NHC yapata tuzo maalum vigezo vitano vikiibeba

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limetunukiwa tuzo maalum, baada ya kuibuka kuwa moja ya mashirika  ya umma yaliyofanya vizuri katika mwaka wa fedha 2023/24.

Tuzo hiyo imetolewa na Ofisi ya Msajili wa Hazina katika hafla rasmi iliyofanyika kwenye Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma, kilichofunguliwa rasmi Agosti 2,2025 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Philip Mpango, jijini Arusha.

Tuzo hizo zilizingatia vigezo vya kiuendeshaji ikiwamo ukuaji wa mapato ya ndani, kuboresha ukwasi, rejesho la uwekezaji, udhibiti wa matumizi na kuimarisha faida.

Vigezo vingine ni kupunguza utegemezi wa ruzuku ya Serikali, ufanisi katika matumizi, utekelezaji wa hoja za kikaguzi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), uchapishaji wa taarifa za fedha, na maboresho ya utoaji huduma kwa jamii.

Taasisi nyingine zilizotunukiwa tuzo maalum zilitangazwa chini ya makundi manne mahsusi kulingana na aina na majukumu husika huku NHC likiwa katika  kundi la mashirika yanayofanya biashara,  ambapo tuzo zilitolewa kwa mashirika yaliyoboresha mapato, faida, ukwasi na rejesho kwa mtaji wa Serikali.

Pamoja na NHC katika kundi hilo wengine walioshinda ni  Bohari ya Dawa (MSD) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi