Rais Dk.Samia aapisha mawaziri, awaonya

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaapisha Mawaziri na Manaibu Waziri aliowateua jana, hafla iliyofanyika leo Novemba 18, 2025, Ikulu Chamwino jijini Dodoma akiwataka kwenda kuwajibika na kuonya haoni tabu kubadili mawaziri.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Profesa Rikizi Shemdoe akiapa mbele ya Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo Novemba 18, 2025.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia amesema mawaziri na manaibu wao hao wamekabidhiwa majukumu ya kuwatumikia wananchi, akiwataka kutanguliza utu na uwajibikaji miongoni mwao na mbele ya wananchi.

‎‎”Kazi ya kuanzia sasa ni kuendelea kuwajibika kwa Taifa, viongozi wazito punguzeni uzito ili kwenda sambamba na kasi ya utekelezaji kwa kuwa muda ni mchache,” amesema.

‎Kwa mujibu wa Rais Samia, Serikali ya Awamu ya Sita anayoiongoza imepanga kuanza kutekeleza miradi kwa kutumia fedha za ndani na mashirika ya maendeleo yawakute  wameshaanza utekelezaji, hatua inayolenga kuepusha ucheleweshaji wa miradi kutokana na masharti ya washirika.

‎Amesema utekelezaji wa miradi ni jukumu la viongozi wote na si jukumu la Rais pekee na kwamba miradi yote inapaswa kutoa matokeo chanya kwa kuwafikia wananchi na si kubaki ofisini kwake.

‎‎Pichani chini;

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Mawaziri wa Wizara mbalimbali aliowateua jana. Hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo Jumanne 18 Novemba, 2025.





 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi