Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2025

NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO

Picha
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Ofisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu wenye ulemavu kwa Chama cha Watu Wenye Ulemavu katika Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam. Ofisa Mkuu wa Habari wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Yahya Charahani, akikabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu wenye ulemavu kwa Chama cha Watu Wenye Ulemavu katika Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo Septemba 18,2025. Msaada huo umejumuisha magongo ya kutembelea (crutches), baiskeli za walemavu, na vifaa vingine vya kusaidia watu wenye uhitaji maalum kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Charahani alisema: "Tumefika hapa leo kwa niaba ya Shirika la Nyumba la Taifa kuonyesha mshikamano wetu na watu wenye ulemavu. Tunatambua changamoto wanazopitia, na msaada huu ni sehemu ndogo ya mchango wetu kwa jamii ambayo sisi pia ni sehemu ya...

MAWAKILI SERIKALI WATAKIWA KUSHIKA, KUZINGATIA SHERIA, KANUNI ZA HIFADHI YA JAMII

Picha
 Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari amewataka Mawakili wa Serikali kuhakikisha kuwa Sheria na Kanuni za Hifadhi ya Jamii zinalinda na kusimamia haki na maslahi ya Wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari akizungumza wakati wa kufungua mafunzo kwa mawakili wa Serikali yaliyoandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF mjini Kibaha, Pwani leo Septemba 18,2025. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kuhusu Hifadhi ya Jamii kwa Mawakili wa Serikali yaliyoandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF yanayofanyika Septemba 18 hadi19 Setpemba, 2025 katika Chuo cha Uongozi Mwalimu Nyerere Kibaha, mkoani Pwani. Johari amesema kuwa mafunzo hayo yatawanufaisha Mawakili wa Serikali kwa kuongeza ujuzi kwenye masuala mbalimbali hasa sheria zinazohusiana na Hifadhi ya Jamii ikiwemo , Sheria ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma [Sura ya 371], Sheri...

Ada Cottrell yawasaidia watoto wenye mahitaji Zanzibar

Picha
  Mwandishi Wetu, Zanzibar Taasisi ya Ada Cottrell Foundation kwa kushirikiana na Taasisi ya Labayka Development Foundation ( LDF ), imetoa msaada kwa watoto wanaoishi kwenye mazingila magumu ili kuwawezesha kujikimu kwa mahitaji yao. Baadhi ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu eneo la Nungwi Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa msaada kutoka taasisi ya A da Cottrell Foundation ya Marekani kwa kushirikiana na Taasisi ya Labayka Development Foundation ( LDF ) ikiwa ni sehemu ya kumuenzi marehemu Robert Cottrell. Msaada huo umetolewa kwa Watoto hao walio katika Kata ya Nungwi, Kijiji cha Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A na Mkoa wa Kaskazini Unguja, visiwani   Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi msaada huo, Mkurungezi Muwakilishi wa taasisi ya Ada Cottrell Foundation, Shedrack Gabriel Albert amesema hatua hiyo ni mwendelezo wa utaratibu unaofanywa kila mwaka na taasisi hiyo, ikiwa ni kumbukizi ya marehemu Robert Cottrel...

Madaktari Bingwa wapiga kambi Hospitali ya Kitengule kuhudumia wananchi

 

BENJAMIN NGAYIWA AAHIDI KUTOKOMEZA MIGOGORO YA ARDHI

Picha
Mwandishi Wetu, Kahama Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kahama Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Benjamin Ngayiwa, ameweka wazi dhamira yake ya kumaliza kabisa changamoto ya migogoro ya ardhi inayowakumba wakazi wa jimbo hilo kwa muda mrefu.  Akiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM ngazi ya jimbo, uliofanyika katika viwanja vya Phantom, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga, Ngayiwa amewahakikishia wananchi kuwa ardhi haitakuwa chanzo cha migogoro tena endapo atapewa ridhaa ya kuwa Mbunge wao. Katika hotuba yake, Ngayiwa alisisitiza kuwa atashirikiana kwa karibu na Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Mitaa ili kuhakikisha kuwa migogoro yote ya ardhi inatatuliwa kwa haki na kwa wakati. Aidha, Ngayiwa ametoa wito maalum kwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kuacha mara moja tabia ya kupima na kuwauzia watu zaidi ya mmoja kiwanja kimoja.  Amesema kuwa utaratibu huo siyo tu unawanyima haki wananchi, bali pia umekuwa chanzo kikuu cha migogoro isiyokwisha ya ardhi katika mae...

WAZAZI WAASWA KUTOACHA MALEZI KWA WALIMU PEKEE

Picha
Mwandishi Wetu, Kahama Wazazi wametakiwa kuendelea kushiriki kikamilifu katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao kielimu na kimaadili, badala ya jukumu hilo kuwaachia walimu  pekee. Wito huo ulitolewa na Mthibiti Ubora wa Shule wilayani Kahama, Athuman Abeid Al - Jabriy, alipohutubia mahafali ya darasa la saba katika Shule ya Msingi Greenstar, yaliyofanyika mwishoni mwa wiki. Abeid amesema kuwa dunia ya sasa inakabiliwa na mmomonyoko mkubwa wa maadili, na hivyo ni muhimu kwa wazazi kushirikiana kwa karibu na walimu katika malezi na maendeleo ya watoto. “Mtoto anapokabidhiwa shule kuanzia awali hadi darasa la saba, ni kipindi cha zaidi ya miaka minane. Kama mzazi hutafuatilia maendeleo yake, na walimu wakipoteza mwelekeo, mzigo wa marekebisho utakuwa juu yako. Tushirikiane katika malezi kwa manufaa ya baadaye ya watoto wetu,” amesema Abeid. Aidha, amewasihi wahitimu wa darasa la saba kutambua kuwa mahafali si mwisho wa safari ya elimu, bali ni mwanzo wa hatua nyingine muhimu. Alisi...

Salum Mwalimu aja na kuwekezesha vijana kuanzisha kampuni za utalii, biashara

Picha
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, ameahidi kuanzisha mfuko maalumu wa kuwawezesha vijana kuwekeza katika sekta ya utalii, iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu, utakaofanyika Oktoba 29,2025. Ametoa ahadi hiyo alipokuwa akiiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Arusha, ambapo amesema mpango huo utahusisha utoaji wa magari ya kuanzia, mitaji midogo na mafunzo maalum kwa vijana wenye ndoto ya kuingia kwenye biashara ya utalii. "Mpango huo ni sehemu ya ajenda ya CHAUMMA ya kupanua wigo wa ajira kwa vijana," amesema Mwalimu. Mgombea urais huyo wa CHAUMMA ameitaka jamii kuwa tayari kuunga mkono juhudi hizo kwa kushiriki kikamilifu kwenye mabadiliko ya kiuchumi kupitia sekta zenye fursa.

Dk. Samia: Tutawaanzishia wakulima vituo kukodi matrekta

Picha
-Asema zana zingine pia zitakodishwa Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan amesema akichaguliwa kuiongoza Tanzania katika uchaguzi ujao Oktoba 29,2025 ataanzisha vituo vya ukodishaji matrekta na zana zingine za kilimo kwa wakulima nchini. Akizungumza katika Uwanja wa Samora ulipofanyika mkutano wa Kampeni za CCM leo Septemba 7 mkoani Iringa, Rais Samia pichani juu, a mesema matrekta na zana hizo za kilimo  zitakuwa zikikodishwa kwa nusu ya bei ya matrekta ya watu binafsi. "Endapo Wananchi watanipa ridhaa ya kuongoza tena nchi kwa kunichagua katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025, Serikali yangu itaendelea kutoa ruzuku ya mbolea na pembejeo kwa wakulima nchini," amesema mgombea. Kwa mujibu wa mgombea urais huyo kitendo cha Serikali kutoa ruzuku katika mbolea kumeleta tija ya uzalishaji wa mazao na hasa mahindi, yaliyoifanya Tanzania kushika nafasi ya pili kwa uzalishaji Afrika kutokana na kuzalisha z...

Tukio la kihistoria la Kupatwa kwa Mwezi usiku huu Septemba 7, 2025

Picha
 Picha tofauti zatukio la Kupatwa kwa Mwezi kama lilivyonaswa na kamera ya daimatznews blogspot usiku huu;

Kairuki: Mkinichagua Kibamba itabamba

Picha
 Mgombea Ubunge Jimbo la Kibamba kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), Angela Kairuki  ( Pichani chini kushoto) , amezindua kampeni za kuwania kiti hicho leo Septemba 7,2025, akisema kuwa iwapo wananchi wa jimbo hilo watamchagua kuwa mbunge wao katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,2025 basi 'Kibamba Itabamba.' Kairuki ametoa kauli hiyo kwenye mkutano wake wa kwanza wa kampeni eneo la Mbezi Stendi jimboni humo mkoani Dar es Salaam ambapo amesema anazijua changamoto za jimbo hilo na matarajio yao, kwa kuwa yeye ni 'mtoto' wa Kibamba na kuwaahidi wananchi kwamba atawatatulia changamoto zote zilizopo jimboni humo. "...Mimi ni mtoto wa Kibamba, nimekulia Kibamba, nimeyaishi maisha ya Kibamba, nimeyaishi mafanikio ya Kibamba, lakini pia changamoto za Kibamba, najua matamanio, nayajua pia matamanio ya wana Kiamba. Niwahakikishie, nimedhamiria kuunganisha nguvu zangu na zenu, ili kupata majawabu ya changamoto za Kibamba. Niwahakikishie, e ndapo mtamchagua Dk. Samia Suluhu H...

NUKUU TATU ZA MGOMBEA URAIS CHAUMMA SALUM MWALIM LEO HIZI HAPA

Picha
                 NUKUU TATU ZA MGOMBEA URAIS CHAUMA KOROGWE 03/09/2025 1."Vijana wenzangu jengeni imani kwangu ili tutatue kero zetu, uwezo ninao na sifa ninazo za kuzalisha ajira, wanawake mtajifungua kwa stara na siyo kubeba vifaa kama mnakwenda kuanza shule ya msingi"  2.  "Msikubali kufanywa mazwazwa, wanaokufa ni watoto na wazazi wenu kwa sababu mmeikubatia CCM, uamuzi wa kuikataa  wakwenu ili kukichagua chama kingine muonje radha yake" Mgombea Salum Mwalimu - CHAUMMA Korogwe Vijijini. 3." Tunatakiwa kuwa na kilimo cha utashi ili kulima.mazao yote ya biashara katika mikoa yote ili kuiondoa Tanzania katika umaskini, tuchagueni  CHAUMMA ili neema aliyotujaalia tuitumie ya kuwekeza katika kilimo hata tukajenga kiwanda kidogo cha juisi ili watu wapate ajira" Mgombea wa CHAUMMA Salum Mwaiim Jimbo la Muheza.

TCU yatoa siku 18 udahili awamu ya pili Vyuo Vikuu

Picha
 -Udahili kuongezeka Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imetangaza kufunguliwa kwa Awamu ya pili ya udahili wa Shahada ya Kwanza kwa Mwaka wa Masomo 2025/2026, utakaofanyika kwa siku 18 ukianzia leo Septemba 3 hadi 21, 2025. Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, a kizungumza na wanahabari leo mkoani Dar es Salaam,  Akizungumza na wanahabari leo mkoani Dar es Salaam,  Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, amewataka  waombaji walioshindwa kutuma maombi ya udahili au kukosa  nafasi katika awamu ya kwanza ya udahili kwa sababu mbalimbali kutumia fursa hiyo kuomba udahili. Profesa Kihampa, amesema kwamba kufunguliwa kwa dirisha hilo ni hatua iliyofuata  kukamilika kwa Awamu ya Kwanza ya Udahili wa Shahada ya Kwanza katika Taasisi za Elimu ya Juu nchini kwa mwaka wa masomo 2025/2026. "Majina ya waliodahiliwa katika awamu ya kwanza yatatangazwa na vyuo husika kwa mujibu wa utaratibu,"amesema Profesa Kiham...

Makamu wa Rais alivyotoa maagizo, NHC yafunguka

Picha
- Mkurugenzi Hamad aeleza NHC ilivyogusa kila mkoa Tanzania - NHC ilivyong’ara mkutano wa Wenyeviti wa Bodi, Wakurugenzi Arusha Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Phillip Mpango, ameliagiza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuongeza juhudi zake katika ujenzi wa nyumba za gharama nafuu, lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wote wanaostahili kupata makazi wanapata fursa hiyo kupitia shirika hilo. Makamu wa Rais Dk. Isdor Mpango(Wa kwanza Kulia) akitembelea mabanda ya maonyesho ya shughuli zinazofanywa na taasisi za umma Viwanja vya AICC, Arusha hivi karibuni. Dk. Mpango ametoa agizo hilo wakati alipotembelea banda la NHC kwenye viwanja vya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), wakati wa Kongamano la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma. Alizungumza kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye kongamano hilo lililofanyika kuanzia tarehe 23 Agosti, 2025. "Nawaagiza muo...