Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2025

Tanzania, Canada kushirikiana kuendeleza sekta ya madini

Picha
▪️Balozi wa Canada apongeza mageuzi madini ▪️Wachimbaji wadogo kujengewa uwezo   Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Waziri wa Madini Anthony Mavunde na Balozi wa Canada nchini Tanzania Emily Burns lwamekutana jijini Dodoma na kufanya kikao kuhusu maendeleo ya sekta ya madini nchini. Waziri wa Madini Anthony Mavunde (Kushoto) na Balozi wa Canada nchini Tanzania Emily Burns walipokutana jijini Dodoma na kufanya kikao kuhusu maendeleo ya sekta ya madini nchini. Balozi Emily Burns pia ametumia kikao hicho kujitambulisha, amesema Canada ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika kuwaendeleza wachimbaji wadogo nchini kwa kuwajengeza uwezo katika uchimbaji wa matumizi sahihi ya teknolojia, utakaozingatia utunzaji wa mazingira na kuwajengea ujuzi, ili kuongeza tija kwenye uzalishaji madini. Balozi Burns ameonesha utayari wa Serikali ya Canada kutoa mafunzo maalum (Tailor-made training) kwa wakinamama na vijana kupitia vyuo vya Ufundi-VETA katika maeneo ambayo uzalishaji madini unafanyika...

Serikali yatunga kanuni kuzuia wageni kuingia kiholela leseni ndogo za uchimbaji

Picha
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde akisoma hotuba  ya bajeti ya wizara yake bungeni mjini Dodoma.   Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Serikali kupitia Wizara ya Madini imetunga kanuni za msaada wa kiufundi katika Leseni ndogo za uchimbaji wa Madini ambazo zitaratibu ushiriki wa wageni katika Leseni ndogo za uchimbaji wa Madini(PML) ambazo kwa mujibu wa kifungu cha 8 cha Sheria ya Madini sura ya 123,kimezitamka Leseni hizi kama maalum kwa ajili ya Watanzania. Kifungu cha 8(3) cha Sheria ya Madini kinatoa ruhusa kwa mmiliki wa Leseni ndogo ya uchimbaji madini kuingia ubia na mgeni kwa makubaliano ya msaada wa kiufundi (𝙏𝙚𝙘𝙝𝙣𝙞𝙘𝙖𝙡 𝙎𝙪𝙥𝙥𝙤𝙧𝙩). Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka 2024/25 Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema Serikali inatarajia kutunga kanuni za kuratibu ushiriki wa wageni katika Leseni ndogo kwa kuwa kumejitokea wimbi kubwa la wageni kuingia katika maeneo ya wachimbaji wadogo kwa mgongo wa “Msaada wa Kiufundi”ambao hauku...

NHC na Sera ya Ubia: Kariakoo inavyong’arishwa ikibeba sura ya kimataifa

Picha
- Majengo mapya yaota kama uyoga - Wazawa wawekeza  - Kitabu cha zama mpya kinaandiwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Kila zama ina kitabu chake; hayo si maneno yangu, bali ni msemo wa lugha adhimu ya Kiswahili, linaloweza kutafsiriwa kwamba, kila jambo lina historia yake. Ndivyo ilivyo kwenye maisha ya binadamu anapotekeleza mipango na malengo yake binafsi au ya jamii inayomzunguka, ili kupata manufaa au tija tarajiwa. Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kwa namna ya pekee katika historia yake liliingia katika zama za ubia Novemba 16, 2022, kwa kumwalika Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), aliyeizindua sera yake ya ubia iliyoboreshwa, ikilenga kufungua milango kwa wawekezaji binafsi kushirikiana na shirika hilo kuendeleza maeneo ya mijini kwa kujenga makazi bora na ya kisasa ya watu, pia majengo ya biashara. Hata hivyo, Sera ya Ubia si mpya sana kwa NHC kwani kati ya mwaka 1993 hadi 2010, shirika hilo lilitekeleza mirai 194 likishirikiana na wawekezaji binafsi. Lakini,...

DCEA yakamata kilo 4500 za dawa za kulevya

Picha
- Yazuia tani 14 za kemikali hatari kuingia nchini, ingeweza kuua watu bilioni 4    -  Yateketeza ekari 178 za mashamba ya bangi  Hussein Ndubikile,daimatznews@gmail.com Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya dola nchini, imekamata kilogramu 4,568 za dawa za kulevya,  magari saba, pikipiki tano na bajaji moja kwa kuhusika katika shughuli za usafirishaji wa dawa hizo  pamoja na kuteketeza ekari 178 za mashamba ya bangi. Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo akizungumza na wanahabari Dar es Salaam Aprili 25, 2025. Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo amebainisha hayo alipozungumza na wanahabari Dar es Salaam Aprili 25, 2025, ambapo ameeleza kuwa walifanya ukamataji huo baada ya kufanya oparesheni kubwa katika mikoa kadhaa ya Tanzania ambapo wamefanikisha kukamatwa kwa kiasi hicho kikubwa cha dawa za kulevya, kemikali bashirifu, magari na watuhumiwa waliokuwa wakijihusisha na biashara hiyo ha...

Dk. Mpango: Wekezeni kwenye utalii wa vyakula

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito kwa wadau wa utalii wa vyakula kuwekeza zaidi katika kuandika vitabu vya vyakula vya kiafrika na machapisho ya kuandaa mapishi, ili kuongeza ujuzi na kupunguza woga kwa watalii wa matumizi ya vyakula wasivyovifahamu. Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango akisalimiana na Mwanzilishi wa Tamasha la Utalii wa Vyakula Zimbabwe, Dk. Auxilia Mnangagwa baada ya kufungua Mkutano wa wa Pili wa Umoja wa Mataifa wa Utalii wa Vyakula Barani Afrika unaofanyika jijini Arusha. Dk. Auxilia ni Mke wa Rais wa Zimbambwe.   Dk. Mpango ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano wa Pili wa Umoja wa Mataifa wa Utalii wa Vyakula Barani Afrika, unaofanyika jijini Arusha, ambapo amesema ni muhimu kutangaza vyakula vya kitamaduni vya Afrika kwa kiwango kikubwa, ili utalii wa vyakula hivyo uweze kukua na kustawi.  “Kwa sasa watalii wengi hawana ufahamu wa utajiri wa vyakula vya kitamaduni vilivyopo barani Afrika, vilevile nd...

Ripoti CAG: Serikali imepata hasara ya Dola milioni 147 kampuni za madini

Picha
-Wakala ununuzi mafuta yakwama uratibu wa bei Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu  za Serikali (CAG), imebainisha kuwa Serikali imepata hasara ya Dola za Marekani milioni 147 sawa  na takriban shilingi bilioni 395.14, zilizolipwa kama fidia kwa kampuni za uchimbaji madini, huku Wakala wa Ununuzi wa Mafuta ukiripotiwa haujatekeleza uratibu wa bei ya mafuta kwa Kampuni za Uuzaji wa Mafuta, hivyo kuweza kuathiri bei za mafuta nchini. Mdhibiti na Mkaguzi wa Fedha za Serikali (CAG), Charles Kichere akizungumza katika moja ya mikutano yake na vyombo vya habari. Kwa mujibu wa  Ripoti Kuu ya Mwaka ya Ukaguzi wa Serikali Kuu kwa Mwaka wa Fedha 2023/24 iliyowasilishwa bungeni wiki hii, Serikali imepata hasara hiyo kutokana na fedha hizo kulipwa fidia kwa kampuni za uchimbaji madini zilizoathiriwa na matumizi ya marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010. Kabla ya kuwasilishwa bungeni, CAG aliwasilisha ripoti hiyo kwa Rais Dk.SamiaSuluhu ...

Waziri Aweso: Ongezeni nguvu tafiti Dodoma wapate maji salama

Picha
-Aagiza kuongezwa mitambo zaidi ya uchimbaji visima Dodoma -Akagua miradi ya maji Nala na Nkuhungu ▪️Miradi ya visima vinavyochimbwa kuzalisha maji lita 32m Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amewataka wataalamu wa wizara hiyo kuhakikisha wanaongeza nguvu na kufanya utafiti wa kina wa maji katika Jiji la Dodoma ili kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Jiji la Dodoma. Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akipanda katika moja ya matenki ya kuhifadhia maji jijini Dodoma, kufanya ukaguzi katika ziara yake Nara jijini Dooma leo.   Waziri Aweso ameyasema hayo leo, wakati akikagua miradi ya maji wa Nala unaogharimu Tsh 3.8 bilioni na Uchimbaji wa Visima katika Kata ya Nkuhungu na maeneo mengine ya jiji hilo katika mradi unatoekelezwa ukiwa  na thamani ya Tsh 41 bilioni. “Ni maelekezo ya Mh. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha tunatatua changamoto ya maji jijini Dodoma.Ndio maana zimetolewa fedha zaidi ya Tsh 45 bilioni kwa ajili ...

Rais Samia mgeni rasmi tuzo za waandishi wa habari

Picha
Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya utoaji tuzo za waandishi wa habari zinazofahamika kwa jina la "Samia Kalamu Awards", itakayofanyika Aprili 29, mwaka huu jijini Dodoma. Mkurugenzi wa TAMWA,Dk.Rose Reuben (Katikati),akizungumza nawanahabariDar es Salaam.Wengine pichani ni wajumbe wa kamati ya tuzo za wanahabari za kuandika habari za maeneleo.  Hayo yamesmwa leo Aprili 15, 2025 jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Dk. Rose Reuben alipozungumza na waandishi wa habari. Tuzo hizo ambazo zimeandaliwa na TAMWA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni Tuzo Maalum za Kutambua  Mchango wao katika kuandika Habari za Maendeleo. Dk. Reuben amesema tuzo hizo zinatolewa kwa mara ya kwanza kwa lengo la kuhamasisha na kuthamini kazi za waandishi wanaojikita katika uandishi unaoleta uele...

Rais Samia aituliza Dodoma tatizo la maji

Picha
-Awapa Sh 445 bilioni kutekeleza mradi -Lita 20 mil kuzlishwa kwa siku -Maji yamweka Waziri Awesoi Dodoma  -Mbunge Mavunde apongeza  Serikali  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com   Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema Rais Dk Samia Suluhu Hassan ameelekeza utekelezaji wa miradi ya maji wenye thamani ya Shlingi Bilioni 445 jijini Dodoma ili kutatua changamoto ya maji jij ini humo. Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akizungumza wakati wa utiaji saini mkataba wa mradi wa maji jijini Dodoma. Aweso ameeleza kuwa Rais Samia ametoa maagizo hayo wakati Jiji la Dodoma likisubiri utekelezaji wa miradi ya kuleta maji kupitia Ziwa Victoria na mradi wa Bwawa la Farkwa. Ameyasema hayo leo Aprili 15, 2025 wakati akishuhudia utiaji wa saini wa Mkataba wa Mradi wa Kusambaza Maji kupitia visima vya maji vya Nzuguni A, wenye thamani ya Shilingi Bilioni 5, unaotarajiwa kuwanufaisha wananchi 123,095. “Mbunge wenu alileta maombi kwa Mh. Rais Samia juu ya uchimbwaji wa visima virefu wakati wa mk...

NLD wapitisha wagombea watakaochuana na Rais Samia, Dk. Mwinyi Uchaguzi Mkuu 2025

Picha
Ni H assan Doyo na Mfaume Khamis Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Chama cha National League for Democracy (NLD) kimetangaza majina ya wagombea urais watakaochuana na wangombea wa chama tawala CCM, katika Uchaguzi Mkuu ujao Oktoba mwaka huu 2025 kikieleza wamefikia hatua hiyo baada ya mchakato wa ndani wa chama hicho kukamilika kwa mafanikio. Katika mchakato huo NLD kimempitisha Doyo Hassan Doyo kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho  huku  Mfaume Khamis akiteuliwa kuwa Mgombea Urais wa Zanzibar. Tayari CCM kimewapitisha Rais Samia Suluhu Hassan kuwania kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  na Dk.Hussein Mwinyi kuwania kiti cha urais visiwani Zanzibar,hivyo sasa watachuana na Doyo na Mfaume Khamis katika  kinyang'anyiro hicho,.  "Uamuzi huo umetokana na vikao halali vya chama, kufuata taratibu zote za kikatiba na mapendekezo ya wajumbe wa Mkutano Mkuu kutoka sehemu mbalimbali kote nchini," imesema  N...

Waziri Mazrui azindua Zanzibar Afya Week 2025

Picha
-Linalenga  kuhamasisha utalii wa afya na kukuza sekta ya afya Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Mazrui amezindua Zanzibar Afya "Week" 2025 Zanzibar Afya Week 2025 itakayofanyika Unguja na Pemba na kubainisha kuwa ni fursa adhimu ya kuimarisha mfumo wa afya, kukuza ubunifu katika sekta ya tiba, na kuhamasisha Utalii wa Afya Visiwani Zanzibar. Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Mazrui Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo Aprili 12, 2025, Waziri Mazrui amewapongeza wadau wote wa sekta ya afya na washirika wa maendeleo wanaoshirikiana nasi kuhakikisha mafanikio ya Zanzibar Afya Week 2025. "Waheshimiwa viongozi na wageni waalikwa, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua kwamba afya bora ni msingi wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Zanzibar Afya Week 2025 inahusiana moja kwa moja na vipaumbele vya Serikali vilivyobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 pamoja na Mpango wa Mkakati wa Afya wa Z...

Askofu ashangazwa jamii kushabikia ‘Ubaya Ubwela’

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com SAME.  Askofu wa Jimbo Katoliki Same, Mhashamu Rogath Kimaryo CSSP, ameshangazwa na tabia ya watu kushabikia neno ubaya ubwela, akilielezea kuwa linayoonesha watu wanafurahia ubaya zaidi kuliko wema. Mhashamu Rogath Kimaryo (CSSP) Akitoa mahubiri yake katika adhimisho la Sadaka ya Misa Takatifu ya Dominika ya Matawi katika Kanisa Kuu la Kristo Mchungaji Mwema jimboni Same, Askofu Kimario amesema Bwana Yesu Kristo alikuwa mwema, alifanya mambo mengi mema na kutoa mafundisho mazuri, lakini yote hayo hayakuonekana na kuishia kuhukumiwa kifo. “Hiyo yote ilitokana na watu kushabikia ubaya. Yeyote anayeshabikia ubaya, lazima utakuja kumrudia,” amesema Askofu.\ Amefafanua kuwa mahali pa kazi, tabia ya ubaya ubwela ndio husababisha watu kushindwa kufuata maadili ya kazi zao na kusababisha kupeana tuhuma mbaya zikiwamo za ugaidi. "Ninayasema haya nikiwa na ushahidi kwamba yametokea. Mtu anapewa tuhuma za ugadi, baada ya muda anatolewa kwamba kesi imefu...

Dk.Nchimbi amuomba kura Lissu, Chadema

Picha
-Ni iwapo watagomea uchaguzi -Asema ni haki yao kutogombea  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Emmanuel Nchimbi, (Pichani) amekishauri Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutopoteza haki zao zote za kushiriki katika uchaguzi mkuu, Oktoba mwaka huu ambayo ni ya kikatiba kwa kupiga kura au kuchaguliwa, badala yake chama hicho kutumia walau haki moja ya kupiga kura kwa kuipigia kura CCM. Dk. Nchimbi ametoa kauli hjiyo katika hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu Maalum wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Aprili 4 na 5 Songea Mkoani Ruvuma, ambapo alikuwa mgeni rasmi. “Angalau katika hizo haki mbili ndugu yangu Tundu Lissu hakikisha unaipata mojawapo. Ukishindwa kuchaguliwa basi chagua. Unakuwa umetutendekea haki na ninaamini rafiki yangu Tundu Lissu na wenzake haki ya kuchagua wataitumia vizuri. Naminaomba kura zenu,” amesema Dk. Nchimbi na kufafanua: “Kugombea na kutogombea vyote ni sawa ni haki yao kikatiba; ......