Baraza la Mawaziri hili hapa
- Dk.Biteko, Jenister, Jafo,Bashe waachwa
-Prof. Shemdoe, Makonda, Nanauka wang'ara
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Imemchukua takriban dakika nane, Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza Baraza lake jipya la Mawaziri uteuzi alioufanya kwa mujibu wa Ibara ya 50 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku sura mpya za vijana zikichomoza na mawaziri waliokuwa maarufu katika baraza lililopita wakiwekwa kando.
![]() |
| Rais Dk. Samia Suluhu Hassan |
Baadhi ya sura mpya za vijana zilizoibuka na kung'ara ni Joel Nanauka aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Vijana, Prof. Riziki Shemdoe(Waziri wa TAMISEMI), Paul Makonda aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Utamaduni na Michezo na Wanu Hafidh Ameir (Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia)
Baadhi ya walioachwa ni aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dotto Biteko, Jenister Mhagama (Wazira wa Afya), Pindi Chana aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Hussein Bashe aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Stergomena Tax aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambaye hata hivyo hakugombea ubunge.
Hata hivyo, mkongwe William Lukuvi, amerejea ulingoni baada ya kuteuliwa kuwa Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, huku Prof. Palamagamba Kabudi akirejea katika nafasi ya uwaziri kwenye Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Angela Kairuki akiwa Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Akizungumza na wanahabari, Ikulu ya Chamwino Dodoma, leo Jumatatu Novemba 17, 2027 Rais Samia amesema; " Juzi nilipozungumza na Bunge, nilisema sitachukua muda mrefu, nitaunda Baraza la Mawaziri."
"Ujio wangu hapa ni kuwataja wale watakaotusaidia kwenye kazi hizo za Mawaziri na Manibu Mawaziri. Lakini niseme kwa ujumla niseme tu, tumeona umuhimu wa vijana kuwa na wizara kamili ambayo itasimama nao.Wizara hii itakuwa chini ya Ofisi ya Rais," amesema Rais Samia.
𝐁𝐚𝐫𝐚𝐳𝐚 𝐥𝐚 𝐌𝐚𝐰𝐚𝐳𝐢𝐫𝐢 𝐥𝐢𝐥𝐢𝐥𝐨𝐭𝐚𝐧𝐠𝐚𝐳𝐰𝐚 𝐧𝐚 𝐑𝐚𝐢𝐬 𝐒𝐚𝐦𝐢𝐚 𝐒𝐮𝐥𝐮𝐡𝐮 𝐇𝐚𝐬𝐬𝐚𝐧 ni hili hapa chini;
I. Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora
a) Waziri:
Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete
b) Naibu
Waziri: Mhe. Regina Ndege Qwaray
2. Ofisi
ya Rais — Mipango na Uwekezaji
a)
Waziri: Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo
b)
Naibu Waziri: Mhe. Pius Stephen Chaya
3. Ofisi
ya Rais - Maendeleo ya Vijana
a)
Waziri: Mhe. Joel Arthur Nanauka
4. Ofisi
ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira
a)
Waziri: Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni
b)
Naibu Waziri: Mhe. Dkt. Festo John Dugange
5. Ofisi
ya Waziri Mkuu — Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu
a)
Waziri: Mhe. William Vangimembe Lukuvi
b)
Ummy Hamisi Nderiananga
1
6. Offsi
ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano
a) Waziri:
Mhe. Deus Clement Sangu
b) Naibu
Waziri: Mhe. Rahma Riadh Kisuo
7. Ofisi
ya Waziri Mkuu — Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
a) Waziri: Mhe. Prof. Riziki Silas
Shemdoe
b) Naibu
Waziri (Elimu): Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa
c) Naibu Waziri (Afya): Dkt. Jafar Rajab
Seif
8. Wizara
ya Fedha
a) Waziri:
Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar
b) Naibu
Waziri: Mhe. Laurent Deogratius Luswetula
c) Naibu Waziri: Mhe. Mshamu Ali Munde
9. Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
a) Waziri:
Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo
b) Naibu
Waziri: Mhe. Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe
c) Naibu
Waziri: Mhe. James Kinyasi Millya
10. Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi
a) Waziri:
Mhe. Boniface George Simbachawene
b) Naibu
Waziri: Mhe. Denis Lazaro Londo
ll. Wizara ya Kilimo
a) Waziri:
Mhe. Daniel Godfrey Chongolo
b) Naibu
Waziri: Mhe. David Ernest Silinde
12. Wizara
ya Maji
a)
Waziri: Mhe. Jumaa Hamidu Aweso
b)
Naibu Waziri: Mhe. Kundo Andrea Mathew
13. Wizara
ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
a)
Waziri: Mhe. Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho
14. Wizara
ya Ujenzi
a)
Waziri: Mhe. Abdallah Hamis Ulega
b)
Mhandisi Godfrey Msongwe Kasekenya
2
15. Wizara
ya Uchukuzi
a)
Waziri: Mhe. Prof. Makame Mbarawa Mnyaa
b)
Naibu
Waziri: Mhe. David Mwakiposa Kihenzile
16. Wizara
ya Viwanda na Biashara
a)
Waziri: Mhe. Judith Salvio Kapinga
b)
Naibu Waziri: Mhe. Patrobas Paschal Katambi
17. Wizara
ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
a)
Waziri: Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki
b)
Naibu Waziri: Mhe. Switbert Zacharia Mkama
18. Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum
a)
Waziri: Mhe. Dkt. Dorothy Onesphoro Gwajima
b)
Naibu Waziri: Mhe. Maryprisca Winfried Mahundi
19. Wizara
ya Afya
a)
Waziri: Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa
b)
Naibu Waziri: Mhe. Dkt. Florence George Samizi
20. Wizara
ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
a)
Waziri: Mhe. Prof. Adolf Faustine Mkenda
b)
Naibu Waziri: Mhe. Wanu Hafidh Ameir
21. Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
a)
Waziri: Mhe. Dkt. Leonard Douglas Akwilapo
b)
Naibu Waziri: Mhe. Kaspar Kaspar Mmuya
22. Wizara
ya Maliasili na Utalii
a)
Waziri: Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji
b)
Naibu Waziri: Mhe. Hamad Hassan Chande
23. Wizara
ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
a)
Waziri: Prof. Palamagamba John Kabudi
b)
Naibu Waziri: Mhe. Hamisi Mwinjuma
c)
Paul Christian Makonda
3
24. Wizara
ya Mifugo na Uvuvi
a) Waziri:
Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
b) Naibu
Waziri: Mhe. Ng'wasi Damas Kamani
25. Wizara
ya Madini
a) Waziri:
Mhe. Anthony Peter Mavunde
b) Naibu
Waziri: Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa
26. Wizara
ya Nishati
a)
Waziri: Mhe. Deogratius John Ndejembi
b) Naibu Waziri: Mhe. Salome Wycliffe
Makamba
27. Wizara
ya Katiba na Sheria
a) Waziri:
Mhe. Juma Zuberi Homera
b) Naibu
Waziri: Mhe. Zainabu Athman Katimba

Maoni
Chapisha Maoni