TAMICO YAPENDEKEZA MABORESHO HALI ZA WAFANYAKAZI NHC
-Mkurugenzi Mkuu NHC ajibu unafanyiwa kazi ndani ya miezi 6
-Ataka
TAMICO ichukue ya NHC kama mfano bora
Chama cha Wafanyakazi wa Migodi, Nishati na Ujenzi (TAMICO), kimependekeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuufanyia maboresho Mkataba wa Hali Bora kwa Wafanyakazi wa shirika hilo uliopo kwa maslahi ya watumishi hao, huku Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah ikiahidi kufanyia kazi ndani ya miezi sita.
![]() |
| Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa shirika hilo leo, Februari 11, 2026 jijini Arusha |
Ushauri huo umetolewa na Katibu Mkuu wa TAMICO Taifa, Partenus Rwechungura, alipokuwa akitoa salam za chama hicho cha wafanyakazi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC kwa mwaka 2026, unaofanyika jijini Arusha.
Hata hivyo, katika hotuba yake ya kumkaribisha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Leonard Akwilapo aliyekuwa mgeni rasmi kufungua mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa shirika hilo alijibu;
![]() |
| Baadhi ya wafanyakazi wa NHC wakifuatilia Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa shirika hilo unaoendelea jijini Arusha. |
“Mkataba
wa hali bora hatujaukalia, tutaufanyia kazi ndani ya miezi sita kwa makubaliano
na TAMICO tawi la NHC, nilishakutana nao Februari 3, 2026. Ninaomba TAMICO
mchukue NHC kama darasa kwenye eneo hilo.”
Hamad alimpongeza Rwechungura kwa kuendelea kusimama kidete kutetea maslahi ya wafanyakazi na kuhimiza mazungumzo yenye tija kati ya menejimenti na watumishi wa NHC, huku Rwechungura akipongeza hatua ya Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa NHC, kutoa muda wa miezi sita kwa ajili ya maboresho ya mkataba huo akieleza ni hatua ya msingi na inaonesha utayari wa pande zote kujenga makubaliano yenye manufaa ya pamoja.



Maoni
Chapisha Maoni