Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Papa Fransisko amuweka kando askofu

-Ni Joseph Strickland wa Marekani

Vatican,

Baba Mtakatifu Francisko, amemsimamisha Askofu Joseph Strickland(65), kutoa huduma ya Kichungaji ndani ya Kanisa Katoliki.

Kufuatia uamuzi huo, Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu Joe Vásquez, wa Austin, kuwa msimamizi wa kitume wa jimbo hilo. 

Papa Fransisko(kushoto), Askofu Strickland (kulia)

Kwa mujibu wa Vatican, Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani ametangaza uamuzi huo baada ya ziara ya kitume ya maaskofu, Juni 2023 katika Jimbo la Tyler.

Kadinali Daniel Nicholas Di Nardo, Askofu Mkuu wa Mji Mkuu wa Galveston-Houston, alitoa barua yake, iliyobainisha kwamba maaskofu waliofanya ziara hiyo, walikuwa ni Askofu Dennis Sullivan, wa Camden, na askofu mstaafu Gerald Kicanas, wa Tucson.

Amesema maaskofu hao walifanya uchunguzi wa kina katika nyanja zote za utawala na uongozi wa Jimbo la Tyler pamoja na Askofu Joseph Strickland.

"Baada ya miezi kadhaa, uamuzi umetolewa," amesema Kardinali Di Nardo.

Sehemu ya ripoti hiyo inaendelea kusomeka: “Kutokana na ziara hiyo, pendekezo lilitolewa kwa Baba Mtakatifu kwamba haiwezekani Askofu Strickland kuendelea tena na huduma ndani ya Kanisa Katoliki."

Ripoti ya ziara hiyo inaelezwa ilitoa miezi kadhaa ya tafakari kwa Baraza la Kipapa la Maaskofu na Baba Mtakatifu, ambapo amuzi ulifikiwa kumwomba Askofu Strickland ajiuzulu.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa Novemba 9, 2023 Askofu Strickland alitoa tamko akikataa kujiuzulu.

"Kwa hiyo ni uamuzi wa Papa  kumwondolea majukumu askofu huyo. Wakati tukingojea masharti maalum  zaidi kwa Jimbo la Tyler, tunamkumbuka Askofu Strickland katika sala zetu, pia tunawaombea mapadre na waamini wa Jimbo la Tyler na Askofu Vásquez," amesema Kardinali DiNardo.


Chapisha Maoni

0 Maoni