Na Hussein Ndubikile,daimatznews@gnail.com
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi ili kuboresha iundombinu kwa lengo la kuongeza ajira kwa Watanzania.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Desemba16,2024 katika Uzinduzi wa Muonekano na chupa mpya ya lita moja ya juisi ya African Fruti inayozalishwa na Kompuni ya Bakhresa Food Products Limited (BFPL), Dk. Jafo amesema sekta binafsi inategemewa kubeba jukumu la kuongeza ajira nchini.
“Serikali haiwezi kuwaajiri watu wote; sekta binafsi ndio nguzo ya kutengeneza ajira. Uwekezaji kama huu unasaidia vijana na wakulima kuongeza uzalishaji,” amesema Dk. Jafo, akitoa mfano wa uwekezaji wa zaidi ya Sh 700 bilioni wa Bakhresa.
Ameongeza kuwa miundombinu kama reli ya Standard Gauge inayotumia umeme (SGR) na barabara inaimarishwa ili kuchochea uzalishaji viwandani na kuhimiza Watanzania kupenda bidhaa za ndani.
Mkurugenzi wa Uhusiano wa Bakhresa Group, Hussein Sufian, amesema bidhaa zinazotumia malighafi za ndani huchangia kukuza uchumi.
Amebainisha kuwa kiwanda hicho kimeongeza uwezo wa kuchakata matunda kutoka tani 50,000 hadi 100,000 kwa mwaka na bidhaa hizo zinauzwa katika mataifa mbalimbali, ikiwemo Kenya, China na Mashariki ya Kati, zikichangia pato la fedha za kigeni kwa taifa na ajira kwa vijana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tetra Pak, Jonathan Kinisu, amesifu ushirikiano wa miaka 17 baina ya kampuni hizo, akisema umeleta teknolojia rafiki kwa mazingira na bidhaa bora zisizo na kemikali.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa BFPL, Salim Aziz, amesema kuwa malengo ya kampuni hiyo yanaendana na ajenda ya Serikali ya kukuza uchumi kupitia bidhaa za ndani na uundaji wa ajira.
Amebainisha kuwa kiwanda hicho kimeongeza uwezo wa kuchakata matunda kutoka tani 50,000 hadi 100,000 kwa mwaka na bidhaa hizo zinauzwa katika mataifa mbalimbali, ikiwemo Kenya, China na Mashariki ya Kati, zikichangia pato la fedha za kigeni kwa taifa na ajira kwa vijana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tetra Pak, Jonathan Kinisu, amesifu ushirikiano wa miaka 17 baina ya kampuni hizo, akisema umeleta teknolojia rafiki kwa mazingira na bidhaa bora zisizo na kemikali.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa BFPL, Salim Aziz, amesema kuwa malengo ya kampuni hiyo yanaendana na ajenda ya Serikali ya kukuza uchumi kupitia bidhaa za ndani na uundaji wa ajira.
0 Maoni