'Miaka 63 ya Uhuru na NHC inayotimizia ndoto Watanzania'
- Ni ya makazi bora, yajenga
zaidi ya nyumba 30,000
- Awamu ya 6 pekee miradi ya zaidi ya Sh 212 bilioni
- Thamani miradi ya ubia yafikia Sh 191 bilioni
![]() |
Sehemu ya Mradi wa nyumba Samia Scheme |
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Tanzania
Bara ilipata Uhuru wake tarehe kama ya leo Desemba 9, mwaka 1961 kutoka kwa
Waingareza, ikihitimisha enzi za ukoloni, ambapo taifa lilitawaliwa na wageni
hao, ambao walikabidhiwa dhamana na Umoja wa Mataifa, lakini waliondoka nchini
bila kuacha mpango mkakati wowote wa makazi bora kwa wananchi.
Hata hivyo, kwa hekima, busara na kutambua mahitaji ya makazi bora kwa wananchi, mwaka mmoja baada Uhuru, Serikali iliyokuwa chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilianzisha Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), mwaka1962 kwa Sheria ya Bunge Na. 45.
Tangu kuanzishwa kwake wakati huo, hata sasa
Tanzania inapoadhimisha miaka 63 ya Uhuru, NHC limebeba jukumu muhimu la kuleta
mageuzi ya kipekee katika sekta ya nyumba nchini, likiwa na ndoto inayoendelea kuitimiza
ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata makazi bora.
Ushahidi
wa NHC kulibeba jukumu hilo kikamilifu ni mageuzi yanayoonekana katika sekta ya
nyumba nchini kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati ya shirika hilo
linalotajwa kuwa kubwa zaidi barani Afrika, likiwa na mtaji unaokadiriwa kufikia Shilingi Trilioni 5.
Awamu ya Sita
![]() |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan |
Kwa kuanzia, ushahidi wa NHC iliyo bora zaidi ikibeba majukumu yake kwa ukamilifu, unapatikana kwenye kipindi hiki cha utawala wa Awamu ya Sita, chini ya Uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na hata miaka ya nyuma awamu zilizotangulia.
Hilo haliwezi kufichika
kwani ndani ya kipindi hicho shirika limetekeleza na linaendelea kutekeleza
miradi mbalimbali ya ukandarasi ambayo moja kwa moja inagusa na kuchangia
maendeleo ya taifa Tanzania, mtu mmoja mmoja, wizara hata mashirika na kampuni.
Katika kipindi cha Awamu ya
Sita pekee yaani mwaka 2023/24, hadi Disemba
2024, miradi mbalimbali imetekelezwa kama ifuatavyo:-
i.
Ujenzi wa
Jengo la Kitengo cha Moyo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wenye
thamani ya shilingi bilioni 3.1 jijini Dar es Salaam umekamilika kwa asilimia
100.
iv.
Ujenzi wa Jengo
la Shule ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, umefikia asilimia 80
yautekelezaji, ukiwa na thamani ya Shilingi Bilioni 9.8.
Hata
hivyo, utekelezaji miradi hiyo na mingine mingi isingewezekana bila NHC
kufanyiwa mageuzi na kuiwekea mpango mkakati ikitazamwa historia yake na
malengo yake katika sekta ya nyumba.
Mpango Mkakati wa Maendeleo
Kwa
kuangalia mambo hayo mawili pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo, Mwaka 2010,
Serikali ilianza awamu mpya ya kuimarisha Shirika la Nyumba la Taifa kwa
kuboresha Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti. Lengo kufanya hivyo lilikuwa
kuongeza ufanisi, kujenga nyumba zaidi na kufanikisha ushirikiano kati ya sekta
ya umma na binafsi.
Katika
mazingira hayo Mpango Mkakati wa Miaka 10 kuanzia mwaka 2015/16–2024 hadi 2025
uliandaliwa. Mpango huu ulilenga ujenzi wa nyumba 10,000, usimamizi wa miradi
mikubwa na kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na taasisi za kifedha.
Pia
unatoa dira ya ukuaji wa sekta ya nyumba nchini, ikizingatiwa mahitaji ya sasa,
ongezeko la idadi ya watu na mustakabali wa taifa kwenye sera ya Ardhi na
Makazi.
Mafanikio
Licha ya machache yaliyotajwa kutekelezwa katika Awamu ya Sita, tangu Uhuru hadi sasa imefanikiwa kutekeleza na kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo, ambayo ni ushahidi mwingine wa mafanikio ya NHC kwa kipindi chote cha uhai wake wa miaka 62, tangu lilipoanzishwa mwaka 1962.
![]() |
Sehemu ya mradi wa majengo ya wizara nane za Serikali katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma. |
Miradi iliyotekelezwa na kukamilishwa na NHC tangu Uhuru inajumuisha:
Ujenzi wa nyumba 887 za makazi za kawaida katika eneo la Iyumbu na Chamwino Mkoani Dodoma (404), Wilaya ya Makete Mkoa wa Njombe (50), Chartur Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga (10) na Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi (24).- Ujenzi wa nyumba 521 kwa ajili ya biashara katika eneo la Mtukula mkoani Kagera (45), Medeli mkoani Dodoma (42), Dar Es Salaam (380) na Mwanza (54).
- Ujenzi wa nyumba 1,187 kwa ajili ya makazi na biashara katika eneo la Morocco Square (1,100) na miradi ya ubia (87) katika Jiji la Dar es Salaam.
- Shirika limeongeza rasilimali zake kwa kununua nyumba 896 zikiwemo nyumba za makazi 389 na nyumba 497 za biashara katika eneo la Urafiki Mkoa wa Dar es Salaam.
Mbali na miradi hiyo iliyokamilishwa, Shirika la
Nyumba la Taifa, linaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi iliyo
katika hatua tofauti za ujenzi.
Miradi hiyo inajumuisha; Ujenzi wa nyumba
560 katika mradi wa “Samia Housing Scheme” Awamu ya Kwanza katika eneo la Kawe jijini
Dar es Salaam ambao umefikia asilimia 54, unaotarajiwa kukamilika Januari 2025. Mradi huu
utawezesha ujenzi wa nyumba 5,000 nchini zitakazogharimu takriban shilingi
bilioni 466.
Mauzo ya nyumba hizo za
Kawe yameshakamilika, hii inatokana na Awamu ya Sita kufungua milango ya uchumi
na uwezeshaji wa mapato kwa wananchi.
Pia
kuna ujenzi wa nyumba 1,533 za makazi na biashara. Katika mradi wa Kawe 711
zinajengwa nyumba (422) na umefikia asilimia 45 ambao unatarajiwa kukamilika
mwezi Aprili 2026. Aidha, pia kuna ujenzi wa nyumba 532 kupitia mradi wa Golden
Premier Residence.
NHC na Sekta ya Fedha
Shirika
la Nyumba la Taifa pia limekuwa kiunganishi muhimu kati ya wananchi na taasisi
za kifedha nchini na tayari zaidi ya benki 22 zimeungana na NHC kuwezesha
mikopo ya nyumba ya muda mrefu.
NHC na Sekta Binafsi
Kupitia
sera ya ubia, NHC imefungua milango kwa sekta binafsi kushiriki katika ujenzi
wa nyumba na majengo ya kisasa. Ushirikiano huo umeongeza ushindani, ubora na
kupanua fursa za uwekezaji katika sekta ya nyumba nchini.
Kupitia
Sera ya Ubia iliyohuishwa mwaka 2022, NHC inaendelea na utekelezaji wa miradi
ya ubia, ambapo jumla ya miradi 20 yenye thamani ya Shilingi bilioni 191 iko tatika hatua mbalimbali za ujenzi.
Katika
eneo hilo, majengo makubwa ya kibiashara katikati ya miji ni ushahidi wa
mchango wa NHC katika kuboresha mandhari ya miji. Miradi kama vile ya nyumba za
makazi na ofisi, zimekuwa chanzo kikuu cha ajira na maendeleo ya kiuchumi kwa
taifa.
NHC historia na maono
Shirika
la Nyumba la Taifa (NHC), lilianzishwa kwa sheria ya Bunge, mwaka mmoja tu
baada ya Uhuru wa Tanganyika, likiwa ni sehemu ya maono ya Mwalimu Nyerere
kuhakikisha mahitaji ya msingi ya mwanadamu kama makazi, chakula na mavazi yanapatikana
kwa kila mwananchi.
NHC
miaka ya mwanzo lilitekeleza majukumu yake kupitia miradi mbalimbali ya ujenzi
wa nyumba na majengo ya umma. Hata hivyo, changamoto za kiuchumi na kisheria
ziliathiri utendaji wa Shirika.
Sheria
ya Zuio la Kodi ya Mwaka 1984 ilikuwa moja ya sheria zilizosababisha NHC na sekta
ya nyumba kusuasua kwa kuzuia uwekezaji wa sekta binafsi, kutokana na masharti
magumu kwa wamiliki wa nyumba.
Hata
hivyo mwaka 1990 mageuzi yalifanyika, ambapo NHC liliunganishwa nailiyokuwa
Msajili wa Majumba. Hili lilifanyika kupitia Sheria Na. 2, na NHC likapewa
mamlaka mapya ya kusimamia nyumba zilizotwaliwa na Serikali mwaka 1971.
Hatua
nyingine muhimu ilikuja mwaka 2005, pale Bunge lilipoondoa sheria zisizokuwa
rafiki na kuweka mazingira bora kwa uwekezaji, ikiwemo kuboresha Sheria ya
Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 na Sheria Na. 2 ya mwaka 1990 iliyounda upya Shirika
la Nyumba la Taifa.
NHC leo na kesho
Shirika
linaendelea kupanua wigo wa shughuli zake kwa kutumia utaalamu wa ndani na
teknolojia za kisasa, lengo ni kuimarisha utendaji, kuongeza ufanisi wa miradi,
na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Katika
miaka ijayo, NHC ina mpango wa kuanzisha miradi mingi zaidi ya makazi,
kuimarisha uhusiano wa kimataifa, pia kutoa ushauri wa kitaalamu katika miradi
mbalimbali.
![]() |
Mradi wa Morocco Square unavyoonekana |
NHC
inaendelea kushirikiana na Shirika la
Nyumba Zanzibar (ZHC) katika kuimarisha maendeleo ya nyumba ukanda wa
Afrika Mashariki. Ikumbukwe kuwa NHC ilishiriki kuasisiwa kwa ZHC mwaka 2014,
ambapo ilitoa mafunzo mbalimbali ya namna Shirika la Nyumba linavyotakiwa
kujiendesha.
Mafunzo
ya kitaalam na kwa wataalam wa ZHC kuja Tanzania Bara na kujifunza mambo ya
nyumba, ikiwemo mafunzo ya utayarishaji wa Sheria za Shirika la Nyumba Zanzibar.
Ziara mbalimbali za kubadilishana uzoefu kwa Bodi na Menejimenti ya pande mbili
za Muungano pia zimefanyika.
Kwa
zaidi ya miaka 61, NHC limekuwa kiungo muhimu katika safari ya Tanzania
kuelekea makazi bora. Kutoka kwenye changamoto za awali hadi mafanikio ya sasa,
Shirika linaonyesha mfano wa jinsi taasisi za umma zinavyoweza kuchangia
maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Mustakabali
wa Shirika ni mzuri na kupitia mipango madhubuti, NHC itaendelea kuwa chachu ya
maendeleo ya sekta ya nyumba nchini Tanzania, ikihakikisha kila Mtanzania
anafurahia haki ya makazi bora.
Maoni
Chapisha Maoni