Waziri Mkuu aagiza Kanisa la Ufufuo na Uzima
-Ataka liwekwe chini ya uangalizi kwa miezi sita
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, amemwagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kulifungulia Kanisa la Ufufuo na Uzima, lakini akataka liwekwe chini ya uangalizi kwa miezi sita.
Waziri Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba
" Kama kutatokea kiongozi amekosa, sasa atashughulikiwa yeye badala ya taasisi yake, maana imani ni kati ya mtu na Mungu wake sio askofu," amesema Mwigulu.
Kanisa hilo ambalo kiongozi wake ni Askofu Josephat Gwajima, lilifungiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani, ikielezwa kwamba kiongozi wake alikiuka masharti ya usajili wake kwa mujibu wa sheria.
Maoni
Chapisha Maoni