Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2025

NUKUU TATU ZA MGOMBEA URAIS CHAUMMA SALUM MWALIM LEO HIZI HAPA

Picha
                 NUKUU TATU ZA MGOMBEA URAIS CHAUMA KOROGWE 03/09/2025 1."Vijana wenzangu jengeni imani kwangu ili tutatue kero zetu, uwezo ninao na sifa ninazo za kuzalisha ajira, wanawake mtajifungua kwa stara na siyo kubeba vifaa kama mnakwenda kuanza shule ya msingi"  2.  "Msikubali kufanywa mazwazwa, wanaokufa ni watoto na wazazi wenu kwa sababu mmeikubatia CCM, uamuzi wa kuikataa  wakwenu ili kukichagua chama kingine muonje radha yake" Mgombea Salum Mwalimu - CHAUMMA Korogwe Vijijini. 3." Tunatakiwa kuwa na kilimo cha utashi ili kulima.mazao yote ya biashara katika mikoa yote ili kuiondoa Tanzania katika umaskini, tuchagueni  CHAUMMA ili neema aliyotujaalia tuitumie ya kuwekeza katika kilimo hata tukajenga kiwanda kidogo cha juisi ili watu wapate ajira" Mgombea wa CHAUMMA Salum Mwaiim Jimbo la Muheza.

TCU yatoa siku 18 udahili awamu ya pili Vyuo Vikuu

Picha
 -Udahili kuongezeka Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imetangaza kufunguliwa kwa Awamu ya pili ya udahili wa Shahada ya Kwanza kwa Mwaka wa Masomo 2025/2026, utakaofanyika kwa siku 18 ukianzia leo Septemba 3 hadi 21, 2025. Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, a kizungumza na wanahabari leo mkoani Dar es Salaam,  Akizungumza na wanahabari leo mkoani Dar es Salaam,  Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, amewataka  waombaji walioshindwa kutuma maombi ya udahili au kukosa  nafasi katika awamu ya kwanza ya udahili kwa sababu mbalimbali kutumia fursa hiyo kuomba udahili. Profesa Kihampa, amesema kwamba kufunguliwa kwa dirisha hilo ni hatua iliyofuata  kukamilika kwa Awamu ya Kwanza ya Udahili wa Shahada ya Kwanza katika Taasisi za Elimu ya Juu nchini kwa mwaka wa masomo 2025/2026. "Majina ya waliodahiliwa katika awamu ya kwanza yatatangazwa na vyuo husika kwa mujibu wa utaratibu,"amesema Profesa Kiham...

Makamu wa Rais alivyotoa maagizo, NHC yafunguka

Picha
- Mkurugenzi Hamad aeleza NHC ilivyogusa kila mkoa Tanzania - NHC ilivyong’ara mkutano wa Wenyeviti wa Bodi, Wakurugenzi Arusha Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Phillip Mpango, ameliagiza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuongeza juhudi zake katika ujenzi wa nyumba za gharama nafuu, lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wote wanaostahili kupata makazi wanapata fursa hiyo kupitia shirika hilo. Makamu wa Rais Dk. Isdor Mpango(Wa kwanza Kulia) akitembelea mabanda ya maonyesho ya shughuli zinazofanywa na taasisi za umma Viwanja vya AICC, Arusha hivi karibuni. Dk. Mpango ametoa agizo hilo wakati alipotembelea banda la NHC kwenye viwanja vya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), wakati wa Kongamano la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma. Alizungumza kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye kongamano hilo lililofanyika kuanzia tarehe 23 Agosti, 2025. "Nawaagiza muo...