Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Rais Samia aigusa CCM

 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi akikigusa Chama Cha Mapinduzi(CCM), kwa kumteua Naibu Katibu Mkuu wake, Anamringi Macha, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Kwa hatua hiyo, kuna uwezekano kwa CCM kumteua na kumpitisha mtu mwingine kushika nafasi ya unaibu katibu mkuu, badala ya Anamringi.

Anamringi anachukua nafasi ya Christina Mndema, ambaye ameteuliwa na Rais kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus leo Machi 12,2024, imeeleza kuwa mbali na uteuzi wa wawili hao, Rais Samia pia amefanya uteuzi na uhamisho wa watendaji mbalimbali, wakiwamo wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji wa halmashauri na makatibu tawala wa wilaya.

Taarifa hiyo ya Ikulu, imeeleza kuwa uapisho wa wakuu wa mikoa na naibu katibu mkuu, utafanyika kesho saa 4 asubuhi Ikulu Dar es Salaam.

Habari zaidi soma orodha ya watbyeule na nafasi zao katika kiambatanisho



Chapisha Maoni

0 Maoni