Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Bwana harusi akimbia na gari aliloazima, aliuza

Adaiwa kutapeli Mil 90

Ajificha kwa mganga Pemba, polisi wamnasa

 
Na Hussein Ndubikile, daimatznews@gmail.com

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam tarehe 15 Desemba, 2024 linamshikilia Vicent Peter Massawe, mkazi wa Kigamboni Dar es Salaam kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na wizi wa kuaminiwa.

Kamanda Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kutengeneza mazingira ya uongo ya kupotea na kutenengeza hisia kwa umma kuwa ametekwa na baadae kwenda kujificha Chakechake,Pemba visiwani Zanzibar nyumbani kwa mganga wa kienyeji aliyetajwa jina na polisi kuwa ni Hamis khalid.

Akizungumza na wanahabari Jijini Dar es Salaam Desemba 17/2024, Kamanda Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro amesema ufutiliaji na mahojiano ya kina kati ya Polisi na mtuhumiwa {Baba harusi}, baada ya kupatikana alikiri kutenda makosa hayo, ambapo alilichukua pesa kwa udanganyifu kutoka kwa watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na Shilingi milioni.55 na gari namba T 642 EGU aina Toyota Ractis kwa udanganyifu kutoka kwa Sylivester Beda Massawe.

Kwa mujibu wa Kamanda Muliro, Massawe alichukua tena Shilingi milioni 10 kwa kutumia udanganyifu kutoka kwa Ramadhani mkazi wa Magomeni, pia alichukua pesa pia kwa udanganyifu Shilingi milioni15 kutoka kwa Ramadhani Bakari mkazi wa Temeke.

"Mtuhumiwa amechukua pesa pia kwa udanganyifu Shilingi milioni tano kutoka kwa Resma Mbuguni Ofisa Rasilimali Watu CBE. Alichukua tena kiasi cha shilingi milioni nne kutoka kwa Asia Mohamed mkazi Madale," amesema Muliro na kuongeza:

"Kwa udanganyifu Massawe alichukua tena Shilingi milioni moja na laki tano kutoka kwa mtu aliyejulikana kwa jina la Ngoma, mkazi wa Kibaha na aliendelea tena kwa udanganyifu kuchukua Sh milioni 8 kutoka kwa Fauz Suleimani Mussa, mkazi wa Tabata baada ya kumuuzia gari ambalo sio lake  bali aliazima siku ya harusi yake likiwa na namba za usahili T642 EGU aina ya Ractis mali ya Sylivester Beda Massawe.".

Kamanda Muliro amesema Novemba,18 mwaka huu Polisi Kigamboni ilipokea taarifa ya kupotea kwa Vicent Peter Massawe, Mfanyabiashara, iliyedaiwa hakuonekana tangu Novemba 18, 2024 baada ya harusi yake na alipotea huku akitumia gari hiyo.

"Baadae ilibainika mtuhumiwa aliiuza gari hiyo badala ya kuirudisha kwa mwenyewe, baada ya harusi yake Novemba 16, 2024 katika ukumbi wa Golden Jubilee,: amesema Kamanda Muliro..

Jeshi la Polisi limesema uchunguzi kuhusu tuhuma  hizo unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa katika mamlaka nyingine za kisheria kwa hatua zaidi.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limetoa onyo na tahadhari kwa kikundi cha watu wanne aliowaelezea kuwa kazi yao ni kujenga taharuki kwa umma kuwa kila anayepotea au kutoonekana, wao hujitokeza na kuandika kwenye mitandao ya kijamii kuwa watu hao wamechukuliwa na gari hard top nyeupe na kulazimisha hisia kuwa ni vyombo vya dola vimehusika.

Amesema malengo makubwa ya kundi hilo kutoa taarifa za uzushi zenye taharuki ni kuichonganisha Serikali, Polisi na Wananchi. Jeshi halitasita kuwachukulia hatua kali na za kisheria wahusika ili kukomesha tabia hizo.


Chapisha Maoni

0 Maoni