kusikiliza pingamizi. Mmoja wa wanafamilia, Salma Mohammed katika shauri hilo anayewakilishwa na Wakili Kaumuliza David awali aliomba apewe muda wa kupitia jalada la shauri hilo la mirathi na mahakama ilikubali maombi hayo. Lakini jana, shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikiliza mapingamizi, lakini upande wa Karim Samji ambaye awali aliyekuwa msimamizi wa mirathi, aliomba shauri lisiendelee kwa sababu wakili wao hakuwepo mahakamani. Karim alidai Wakili wao hakuwepo kwa sababu hakujua mahakamani shauri linaloendelea ni lipi na baada ya Mahakama kuwafahamisha kwamba kinachoendelea ni usikilizwaji wa mapingamizi, waliomba kuahirisha. Wakili Kaumuliza aliomba Mahakama iahir...

Mbowe kusuka au kunyoa kortini kesho

 Mwandishi Wetu,  daimatznews@gmail.com Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kesho Machi 13,2024 'atasuka au kunyoa'. Ndivyo unavyoweza kusema, wakati Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi itakapotoa uamuzi wa shauri alilofungua Mbowe kuwadai gharama waandishi wa habari 10, wanaomdai mtoto wake Dudley. Leo waandishi wa habari 10 wanaomdai Dudley ambaye ni Mkurugenzi wa Tanzania Daima, Sh milioni 62.7 wameachia nyumba ya Freeman Mbowe waliyoikamata ili kuipiga mnada kufidia deni lao. Hata hivyo, wamegoma kulipa gharama za kesi zilizoombwa na Mbowe wakieleza sababu hata wao wameingia gharama katika kudai haki yao. Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi ilisikikiza shauli hilo mbele ya Naibu Msajili, Mary Mrio leo Machi 12,2024 ikieleza itatoa uamuzi kuhusu gharama kesho saa 8 mchana. Mbowe kupitia Wakili wake John Mallya aliwasilisha maombi chini ya kiapo kilichoapwa na Freeman Mbowe Februari 26 mwaka huu, akitaka wajibu maombi kuondoa nyumba hiyo kwa sababu si mali ya Dudley na Ma...

NEEC, wanawake 5000 kumpongeza Rais Samia Dar

Mwandishi Wetu daimanewstz@gmail.com Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za wanawake nchini wameandaa hafla maalumu ya kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan na kutambua umahiri wake wa kuwa mwanamke kinara kwa masuala ya nishati safi ya kupikia na utunzaji wa mazingira. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  Machi 9, 2024, Katibu Mtendaji wa  NEEC, BengI Issa hafla hiyo ambayo itahudhuriwa  pia na  Rais Samia itafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee sambamba na kumpongeza kwa ujasiri na uthubutu wake. “Hii ni fursa ya kipekee kwa wanawake wa Mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kwenye  hafla hiyo maalumu ya kutambua kuwa Rais Samia Suluhu ni mwanamke kinara wa masuala ya nishati safi ya kupikia na utunzaji wa mazingira,” amesema. Issa amesema Rais Samia kwa ujasiri wake, mbali ya kuwa mwanamke kinara kwenye masuala nishati safi ya kupikia na utunzaji wa mazingira nchini, amefanik...

Chongolo arejea kivingine

Picha
 -Aendelea kuaminiwa kuitumikia CCM Exuperius Kachenje, daimanewstz@gmail.com Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, amerejea madarakani kwa namna nyingine, safari hii akiteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe.  Uteuzi wa Chongolo umefanywa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan leo na kutangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Dk. Moses Kusiluka. Taarifa hiyo ya Katibu Mkuu Kiongozi, umetaja pia wateule wengine na ukuu wa mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, sanjari na uhamisho wa watendaji wa nafasi hizo. Chongolo anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe kutoka nafasi ya ukatibu mkuu wa CCM, aliyojiuzulu Novemb mwaka 2023 kwa kilichoelezwa ni kutokana na kuchafuliwa mtandaoni, jambo ambalo Rais Samia alisema linachunguzwa. Hata hivyo, uteuzi huo unaweza kuelezwa kwamba Rais amejiridhisha na usafi wa Chongolo, ambaye alibeba jukumu la kuwajibika baada ya kuchafuliwa.  Unaweza kuelezwa pia ni wa kimkakati, utakaomfanya Chongolo aendelee kuitumikia CCM, akiwa Mkuu wa Mkoa ...

ACT yataka kuwakutanisha Rais Samia, Dk.Mwinyi Z'bar

 Makuburi Ally CHAMA cha ACT Wazalendo kinatarajia kuwakutanisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ikiwamo nia ya chama hicho kujitoa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar (GNU). Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu  amesema hayo leo Machi 8,2024 mbele ya waandishi wa habari akieleza kwamba hatua hiyo ni zao la kikao cha Halmashauri Kuu Taifa ya ACT Wazalendo iliyokutana Machi 4 mwaka huu, makao makuu ya chama hicho, Magomeni jijini Dar es Salaam. Amesema uwepo wa GNU ni utulivu wa kiuchumi, utalii, mikopo, biashara na kwamba roho ya uchumi wa Zanzibar inategemea utulivu. "Kikao cha Halmashauri Kuu Taifa kilifanya tafakuri ya kina juu ya mwenendo na mwelekeo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar," amesema Shaibu. Amebainisha kuwa Serikali hiyo ni matakwa kisheria kwa hoja tatu ambazo ni kuachiwa huru kwa viongozi wote wa ACT walioshikiliwa, watuhumiwa hao ni la...

Diamond ajipeleka BRELA

Picha
-Aelimishwa kuhusu ulinzi wa kazi zake  Mwandishi Wetu, daimanewstz@gmail.com Mwanamuziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz ametembelea Ofisi za BRELA jijini Dar es Salaam Machi 7, 2024, ambapo amekutana na kuzungumza na  Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa ambapo alipata elimu kuhusu ulinzi wa kazi na chapa zake .  Akizunguza baada ya mkutano wake na Nyaisa, Diamond amesema mbali na kuwa mwanamuziki yeye ni mfanyabiashara na mwekezaji ambaye hutengeneza na kuanzisha chapa na kuwainua vijana ili kujipatia kipato hivyo BRELA hawezi kupakwepa kwa kuwa yeye ni mfanyabiashara. Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa (Kulia), akimkabishi nyaraka nyota wa muziki nchini na mkurugenzi wa Wasafi Media, Diamond Platnums, wakati alipotembelea ofisi za BRELA makao makuu Machi 7, 2024.  “Nilipokutana  na Nyaisa naye kujitambulisha kwangu alinieleza kwamba BRELA panafaa kuwa  nyumbani kwangu kwa...

Dk.Kijaji awaita BRELA wanawake wajasiriamali

Picha
Mwandishi Wetu, daimanewstz@gmail.com Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji amewataka wajasiriamali wanawake wanaoendesha biashara zao sokoni kurasimisha biashara zao na kuzisajili kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Amesema hilo litaziongezea thamani na kulinda bunifu zao na kuwawezesha kunufaika nazo kiuchumi. Dk. Kijaji ametoa rai hiyo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, leo Machi 7, 2024 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 8 kila mwaka. Hafla hiyo iliandaliwa na Wanawake wa Masokoni wa Mkoa wa Dar es Salaam (WOMEN TAPO) katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Afisa Mtendaji Mkuu huyo wa BRELA amewataka wanawake wajasiriamali hao kuacha kuendesha biashara  kienyeji, huku akiwaeleza faida watakazopata kwa kusajili biashara na vumbuzi zao. “Niwahakikishie kuwa BRELA inazipa ulinzi wa kisheria biashara na bunifu iwapo mtu yeyote ataiga kazi yako, kwa wewe mwan...

Utafiti: Akili bandia hubashiri kifo kwa usahihi

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Utafiti mpya wa kisayansi ubebaini kuwa mfumo wa akili bandia (AI), una uwezo mkubwa wa kubashiri kifo cha binadamu kwa usahihi pamoja na kubainisha hatari za kutokea vifo vya mapema. Mfumo huo wa akili bandia uliowezeshwa na historia za mamilioni ya watu na takwimu, una kiwango kikubwa cha usahihi katika kutabiri maisha na uwezekano wa vifo kutokea kuliko mifumo yote iliyopo sasa. Wanasayansi kutoka Technical University of Denmark (DTU), wamebainisha. Jarida la Computational Science Katika utafiti wao, wanasayansi hao walitumia takwimu za soko la ajira na afya zaidi ya milioni sita zilizokusanywa kati ya mwaka 2008 na 2020, zilizojumuisha taarifa za mtu mmoja mmoja, elimu, alivyokwenda kutibiwa hospitali na matokeo ya vipimo, kipato na shughuli wanazofanya. Wanasayansi hao walibadili takwimu hizo kuwa katika maneno ili kufundisha lugha ya kisayansi iitwayo “life2vec” inayoelezwa ni sawa na mifumo ya teknolojia ya akili bandia   kama ule...

BRELA yazipa makali taasisi za kuchunguza uhalifu

Picha
-Ni kuhusu kuzuia uhalifu umiliki manufaa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imetoa mafunzo ya kutambua wamiliki manufaa wa kampuni na Majina ya Biashara kwa taasisi za uchunguzi. Kwa mujibu wa BRELA lengo la mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Arusha Februari 25, 2924 ni kurahisha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo kuzuia na kupambana na uhalifu wa kifedha.  Kaimu Mkurugenzi wa Makampuni na Majina ya Biashara wa BRELA, Isdori Nkindi akitoa mafunzo kwa Taasisi za Uchunguzi juu ya namna ya kutambua mmiliki manufaa wa Kampuni na Majina ya Biashara, jijini Arusha Februari 24,2024. Kaimu Mkurugenzi wa Makampuni na Majina ya Biashara BRELA, Isdor Nkindi ameeleza hayo akibainisha kuwa, Wakala yake imekasimiwa na Serikali pendekezo namba 24 kati ya mapendekezo 40 ya Kikosikazi cha Kushughulika na Makosa ya Uhalifu wa Kifedha Ulimwenguni (FATIF), linalohimiza uwazi katika makampuni, hivyo ni jukumu lao kuzijengea uwezo taasisi hizo za ...

Mawakili watakiwa kuwaibua wahalifu wa fedha

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mawakili na Wafanyabiashara nchini, wametakiwa kuwaibua wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya uhalifu wa kifedha kwa kuwa vinakwamisha maendeleo ya Taifa. Rai hiyo imetolewa leo Machi mosi mjini Arusha na Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa huo anayesimamia  Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Frank Mmbando aliyezungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, wakati akifungua kikao kazi kati ya BRELA na Wadau Jijini Arusha.  Washiriki wa kikao kazi kuhusu Dhana ya Wamiliki Manufaa  iliyotolewa na BRELA kwa wadau wakiwemo Mawakili na Wafanyabiashara Jijini Arusha, wakifuatilia mafunzo hayo mapema Februari 27,2024. “Serikali inatambua kuwepo kwa changamoto za taarifa za baadhi ya wamiliki wa kampuni wanaoweza kutumia kampuni zao kukwepa kodi, kupitisha fedha haramu, kujihusisha na ufadhili wa vitendo vya ugaidi na ndio maana BRELA ilikutana na wawakilishi wa Taasisi za Uchunguzi na Mamlaka za Udhibiti ili kushauriana jinsi ya kukabiliana ...