-Ni wa umri kuanzia mwaka mmoja
Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com
Wakati dunia leo imeungana kuadhimisha Siku ya Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kisukari, inayoadhimishwa Novemba 14 ya kila mwaka, bado yapo maswali kuhusu ugonjwa huo, moja likiwa: je watoto huugua kisukari?
Jibu la swali hilo kitaaluma ni ndiyo na kwamba ugonjwa huo umegawanyika katika makundi matatu.
Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Afya, Viashiria na Malaria, watoto wenye umri kati ya miezi sita hadi miezi 23, wapo hatarini kupata ugonjwa wa kisukari.
Hali hiyo inatajwa kusababishwa na kubadilika kwa mtindo wa maisha na malezi, lakini pia kurithi vinasaba kutoka kwa wazazi.
Ripoti hiyo ya mwaka 2022 iliyoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) nchini inaonyesha kuwa kundi hilo lipo katika hatari kupatwa na kisukari pamoja na kuongeza uzito uliopitiliza.
Aina tatu za Kisukari
Aina ya kwanza
Aina hii huwapata watoto kati ya mwaka mmoja na 24.
Watoto hupatwa na aina hii kutokana na tatizo la kongosho kutoa insulini kidogo au kukoma kutoa jimeng'enya hicho.
Dalili za mtoto kuugua aina ya kwanza ya kisukari ni pamoja na kuongezeka kwa kiu, kukojoa mara kwa mara, njaa, kupungua uzito ghafla na udhaifu.
Kisukari aina ya kwanza ni huanza wakati seli zinazotengeneza insulini (seli za beta) zinapoharibiwa kwa kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili.
Ikumbukwe kuwa Insulini ni homoni inayohitajika kwa seli kutumia sukari ya damu kwa ajili ya kuzalisha nishati, ikiwa na kazi ya kudhibiti kiwango cha sukari katika mzunguko wa damu.
Kwa aina hii ya kisukari, kuna dalili za ziada ambazo ni uoni hafifu, uchovu na majeraha kuchukua muda mrefu kupona.
Kisukari aina ya pili
Aina hii hjwapata watu wazima kati ya miaka 25 - 70 au zaidi, chanzo kikuu kikiwa mtindo mbaya wa maisha hasa ulaji na kutofanya mazoezi.
Hali hii husababisha mwili kushindwa kudhibiti na kuitumia sukari kama nishati hivyo kusababisha sukari nyingi kuzunguka kwenye damu.
Matokeo ya hali hiyo, viwango vya juu vya sukari kwenye damu inaweza kusababisha matatizo ya mfumo wa mzunguko, wa neva na wa kinga.
Kimsingi kisukari aina ya pili kina shida mbili, moja ni kongosho kushindwa kuzalisha insulini ya kutosha kuzalisha insulin na pili kuzalisha kimeng'enyo hicho kwa kiasi kikubwa.
Kisukari kwa Wajawazito
Hii ni aina ya tatu ya kisukari, ambapo wanawake hupatwa na kisukari, ambayo huwa juu kwenye damu.
Dalili za tatizo hili ni mjamzito kupatwa na kiu ya kupita kiasi, kukojoa mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi.
Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com
Wakati dunia leo imeungana kuadhimisha Siku ya Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kisukari, inayoadhimishwa Novemba 14 ya kila mwaka, bado yapo maswali kuhusu ugonjwa huo, moja likiwa: je watoto huugua kisukari?
Jibu la swali hilo kitaaluma ni ndiyo na kwamba ugonjwa huo umegawanyika katika makundi matatu.
Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Afya, Viashiria na Malaria, watoto wenye umri kati ya miezi sita hadi miezi 23, wapo hatarini kupata ugonjwa wa kisukari.
Hali hiyo inatajwa kusababishwa na kubadilika kwa mtindo wa maisha na malezi, lakini pia kurithi vinasaba kutoka kwa wazazi.
Ripoti hiyo ya mwaka 2022 iliyoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) nchini inaonyesha kuwa kundi hilo lipo katika hatari kupatwa na kisukari pamoja na kuongeza uzito uliopitiliza.
Aina tatu za Kisukari
Aina ya kwanza
Aina hii huwapata watoto kati ya mwaka mmoja na 24.
Watoto hupatwa na aina hii kutokana na tatizo la kongosho kutoa insulini kidogo au kukoma kutoa jimeng'enya hicho.
Dalili za mtoto kuugua aina ya kwanza ya kisukari ni pamoja na kuongezeka kwa kiu, kukojoa mara kwa mara, njaa, kupungua uzito ghafla na udhaifu.
Kisukari aina ya kwanza ni huanza wakati seli zinazotengeneza insulini (seli za beta) zinapoharibiwa kwa kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili.
Ikumbukwe kuwa Insulini ni homoni inayohitajika kwa seli kutumia sukari ya damu kwa ajili ya kuzalisha nishati, ikiwa na kazi ya kudhibiti kiwango cha sukari katika mzunguko wa damu.
Kwa aina hii ya kisukari, kuna dalili za ziada ambazo ni uoni hafifu, uchovu na majeraha kuchukua muda mrefu kupona.
Kisukari aina ya pili
Aina hii hjwapata watu wazima kati ya miaka 25 - 70 au zaidi, chanzo kikuu kikiwa mtindo mbaya wa maisha hasa ulaji na kutofanya mazoezi.
Hali hii husababisha mwili kushindwa kudhibiti na kuitumia sukari kama nishati hivyo kusababisha sukari nyingi kuzunguka kwenye damu.
Matokeo ya hali hiyo, viwango vya juu vya sukari kwenye damu inaweza kusababisha matatizo ya mfumo wa mzunguko, wa neva na wa kinga.
Kimsingi kisukari aina ya pili kina shida mbili, moja ni kongosho kushindwa kuzalisha insulini ya kutosha kuzalisha insulin na pili kuzalisha kimeng'enyo hicho kwa kiasi kikubwa.
Kisukari kwa Wajawazito
Hii ni aina ya tatu ya kisukari, ambapo wanawake hupatwa na kisukari, ambayo huwa juu kwenye damu.
Dalili za tatizo hili ni mjamzito kupatwa na kiu ya kupita kiasi, kukojoa mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi.
0 Maoni