Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Utafiti: Akili bandia hubashiri kifo kwa usahihi

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Utafiti mpya wa kisayansi ubebaini kuwa mfumo wa akili bandia (AI), una uwezo mkubwa wa kubashiri kifo cha binadamu kwa usahihi pamoja na kubainisha hatari za kutokea vifo vya mapema.

Mfumo huo wa akili bandia uliowezeshwa na historia za mamilioni ya watu na takwimu, una kiwango kikubwa cha usahihi katika kutabiri maisha na uwezekano wa vifo kutokea kuliko mifumo yote iliyopo sasa. Wanasayansi kutoka Technical University of Denmark (DTU), wamebainisha.

Jarida la Computational Science

Katika utafiti wao, wanasayansi hao walitumia takwimu za soko la ajira na afya zaidi ya milioni sita zilizokusanywa kati ya mwaka 2008 na 2020, zilizojumuisha taarifa za mtu mmoja mmoja, elimu, alivyokwenda kutibiwa hospitali na matokeo ya vipimo, kipato na shughuli wanazofanya.

Wanasayansi hao walibadili takwimu hizo kuwa katika maneno ili kufundisha lugha ya kisayansi iitwayo “life2vec” inayoelezwa ni sawa na mifumo ya teknolojia ya akili bandia  kama ule wa ChatGPT.

Kwa mujibu wa utafiti huo uliochapichwa katika Jarida la Nature Computational Science hivi karibuni,  mara akili bandia inapofundishwa na kuelewa takwimu hizo, huzalisha mfumo bora zaidi unaoweza kuchambua kuhusu mtu binafsi  na kutoa majibu yenye usahihi kwa kiwango kikubwa cha usahihi kuonyesha muda atakaokufa.

Watafiti hao walichukua takwimu kutoka kikundi cha watu weny umri wa miaka 35 hadi 65 na nusu kati ya hao tayari wamefariki kati ya mwaka 2016 na 2020, ambapo akili bandia iliulizwa kati ya hao yupi aliye hai na aliyefariki. 

Majibu ya mfumo huo wa akili bandia ulitoa majibu sahihi kwa asilimia 11 zaidi ya mifumo iliyopo sasa hata mifumo inayotumika  na kampuni za bima kupanga bei na miongozo ya sera. 

“ Jambo muhimu la kushangaza hapa ni maisha ya watu kama mfululizo wa matukio, sawa na sentesi inavyoundwa na maneno yanayofuatana,” amesema mtafiti Sune Lehman wa chuo kikuu DTU na kuongeza:

Mtafiti, Sune Lehmann
“ Kwa kawaida hii ni kazi ambayo mtendaji huitumia katika akili bandia, lakini katika mjaribio yetu, huwatumia kuchambua kitu tunachoita mpangilio wa matukio yanayotokea katika maisha ya watu.”

Hata hivyo, wanasayansi hao wameonya kuwa mfumo huo haufai kutumika katika bima za afya kwa mujibu wa taratibu za kimaadili.

Chapisha Maoni

0 Maoni