Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Waandishi wataka Dudley Mbowe aende gerezani

-Kuuanza mwaka 2025 mahakamani 
-Ni kwa kushindwa kuwalipa
-Adaiwa kuvunja makubaliano mara mbili

Na Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com

Jengo la Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi Dar es Salaam 

MAHAKAMA Kuu Divish.eni ya Kazi, Januari 6,2025  inatarajia kuanza kusikiliza maombi ya waandishi wa habari Maregesi Paul na wenzake 9 wanaotaka Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe aamriwe kwenda gerezani kama mfungwa wa madai kwa kushindwa kulipa malimbikizo ya misharaha yao.

Mbele ya Naibu Msaiji wa Mahakama Kuu, Mary Mrio mahakamahiyo imetoa uamuzi huo leo Desemba 17,2024 wakati shauri hilo lilipokuwa likitajwa.

Akiwakilisha wenzake, Maregesi aliieleza Mahakama kwamba hati ya wito ilimfikia Dudley ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na aliahidi kufika lakini hakutokea bila kuwepo taarifa zozote.

Msajili Mrio amesema kwa kuwa Dudley alishapelekewa wito, shauri hilo litaendelea Januari 6 mwakani 2025 na pande zote zinatakiwa kuwepo mahakamani.

Wanahabari hao waliamua kuwasilisha maombi ya kumkamata na kumweka gerezani Dudley kwa  kushindwa kuwalipa  tuzo yao waliopatiwa na mahakama na hata walipoingia kwenye makubaliano nje ya mahakama Aprili 22, 2024 ya kulipa misharaha mitano hadi Mei mwaka huu hakufanya hivyo hadi leo.
Dudley Mbowe

Waandishi hao walishinda tuzo katika Tume ya Usuluhishi na Uamuzi(CMA) Julai 17, 2023 mbele ya Msuluhishi wa CMA Ilala,  Bonasia Mollel.

Madai ya awali yalikuwa jumla ya Sh milioni 114, lakini baada ya kukaa mezani kwenye majadiliano kwa pamoja walikubaliana kiwango hicho cha fedha kishuke hadi Sh milioni 62.7.

Dudley alikubali kulipa fedha hizo kwa awamu tatu, Oktoba 30, Desemba 30 mwaka 2023 na awamu ya mwisho ilikuwa mwishoni Februari, 2024, hata hivyo hakulipa na walipoingia katika makubaliano nje ya Mahakama pia akayavunja kwa kushindwa kutekeleza makubaliano.

Chapisha Maoni

0 Maoni