Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Hatari yako, majibu ya kisukari

 Mwandishi Wetu

Novemba 14 kila mwaka kama kesho, ulimwengu wa wadau wa afya huadhimisha Siku ya Ugonjwa wa Kisukari Duniani, ambao ni miongoni mwa magonjwa yasiyoambukiza unaosumbua watu wengi zaidi duniani.

Kutokana na ukweli huo, kila binadamu yupo katika hatari ya kupatwa na ugonjwa huo, lakini pengine kuwa na maswali kuhusu kisukari.

Kwa mwaka huu 2023,  maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa mkoani Dar es Salaam, huku katika mikoa yote nchini ikiadhimishwa kwa wananchi kupata fursa ya kupima na kujua hali zao kuhusu kisukari.

Mkoani Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja pia wananchi wanapewa fursa ya kupima bure baadhi ya magonjwa yasiyoambukiza kuanzia tarehe 14  hadi 18/11/2023.

Maadhimisho hayo yanafanyika yakiongozwa na kauli mbiu isemayo: "IJUE HATARI YAKO, FAHAMU MAJIBU YAKO".

Wakati hayo yakiendelea, kwa niaba ya Shirikisho la Magonjwa Yasiyoambukiza nchini (TANCDA), ifuatayo ni makala fupi inayoeleza hatari na majibu kuhusu kisukari, ambao wataalam wanaeleza upo katika makundi matatu, ambayo ni: Kisukari aina ya Kwanza, Kisukari aina na Pili na Kisukari kwa Wajawazito.

Ni kweli kwamba huenda ni mimi au wewe au ndugu na jamaa zetu wapo kwenye dalili za kupata ugonjwa wa kisukari au tuunaishi au wanaishi na ugonjwa wa kisukari. 

Ni jukumu la kila mmoja wetu kujua hatari ya ugonjwa huu wa kisukari na kuchukua taadhari.

Baadhi ya visababishi vya ugonjwa wa kisukari ni pamoja na ukosefu wa mazoezi na ushugulishaji mwili, matumizi ya sukari nyingi kwenye vyakula na vyinjwaji na unjwaji wa pombe uliopitiliza na uvutaji wa tumbaku na bidhaa zake.

Dalili za Ugonjwa wa Kisukari.

Kukojoa mara kwa mara, kuhisi kiu mara kwa mara, kuhisi njaa kila wakati, kupoteza uzito. Uoni hafifu, uchovu, na uponyaji wa polepole wa jeraha. 

Jinsi ya Kujikinga na Ugonjwa wa Kisukari.

Fanya mazoezi angalau dakika 30 kwa siku mara 5 kwa wiki.

Epuka matumizi ya sukari iliyopitiliza kwenye chakula na vinjwaji.

Epuka unjwaji wa pombe uliopitiliza.

Epuka uvutaji wa tumbaku na bidhaa zake.

Chapisha Maoni

0 Maoni