Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2024

Kunani tarehe 29 kwa Rais Dk. Samia CCM?

Picha
- Aliamua ya Chongolo, ameamua ya Kinana Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Sijui unakumbuka.. au najua? Kama hukumbuki au hujui, nitakuwekea sawa kumbukumbu kuhusu maamuzi makubwa, mazito mawili ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (CCM), Rais Dk, Samia Suluhu Hassan ndani ya chama hicho tawala. Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan Ni hivi, kumbukumbu zinaonyesha kuwa tarehe 29 ndiyo CCM ilitangaza maamuzi magumu ya Mwenyekiti wake huyo wa Taifa, yaliyobeba mustakabali wa chama hicho tawala ndani ya miezi minane, Novemba 29,2023 hadi Julai 29,2024. Tarehe hiyo, ndipo alitangaza kuridhia kujiuzulu kwa Daniel Chongolo aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, mwaka uliopita 2023 na mwaka huu 2024, ameridhia kujiuzulu kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Kanali Mstaafu, Abdulrahman Kinana. Taarifa ya CCM ya jana Julai 29, 2024 imeeleza kwamba Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ameridhia ombi la Makamu Mwenyekiti wake, Kinana kujiuzulu wa...

Kimbunga cha Rais Samia chang'oa vigogo wengine sita

Picha
  Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Siku chache baada ya kuwaondoa madarakani mawaziri watatu wa Serikali yake, akiwamo aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia na Habari, Nape Nnauye, kimbunga cha Rais Dk Samia Suluhu Hassan safari hii kimewakumba watendaji sita wa taasisi zilizokuwa chini ya wizara hiyo iliyoongozwa na Nape. Rais Dk, Samia Suluhu Hassan akisistiza jambo katika moja ya mikutano yake. Taarifa iliyotolewa leo Julai 23, 2024 na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,Ikulu, Sharifa Nyanga ikinukuu taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka imeeleza kuwa Rais Samia ametengua uteuzi wa viongozi mbalimbali. "Waliotenguliwa ni kama ifuatavyo;..Zuhura Sinare Muro, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurgenzi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na Mhandisi Peter Rudolf Ulanga, Mkurugenzi wa TTCL," imeeleza taarifa hiyo ikimnukuu Balozi Dk. Kusiluka na kutaja wengine waliotenguliwa nyadhifa zao kuwa ni: "Brigeia Mstaafu Yohaya Ocholla Mabongo, ...

Serikali yatoa Sh16.8 BIL kujenga minara ya mawasiliano

Mwandishi Wetu, WHMTH, Shinyanga  Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni 16.89 kwa mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa, ili kujenga minara ya mawasiliano. Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (Mb), amebainisha hayo akieleza kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa minara 117 katika kata 113, vijiji 240 vya mikoa ya Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza na Shinyanga. Nape amebainisha hayo leo Julai 19, 2024, alipowahutubia wananchi katika Kata ya Bukomela, Wilaya ya Kahama, Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga, katika majumuisho ya ziara yake ya siku tano katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa. ā€œNdugu zangu wa Ngokolo, ndani  mradi huu wa Tanzania ya Kidigitali, upo mradi mwingine mkubwa wa ujenzi wa minara 758, tunapeleka mikoa 26 ya Tanzania Bara na ndiyo maana napita mkoa kwa mkoa.  Kwanzaa minara hii tumelenga kuwaunganisha Watanzania milioni 8.5 na wote tunataka waguswe na huduma za mawasiliano kama vile Ngok...

UCSAF yatumia Bil 4.27 kujenga minara 30 Shinyanga

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Shinyanga  Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), imetoa ruzuku ya Shilingi Bilioni 4.27, kuwawezesha watoa huduma za mawasiliano, kujenga minara 30 ya mawasiliano mkoani Shinyanga. Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Justina Mashiba akisoma taarifa kuhusu ujenzi wa minara ya mawasiliano unaotekelezwa kati ya mfuko huo na waau mbalimbali wa mawasiliano mbele ya  W aziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (Mb.), aliye katika ziara ya kikazi mkoani Shinyanga . Mashiba amemweleza Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (Mb.), aliye katika ziara ya kikazi mkoani Shinyanga kwamba, minara hiyo imejengwa katika Wilaya za Kahama Manispaa, Kishapu, Msalala, Shinyanga DC na Ushetu.            Kuhusu mradi wa mnara 758 inayojengwa katika mikoa 26 ya Tanzania Bara,  Mashiba amesema Mkoa wa Shinyanga ni moja ya mikoa hiyo, inakojengwa minara 30, na ruzuku ya UCSAF iliyotumika...

Shinyanga yasajili laini milioni mbili za simu, kitaifa zafikia bilioni 72

Picha
Mwandishi Wetu,WHMTH, Shinyanga  Wakati laini za simu zilizosajiliwa nchi nzima zikifikia milioni 72.4, Mkoa wa Shinyanga pekee, zimesajiliwa laini 1,966,528 ambazo ni sawa na asilimia 2.71 ya laini zote nchini . Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe Nape Nnauye (kulia) akiwa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba  kwenye Boti ya Mwendokasi  Ziwa Viktoria, kuelekea kukagua mnara wa VODACOM uliopo katika Kata ya Chifunfu, Kijiji cha Chifunfu, Kisiwa cha Lyakanyasi, Sengerema mkoani Mwanza Julai 18,2024 katika ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa minara ya Mawasiliano mkoani humo. Mkurugenzi wa Leseni na Ufuatiliaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Wakili John Daffa amebainisha hayo leo Julai 19, 2024 wakati akitoa wasilisho la hali ya huduma ya mawasiliano kwa mkoa huo, mbele ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (Mb), na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa...

'Wananchi msinunue vocha kwa bei isiyo ya Serikali'

Mwandishi Wetu, WHMTH, Mwanza Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) amewataka wananchi kutokubali kununua vocha kwa bei tofauti na iliyoandikwa kwenye vocha hizo ambayo zimeelekezwa na Serikali. Waziri Nape ametoa kauli hiyo tqrehe 18 Julai akiwa katika Kisiwa cha Lyakanyasi Ziwa Viktoria katika Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wanaouziwa vocha za sh 1,000 kwa sh 1200 na za sh. 500 kwa sh. 600. "Vocha ya 1,000 nunua kwa 1,000, vocha ya 500 nunua kwa 500 ukinunua kwa bei zaidi unalanguliwa, ni wizi na unatusumbua, kwa sababu muuza vocha ameingia mkataba na mwenye vocha kama kuna mahesabu ya kuongezeka wanajuana wao tunachotaka sisi mwananchi anunue vocha kwa bei iliyoandikwa kwenye vocha," amesema Waziri Nape. Amewaagiza wauza vocha kwenye kisiwa hicho kuacha mara moja ulanguzi huo kwani Serikali imepeleka mnara ili kuwasaidia wananchi visiwani huko.  "Nimepanda boti kuja hapa ku...

Wananchi 30,000 visiwa vitano wanufaika mawasiliano Sengerema

Mwandishi Wetu, WHMTH, Mwanza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imetoa ruzuku  ya Sh. Milioni 135, kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania zaidi ya 30,000 katika visiwa vitano vya Ziwa Viktoria vilivyoko Wilaya ya Sengerema kupata huduma za mawasiliano. Mnara huo uliojengwa katika Kisiwa cha Lyakanyasi Kijiji cha Chifunfu umelenga kutatua tatizo la kukosa mawasiliano hasa nyakati za majanga kama kuzama ziwani, kutekwa na kupata majanga mengine bila kupata msaada wa haraka kutokana na kukosekana kwa mawasiliano. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) wakati akizungumza na wanakijiji wa Kisiwa cha Lyakanyasi Kata ya Chifunfu akiwa katika siku ya nne ya ziara yake ya kukagua mradi ya ujenzi wa Mnara mikoa ya Kanda ya Ziwa.  "Mbali na wakazi wa visiwa vitano alivyovitaja Mbunge, mnara huu utawanufaisha watu zaidi ya 30,000, wa Kata ya Chifunfu Pia utawanufaisha wakazi 3,200 wa Kisiwa cha Chitandere na wapitaj...

Bil 2.2 kujenga minara 17 ya mawasiliano Geita

Picha
  Mwandishi Wetu - WHMTH, Geita  Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imetoa ruzuku ya Shilingi Bilioni 2.2 kwa ajili ya ujenzi wa minara 17 mkoani Geita kwenye mradi wa ujenzi wa minara 758 katika mikoa 26 ya Tanzania Bara. Waziri wa Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye, aliyenyoosha mkono, akizungumza na wananchi wa Geita baada ya kupokea taarifa ya hali ya mawasiliano kwa mkoa huo, wakati wa ziara yake ya kikazi leo Julai 17,2024. Ujenzi wa minara hiyo 17 utanufaisha kata 16, vijiji 27 huku wananchi 241,240 wanaoishi vijijini watanufaika na huduma ya mawasiliano mkoani humo. Hayo yamesemwa leo Julai 17, 2024 mjini Geita wakati Waziri wa Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (Mb), alipokuwa akipokea taarifa ya hali ya mawasiliano ya mkoa huo alipotembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Juni, 2024 tayari jumla ya minara 6 imewashwa mkoani humo na inatoa huduma ya mawasili...

Furaha ya Bibi na wajukuu; Rukwa inaruka kwa maendeleo

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan (Kulia) akifurahia jambo na wanafunzi waliohudhuria hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa,  hafla iliyofanyika  Kijiji cha Mtindilo Laela mkoani Rukwa leo Julai 17, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa kwenye hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Mtindilo, Laela mkoani humo leo Julai 17, 2024.

Wananchi ipeni thamani miradi ya minara- Waziri Nape

Picha
-Aitaka Vodacom kukopesha zaidi simu kwa wananchi Mwandishi Wetu, WHMTH, Kagera Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye(pichani), amewataka wananchi wa vijijini waliofikishiwa huduma za mawasiliano kuipa thamani miradi hiyo kwa kuitumia. Amesema wananchi wasipoitumia ipasavyo miradi hiyo, uwekezaji uliofanywa na Serikali kwa ku5shirikiana na Sekta binafsi hautakuwa na maana, huku  akiitaka Kampuni ya Vodacom kuongeza nguvu ya kukopesha wanavijiji simu, ili kuongeza idadi ya watumiaji wa huduma hizo.  Waziri Nape ametoa kauli hiyo leo Julia 16, 2024, baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa mnara wa mawasiliano katika Kijiji cha Kisharara, Kata ya Karambi wilayani Muleba, mkoani Kagera akiwa katika siku ya pili ya ziara yake kwenye Mikoa ya Kanda ya Ziwa. ""Wito wangu kwa wananchi watumie hizi huduma, kwa sababu kadri idadi yao inavyoongezeka inatusaidia kuona namna gharama zitakavyopungua, lakini pia tunaupa thamani mradi huu, fedha iliyolazwa hapa (zaid...

'Iwe' Kagera tumo, sh6.6 bil kujenga minara 45'

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Kagera Katika kuhakikisha mikoa iliyo pembezoni inaungwanishwa na Tanzania ya Kidigitali, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ((UCSAF), unatarajia kutumia takriban shilingi bilioni 6,6 kujenga minara 45 katika Kata 44 mkoani Kagera.  Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,  Nape  Nnauye  na watendaji wengine wa Mkoa wa Kagera, wakimsikiliza  Mtendaji Mkuu wa UCSAF,  Justina Mashiba  leo Julai 16,2024 wakati akitoa taarifa ya utendaji wa mfuko huo katika Mkoa wa Kagera. Mtendaji Mkuu wa UCSAF,  Justina Mashiba mebainisha hayo leo Julai 16, wakati akitoa taarifa ya utendaji wa mfuko huo katika Mkoa wa Kagera, mbele ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,  Nape  Nnauye katika siku ya pili ya ziara ya kikazi ya waziri huyo Mikoa ya Kanda ya Ziwa kukagua ujenzi wa Minara ya Mawasiliano ya Simu.  "Minara 45 ya Kagera ni sehemu ya minara 758 inayofadhiliwa na Serikali kwa kipindi cha miaka ...

Kigoma, minara ya mtandao 47, watu laki nane wanufaika

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Kigoma Takriban  Watanzania 866,352, wamenufaika na huduma bora za mawasiliano katika Mkoa wa Kigoma, kutokana na mradi wa minara ya simu 47 iliyojengwa na kuanza kutumika mkoani humo. Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Kigoma, wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na watendaji wa Mkufo wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Julai 15, 2024. Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba, amebainisha hayo Julai 15, 2024, wakati akitoa taarifa ya utendaji wa mfuko huo katika Mkoa wa Kigoma, mbele ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye. Mashiba amesema, minara hiyo imejengwa kwa teknolojia ya 2G, 3G na 4G, kwa ruzuku iliyotolewa na UCSAF, kwa makubaliano na watoa huduma, imegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 6.3. Ametaja wilaya zilizofaidika na minara hiyo pia minara iliyojengwa, kwenye mabano, kuwa ni Buhigwe (6), Kakonko (12), Kasulu DC (6), Mji wa Kasulu (5), Kibo...

TTCL, Vodacom zapewa 'siku 75' kukamilisha ujenzi minara ya mtandao

Picha
Mwandishi Wetu, WHMTH, Kigoma Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (pichani chini), ametoa siku 75, akizitaka kampuni za simu za Vodacom na TTCL kukamilisha ujenzi wa minara nane ya mawasiliano ya simu mkoani Kigoma. Nape amesema anataka kazi hiyo iwe imekamilika ifikapo Oktoba mwaka huu 2024, ambapo kimahesabu kutoka Julai 15, 2024 alipotoa agizo ni takriban siku 75, sawa na miezi miwili na nusu. Nape ametoa maagizo hayo leo Julai 15, 2024 wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Kigoma wakiwamo wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari, pamoja na watoa huduma za mawasiliano, baada ya kupokea taarifa ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) na Mamlaka ya Mawasiliano Tannzania (TCRA), kuhusu hali ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano na mradi wa ujenzi wa minara katika mkoa huo. "Vodacom mna minara minne ambayo bado hamjaanza kujenga, tukubaliane hadi kufikia Oktoba mwaka huu 2024 iwe im...

Mkurugenzi TASAF alivyopiga hodi Arumeru

Picha

Ni haki ya kila mwananchi kufaidi huduma ya mtandao-Nape

Picha
  -Minara 760 ya mawasiliano kukamilika 2025, Wananchi 8500 kunufaika Mwandishi Wetu,   daimatznews@gmail.com Jumla ya minara 758 ya mawasiliano inajengwa nchini ikitarajiwa kukamilika mwaka 2025 na kuwanufaisha w ananchi 8,512, 952 wa viji ji ni kwa kupata huduma ya mawasilino hasa mitandao, huku Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye akisema ni haki ya kila mwananchi kunufaika na huduma hizo.  Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye akisisitiza jambo, wakati wa mkutano wake na uongozi wa Mkoa wa Kigoma leo Julai 15, 2024. Kutekelezwa kwa mradi huo mkubwa kunafanyika katika mikoa 26 ya Tanzania Bara inayojumuisha wilaya 127, vijiji 1,407 vilivyo katika kata 713, kumebainishwa leo Julai 15, 2024 mkoani Kigoma, wakati Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akipokea taarifa za mawasiliano alipofanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani humo. Katika ziara yake mkoani humo, Nape amekagua ujenzi wa minara hiyo na...

Waziri Nape ziarani mikoa minne Kanda ya Ziwa

Picha
Pichani juu na chini, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa taasisi zilizo chini ya wizara yake, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kigoma Julai 14, 2024 tayari kuanza ziara ya siku tano katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Kigoma, Kagera, Mwanza, Geita na Shinyanga kwa ajili ya kukagua Miradi ya Ujenzi wa Minara ya Mawasiliano.