Rais Paul Kagame, Balozi Kombo wateta Ikulu ya Rwanda
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, pichani chini, wamekutana na kufanya mazungumzo, Ikulu ya Kigali, nchini Rwanda.
Katika mazungumzo yao wawili hao, wamezungumzia ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Rwanda pamoja na matunda ya Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Rwanda, uliofanyika kwa siku tatu jijini Kigali, tarehe 24 hadi 26 Julai, 2025.
Maoni
Chapisha Maoni