-Yajipanga kujenga nyumba za makazi mikoa 20
-Wizara, Bodi ya Wakurugenzi yafurahishwa
-Yataka iendelee kutimiza ndoto ya makazi bora kwa wananchi
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail,com
“Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linaendelea kukua, linaendelea kukomaa, linajitosheleza kila eneo na sasa linaweza kuaminiwa kutekeleza mradi wowote mkubwa wa ujenzi wa nyumba, tunajivunia kuwa na kiwango bora katika utekelezaji miradi.”
Katika ziara hiyo Dk.Kongela aliambatana na wajumbe wa Bodi anayoiongoza, ambapo kwa pamoja walishuhudia miradi hiyo ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika, kabla ya kuanza kutumika.
Kupitia mkataba wake na Serikali, NHC inajenga majengo ya Wizara ya Nishati, Wizara Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo, Wizara ya Madini, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Pia inajenga ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Nishati, huku ujenzi wa miradi hiyo ukifikia asilimia 90.
“Ni fahari kuwa wataalam vijana wanaotekeleza mradi huu, ni hazina kwa NHC na taifa kukamilisha mradi mkubwa bila kuwa na wataalam wa kigeni,” anasema Dk.Kongela.
Kuhusu kukamilika, kukabidhi na kuanza kutumika majengo hayo Mwenyekiti huyo wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC anasema:
“Ushauri wangu Menejiimenti ya NHC kupambana kwa muda mfupi uliopo kukamilisha mradi ndani ya muda. Hiyo ndiyo fahari yetu, sote tunapambania jambo hilo.”
Akizungumzia mikakati ya baadae ya Shirika la Nyumba laTaifa, Dk, Kongela anasema katika bajeti ya mwaka 2025/26 NHC ina mpango wa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa nyumba za makazi zikitarajiwa kunufaisha Watanzania wenye uhitaji wa nyumba.
“Tutakuwa na mradi
mkubwa wa ujenzi wa nyumba za makazi, nyingi zitajengwa na Dodoma ni
kipaumbele, mradi wa Medeli awamu ya
pili utaiongezea makao makuu ya Serikali hadhi katika makazi,”anasema Dk,
Kongela.
Anaongeza kuwa ujenzi wa nyumba za makazi utawafikia hata wananchi wa Kahama wenye hamu ya kupata nyumba za NHC na kwamba shirika hilo linatambua uhitaji wa nyumba za makazi kila mkoa.
“NHC ina orodha ya mahitaji ya nyumba za makazi, sio Kahama peke yake, mikoa 20 itaanza kuongezewa nyumba za makazi,” anasema Mwenyekiti huyo wa Bodi ya NHC huku akitoa maagizo;
“Kwa Menejimenti
tunaelekeza,ndoto yetu ni kuona NHC inatimiza haja ya uhitaji wa nyumba za
makazi kwa wananchi, wafanye yote ndani ya muda, itekeleze hayo.”
Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, Mhandisi Anthony Sanga
aliyefika kwenye eneo hilo ameipongeza Bodi ya NHC kwa kukagua maendeleo ya
ujenzi huo akiwasihi NHC kuongeza kasi kukamilisha kazi hiyo.
“Nimewasihi waongeze kasi, ujenzi ukamilike ili Januari 2025 tuingie na kufanyia kazi humu.
Hatuna shaka na ubora wa kazi ya NHC. Sasa wanamalizia, Bodi na Menejimenti ya NHC wanafanya kazi nzuri, sisi wasimamizi wa Wizara tumeridhika,” anasema Mhandisi Sanga.
“Kwa ujumla ziara imekwenda vizuri, Bodi imechangia ufanisi wakazi hii kwani ndiyo inatusimamia hasa katika miradi ya Serikali nao wamekuwa wakitaka kuona maendeleo ya miradi mara kwa mara, bila usimamizi wa Bodi maana yake hakuna usimamizi mzuri,” anasema Hamad na kuongeza;
“Sisi menejimenti kila miezi mitatu tunapeleka taarifa kwa Bodi, bahati nzuri Bodi ya NHC inafanya maamuzi yenye tija. Maamuzi yao mazuri, usimamizi wao unatuwezesha kukamilisha kazi hii kwa wakati.”
Anasema mbali ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti ya NHC ina Kamati za Utekelezaji zinazofanya kazi katika miradi ya Serikali ikiwamo huo wa Ujenzi wa Ofisi za Wizara nane za Serikali Mtumba, Dodoma na kuwasilisha taarifa za utekelezaji kwa kila mwezi na yeye (Mkurugezi) huziwasilisha kwa Bodi.
Ametaja moja ya faida ya mradi huo ni kuzalisha ajira hasa kwa vijana na kupata fursa za kujifunza umahiri wa taaluma mbalimbali zinazoendana na fani ya ujenzi.
Mkurugenzi Mkuu huyo wa NHC, anaweka wazi gharama za kazi hiyo kuwa ni shilingi bilioni 186.8 akichanganua kwamba mradi wa ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 22.30, Wizara ya Viwanda unajengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 22.99, Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo utagharimu shiingi bilioni 22.84 na jengo la Wizara ya Madini ukigharimu shilingi bilioni 22.84.
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ujenzi wake unagharimu shilingi bilioni 23.94 huku Wizara ya Nishati likigharimu shilingi bilioni 23,68 na la Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi linalojengwa kwa thamani ya shilingi bilioni 24. 98.
![]() |
Jengo la ofisi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi linalojengwa na NHC katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma, likiwa hatua za mwisho kukamilika, |
0 Maoni