Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2023

IKULU UTEUZI

Picha

Dk Mwinyi, Othman Masoud watia ubani Maulid Z'bar

Picha
Viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,(Pichani chini), wameshiriki katika Hafla ya Maulid Matukufu ya Kuadhimisha Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW), Viwanja vya Maisara, Mkoa wa Mjini-Magharib, Unguja iliyofanyika Septemba 27, 2023. Viongozi hao Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi(kushoto), Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Othman Masoud Othman (kulia) na Makamu wa Pili wa Rais visiwani humo, Hemed Suleiman Abdulla, wameonyesha mshikamano kwa kushiriki tukio hilo muhimu katika imani ya dini ya Kiislam wakijumuika pamoja na Masheikh, Ulamaa, Walimu, Wanavyuoni Mashuhuri na Waumini wa Kiislamu kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Visiwa vya Unguja na Pemba vinavyounda Zanzibar. Hafla hiyo ya kitaifa pia ilihudhuriwa na baadhi ya Mabalozi na Wanadiplomasia wanaowakilisha nchi Tanzania, viongozi wa taasisi na madhehebu tofauti ya kidini, wageni kutoka mataifa mbalimbali, sanjari na walimu na wanafunzi wa madrasa. Hafla hiyo ambayo hufanyika kila ifika...

Namba zinaipaisha MSD

Picha
-Mapato yaongezeka, ufanisi wapaa   Exuperius Kachenje, daimatznews@gmail.com Namba zinaipaisha Bohari ya Dawa nchini (MSD), ndivyo unavyoweza kueleza, baada taasisi hiyo kupata mafanikio makubwa katika utendaji wake kwa mwaka 2023. MSD imetangaza ongezeko la shilingi bilioni 52 katika mapato yake, sanjari na upatikanaji dawa kuongezeka kutoka asilimia 57 kwa mwaka 2022 hadi asilimia 81 kufikia Juni mwaka 2023   Taasisi hiyo ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya, iliyoanzishwa mwaka 1993, pia imetangaza kuongezeka kwa u patikanaji wa bidhaa za afya kutoka asilimia 51, Juni 2022 hadi kufikia asilimia 64 Juni 2023. Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari leo jijiniDar es Salaam, chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai amebainisha hayo akitaja majukumu na muundo wa bohari hiyo, pia kubainisha ongezeko la mapato yake kwa usambazaji kufikia shilingi bilioni 372.4 mwaka huu kutoka shilingi bilioni 320.9 mwaka 2022. Mk...
Picha
 Makamu wa Rais ahutubia UN  Mwandishi Wetu, DAIMATANZANIA Makamu wa Rais Dk Philip Mpango, ameshiriki na kuhutubia mkutano wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaondelea katika Jiji la New York nchini Marekani, akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan. Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango anaongoza ujumbe wa Tanzania ambapo awali Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa ulijadili kuhusu Malengo Endelevu 17 ya Dunia (SDGs), unaotarajiwa kufanyika Septemba 18 na 19, huku Tanzania ikitajwa kufanya vizuri. Mkutano huo, umefanyika huku ripoti ya tathmini ya pili ya hiari iliyofanywa na Umoja wa Mataifa (UN) kati ya mwaka 2019 hadi Juni mwaka 2023, kuhusu utekelezaji malengo hayo kufikia mwaka 2030 (VNR) ikionyesha kuwa Tanzania imefanya vizuri katika maeneo sita. Akiwasilisha mada katika kikao kazi na Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF), kwenye Ofisi za Shirika la Mpango wa Maendeleo Duniani (UNDP) leo jijini Dar es Salaam, ...