NHC YAELEKEZWA KUWEKEZA AFCON

 Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo(pichani), amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuwekeza jijini Arusha katika eneo la viwanja vitakavyotumika kwa Mashindano ya Kombe la Afrika(AFCON), mashindano yatakayofanyika mwakani 2027. 

Mashindano hayo yatajumuisha uenyeji wan chi tatu ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda, ambapo Dk. Akwilapo amesema Serikali imeelekeza kila Wizara na taasisi za umma zifanye jambo kuwezesha ACON kuwa bora zaidi, ikiwezekana kuliko iliyofanyika Morocco na kumalizika mwaka huu 2026. 

“Wizara ya Ardhi imepima maeneo kwenye eneo la AFCON, NHC iangalie namna ya kushiriki kwa kujenga na kuwekeza,”amesema Dk. Akwilapo na kuongeza:

“Mimi napenda mambo ya  ‘Here and now’, (Hapa tulipo na sasa), natarajia NHC itafanya jambo kuwa na majengo yatakayofanikisha AFCON.” 

Awali, akimkaribisha Waziri Dk. Akwilapo kuzungumza, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, alisema yupo NHC ipo tayari kusikiliza na kupokea maelekezo ya Serikali.

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi