-Takwimu zawataja kujamiiana zaidi
Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com
Karibu nusu ya wanaume Tanzania, wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 49, walifanya mapenzi na mwanamke zaidi ya mmoja ndani ya miezi 12, wakati asilimia nne pekee ya wanawake wenye umri kama huo, walifanya mapenzi na wanaume tofauti kwa kipindi hicho.
Matokeo ya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 inayopatikana Ofisi ya Taifa ya Takwimu, yamebainisha hayo yakieleza kwamba, asilimia 21 ya wanawake walijamiiana na watu ambao ama walikuwa w waume zao au waliishi nao.
Kuhusu kupima Virusi vya Ukimwi (HIV), matokeo ya utafiti huo yamebainisha kwama wanawake wanane kati ya kumi wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 49 hawajawahi kupima wala kupokea matokeo ya vipimo hivyo.
“Kwa upande wa wanaume asilimia 64 hawajawahi kupima wala kupokea matokeo ya vipimo hivyo katika miezi 12 iliyopita,” inawka wazi ripoti hiyo.
Matokeo hayo yanaonyesha katika kipindi hicho asilimia 37 ya wanawake na asilimia 31 ya wanaume walipima HIV na kupokea matokeo yao mara ya mwisho walipopima.
Hata
hivyo, ni wanawake wachache sawa na asilimia 18 ndio wamesikia kuhusu uwepo wa
vifaa vya upimaji binafsi HIV, huku asilimia 31 ya wakiwa wanaume, ambapo
asilimia tatu ya wanawake na tano ya wanaume wametumia vipimo hivyo.
0 Maoni