Msajili Hazina kuwa Mfuko wa Uwekezaji

-Lengo kuongeza tija -Yasiyo faida kuchukuliwa hatua Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Msajili wa Hazina (TR), Nehemiah Mchechu amesema, Ofisi yake ipo mbioni kufanyiwa marekebisho kisheria na kuwa Mfuko wa Uwekezaji wa Umma (PIA) , lengo likiwa kuongeza tija kwenye Taasisi za Umma inazozisimamia. Amesema kutokana na mabadiliko hayo, taasisi hizo zinapaswa kuzalisha kwa ajili kugharamia mipango binafsi iliyonayo na ile ya Serikali, akionya kwamba mashirika yasiyofanya vizuri itabidi yachukuliwe hatua. Mchechu amebainisha hayo leo Novemba 28, 2023, katika Kikao Kazi na Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini, jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Msajili huyo wa Hazina, ma tarajio ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni kuona taasisi hasa za kibiashara, zinazalisha faida na kuingizwa Serikalini au kujiendesha bila kutegemea Serikali Kuu. "Kwa hali hiyo ni lazima kuwepo mabadiliko, ili kuziongezea tija na ufanisi taasisi hizo" amesema Mche...