Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2023

Msajili Hazina kuwa Mfuko wa Uwekezaji

Picha
 -Lengo kuongeza tija -Yasiyo faida kuchukuliwa hatua   Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Msajili wa Hazina (TR),  Nehemiah Mchechu amesema, Ofisi yake ipo mbioni kufanyiwa marekebisho kisheria na kuwa Mfuko wa Uwekezaji wa Umma  (PIA) , lengo likiwa kuongeza tija kwenye   Taasisi za Umma inazozisimamia. Amesema kutokana na mabadiliko hayo,  taasisi hizo zinapaswa kuzalisha kwa ajili kugharamia mipango binafsi iliyonayo na ile ya Serikali, akionya kwamba mashirika yasiyofanya vizuri itabidi yachukuliwe hatua.  Mchechu amebainisha hayo leo Novemba 28, 2023, katika Kikao Kazi na Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini, jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Msajili huyo wa Hazina, ma tarajio ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni kuona taasisi hasa  za kibiashara, zinazalisha faida na kuingizwa Serikalini au kujiendesha bila kutegemea Serikali Kuu. "Kwa hali hiyo ni lazima kuwepo mabadiliko, ili kuziongezea tija na ufanisi taasisi hizo" amesema Mche...

Katibu Mkuu Chongolo yupo, hayupo?

Picha
Mwandishi Wetu , daimatznews@gmail.com Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amefungua semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana akifungua semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam.   Wakati Kinana akifungua semina hiyo, kitendawili kinabaki ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Daniel Chongolo yupo au hayupo kwenye nafasi yake, kufuatia kuenea kwa taarifa kwamba ameandika barua ya kujiuzulu. Tayari, barua inayodaiwa kuandikwa na Chongolo jana Novemba 27, 2023 kwenda kwa mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, imeonekana kwenye mitandao ya kijamii. Hata hivyo, CCM bado ipo kimya kuhusu taarifa hizo, hata Kinana hakueleza chochote kuhusu mtendaji huyo mkuu wa Sekretarieti wakati akifungua semina hiyo, aliyoielezea kwamba itawafundisha mada tofauti kuhusu uongozi, maadili na uwajibik...

Wasanii 10 wenye 'maokoto' zaidi Afrika Mashariki 2023

Picha
-Diamond, Harmonize, Kiba watajwa -Profesa Jay, Lady Jay Dee waibuka, Tanzania ikizoa nafasi tano, Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Waswahili husema, biashara asubuhi, jioni ni mahesabu. Usemi huu unaweza kuulinganisha na matokeo ya kufunga mwaka ya viwango vya maokoto kwa wasanii wa muziki Afrika Mashariki katika mwaka 2023 unaoishia, yakibainisha wasanii kumi bora, huku Mtanzania Diamond Platnumz, akitajwa kushika nafasi ya pili. Katika matokeo hayo yaliyotolewa na Jarida maarufu la Forbes, leo Novemba 27, mwaka 2023, pamoja na Diamond Plutnumz, wametajwa pia wengine wanne, wakiwemo wakongwe Professor Jay   na Lady Jay Dee kuwa miongoni mwa wasanii wanaoongoza kwa utajiri Afrika Mashariki kwa mwaka 2023. Msanii Diamond Platnumz (Picha zote kwa hisani ya Mtandao) Diamond ametajwa na jarida hilo kushika nafasi ya pili kwa utajiri Afrika Mashariki katika mwaka 2023, kwa kumiliki ukwasi unaofikia Dola za Marekani milioni 9.1. Fedha hizo ni sawa na takriban shilingi bil...

Ruto Rais tajiri zaidi Afrika Mashariki 2023

Picha
 -Yumo kati ya 10 matajiri zadi Afrika -Awaacha mbali King Mswati, Ramaphosa -Kagame amfuatia Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com Wakati zimesalia takriban siku 34 kuumaliza mwaka 2023, sawa na mwezi mmoja na siku tatu, orodha ya marais 10 wanaoongoza kwa utajiri barani Afrika imewekwa hadharani, ikimtaja Rais William Ruto wa Kenya kuwa kinara wa utajiri ukanda wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2023. Orodha hiyo imechapwa na Jarida la Forbes mtandaoni leo tarehe 27 Novemba 2023, likimtaja Ruto kumiliki utajiri unaofikia Dola za Marekani   milioni 510, sawa na takriban shilingi trilioni 1.22. Rais William Ruto wa Kenya (Kushoto), akisalimiana na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Nairobi wakati Dk Samia alipofanya ziara nchini Kenya mapema Juni mwaka huu 2023. Kutokana na utajiri huo, jarida hilo limemtaja Ruto kushika nafasi ya nne kati ya marais kumi matajiri zaidi Afrika katika mwaka 2023. Katika orodha hiyo, Rais Paul Kagame wa Rwanda anatajwa kushika nafasi ya sita...

Kumbe watoto huugua kisukari

-Ni wa umri kuanzia mwaka mmoja Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Wakati dunia leo imeungana kuadhimisha Siku ya Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kisukari, inayoadhimishwa Novemba 14 ya kila mwaka, bado yapo maswali kuhusu ugonjwa huo, moja likiwa: je watoto huugua kisukari? Jibu la swali hilo kitaaluma ni ndiyo na kwamba ugonjwa huo umegawanyika katika makundi matatu. Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Afya, Viashiria na Malaria, watoto wenye umri kati ya miezi sita hadi miezi 23, wapo hatarini kupata ugonjwa wa kisukari. Hali hiyo inatajwa kusababishwa na kubadilika kwa mtindo wa maisha na malezi, lakini pia kurithi vinasaba kutoka kwa wazazi. Ripoti hiyo ya mwaka 2022 iliyoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) nchini inaonyesha kuwa kundi hilo lipo katika hatari kupatwa na kisukari pamoja na kuongeza uzito uliopitiliza. Aina tatu za Kisukari Aina ya   kwanza Aina hii huwapata watoto kati ya mwaka mmoja na 24. Watoto hupatwa na aina hii kutok...

Papa Fransisko amuweka kando askofu

Picha
-Ni Joseph Strickland wa Marekani Vatican, Baba Mtakatifu Francisko, amemsimamisha Askofu Joseph Strickland(65), kutoa huduma ya Kichungaji ndani ya Kanisa Katoliki. Kufuatia uamuzi huo, Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu Joe VĆ”squez, wa Austin, kuwa msimamizi wa kitume wa jimbo hilo.  Papa Fransisko(kushoto), Askofu Strickland (kulia) Kwa mujibu wa Vatican, Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani ametangaza uamuzi huo baada ya ziara ya kitume ya maaskofu, Juni 2023 katika Jimbo la Tyler. Kadinali Daniel Nicholas Di Nardo, Askofu Mkuu wa Mji Mkuu wa Galveston-Houston, alitoa barua yake, iliyobainisha kwamba maaskofu waliofanya ziara hiyo, walikuwa ni Askofu Dennis Sullivan, wa Camden, na askofu mstaafu Gerald Kicanas, wa Tucson. Amesema maaskofu hao walifanya uchunguzi wa kina katika nyanja zote za utawala na uongozi wa Jimbo la Tyler pamoja na Askofu Joseph Strickland. "Baada ya miezi kadhaa, uamuzi umetolewa," amesema Kardinali Di Nardo. Sehemu ya ripoti hiyo inaende...

Hatari yako, majibu ya kisukari

 Mwandishi Wetu Novemba 14 kila mwaka kama kesho, ulimwengu wa wadau wa afya huadhimisha Siku ya Ugonjwa wa Kisukari Duniani, ambao ni miongoni mwa magonjwa yasiyoambukiza unaosumbua watu wengi zaidi duniani. Kutokana na ukweli huo, kila binadamu yupo katika hatari ya kupatwa na ugonjwa huo, lakini pengine kuwa na maswali kuhusu kisukari. Kwa mwaka huu 2023,  maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa mkoani Dar es Salaam, huku katika mikoa yote nchini ikiadhimishwa kwa wananchi kupata fursa ya kupima na kujua hali zao kuhusu kisukari. Mkoani Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja pia wananchi wanapewa fursa ya kupima bure baadhi ya magonjwa yasiyoambukiza kuanzia tarehe 14  hadi 18/11/2023. Maadhimisho hayo yanafanyika yakiongozwa na kauli mbiu isemayo: "IJUE HATARI YAKO, FAHAMU MAJIBU YAKO". Wakati hayo yakiendelea, kwa niaba ya Shirikisho la Magonjwa Yasiyoambukiza nchini (TANCDA), ifuatayo ni makala fupi inayoeleza hatari na majibu kuhusu kisukari, ambao wataalam wana...

Mtindo bora wa maisha huu hapa

Picha
 -TANCDA yataka watu wajifunze kubadilik- -Magonjwa yasiyoambukiza huchangia asilimia 33 ya vifo  Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani, kuadhimisha Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza,(WMY), ambayo hufanyika Novemba ya kila mwaka, kuanzia tarehe 11 hadi 17. Kwa mwaka huu kitaifa wiki hiyo inafanyika mkoani Dar es Salaam, huku magonjwa hayo yasiyoambukiza yakitajwa kuchangia zaidi ya asilimia 70 ya vifo vya mapema duniani. Kwa mujibu wa Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyoambukiza (TANCDA), katika kila vifo vitatu, kimoja kinasababishwa na Magonywa Yasiyoambukiza (MY), huku yakitajwa kusababisha asilimia 33 ya vifo hapa nchini. Hata hivyo, wataalam wa afya wanaeleza kuwa Mtindo Bora wa Maisha ndiyo suluhu ya kuepuka magonjwa yasiyoambukiza. Mwenyekiti wa TANCDA, Profesa Andrew Swai, pichani juu, ameeleza kuwa sababu kubwa za magonjwa hayo ni mtindo mbaya wa maisha katika ulaji na kutofanya mazoezi, zikiwamo pia vinasaba vya kurithi. Pro...

Takukuru yakunjua makucha Kigoma

Picha
-Wakandarasi ' watemeshwa bungo'  Mwandishi Wetu,Kigoma Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa Mkoa wa Kigoma (TAKUKURU) imebaini upungufu mkubwa katika miradi 33 yenye thamani ya shiligi bilioni 12.5, iliyoifuatilia, ikionyesha kuwa chini ya kiwango. Kufuatia uchunguzi huo, wazabuni wawili waliobanwa na Takukuru, mmoja amerudisha fedha zadi ya shilingi milioni 125 na mwingine kuwasilisha mabati mapya kwenye mradi. Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma Mkoa Kigoma, Leonida Mushama amesema hayo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji ya taasisi Takukuru mkoani humo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Septemba mwaka huu. Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma Mkoa Kigoma, Leonida Mushama akiwasilisha taarifa ya Takukuru mkoani humo. Alitoa taarifa hiyo kwa niaba ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa Kigoma, Stephen Mafipa. Mushama amesema kuwa katika miradi hiyo pia ipo miradi ya ujenzi wa madarasa inayotekelezwa kwa mpango wa BOOST, yenye thamani ya takriban shilingi bilioni tatu. Amesema Takuk...

Wafanyabiashara Kisarawe 'walilia' TRA

Mwandishi Wetu, Kisarawe  WAFANYABISHARA wilayani Kisarawe Mkoa wa Pwani, wameiomba Mamlaka ya Mapato (TRA), kuwapa elimu ya kutosha kuhusu ulipaji kodi kwa hiari na matumizi ya mashine za EFD. Ombi hilo limetolewa na wafanyabishara wilayani humo, wakati wa mkutano wao na viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabishara (JWT), wakiongozwa na Mwenyekiti wake Hamis Livembe, wakiwa kwenye ziara ya kikazi ya kusikiliza kero mkoani humo. Mfanyabishara Christina Mulu, amesema TRA wanatakiwa kuwapa elimu ya kutosha kuhusu ulipaji kodi badala ya kukazania kukusanya bila kuwasikiliza wafanyabishara kwanza. "Wafanyabiashara wengi hatuna elimu ya kodi, matumizi ya EFD hatujui wakati mwingine risiti zinagoma kutoka na mashine kusumbua sasa TRA wakija wao ni kutaka tu kutoza faini badala ya kutupa elimu kwanza," amesema Mulu. Mfanyabishara John Masine, amewataka TRA kuwasaidia wafanyabishara urahisi wa kupata kodi na kuwalinda kwa kuondoa wamachinga mbele ya fremu za biashara. "Mfanyabishara am...

Waziri Mkuu akemea wathamini wababaishaji

Picha
 -Awataka kushirikiana na wathaminj binafsi kuchochea maendeleo Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekemea tabia ya baadhi ya wathamini wanaokiuka miiko ya kazi hiyo akiwataka kuwa waadilifu, weledi na wazingatie miiko ya taaluma kwenye kazi zao za kila siku. Majaliwa ametoa karipio hilo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Mwaka wa Wathamini unaofanyika kwa siku mbili, jijini Dodoma ambapo ameeleza kuwa wathamini ni watu muhimu katika kufanikisha mipango ya maendeleo ya Taifa. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua mkutano mkuu wa Watahamini, jijini Dodoma, Novemba 10, 2023.  ā€œKazi ya uthamini si ya wababaishaji au vishoka, kila mthamini hana budi kuthamini na kuheshimu taaluma yake, ninyi mnapaswa kuwa waadilifu na kuzingatia thamani halisi ya ardhi, jengo au chochote kinachofanyiwa uthamini,ā€ amesema Waziri Mkuu na kuongeza:  ā€œKuna baadhi ya wathamini  si waadilifu na kwa kushirikiana na watendaji wengine, hutoa makadirio yasiyowiana...

Rais Dk.Samia atimua Bodi, afanya uteuzi

Picha

Bilionea Rostam Aziz aigeukia Zambia

Picha
  -Amwaga mabilioni ya fedha Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Bilionea Mtanzania, Rostam Aziz ametangaza kutanua uwekezaji wake kwa kufanya uwekezaji mpya, safari hii akiwekeza nchini Zambia kiasi cha Dola za Marekani milioni 100 katika sekta ya nishati na madini. Rostam ambaye pia ni Mwenyekiti wa kampuni za Taifa Group inayofanya kazi ukanda wa Afrika Mashariki amefanya uamuzi wa kuwekeza fedha hizo, sawa na takriban shilingi bilioni 250, unaoashiria kuwa na mkakati wa kupanua zaidi wigo wa uwekezaji wake kwenye ukanda wa kusini mwa Afrika. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan(kushoto) akishuhudia Mfanyabiashara Rostam Aziz, akitia saini moja ya mikataba ya kibiashara katika moja ya ziara za Rais nje ya nchi. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na Mtandao wa billionaires.africa za hivi karibuni, Rostam   anayetajwa kumiliki utajiri mkubwa barani Afrika, tayari amekutana na Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema, Oktoba 20 mwaka huu 2023, ambapo walijadili kuhusu maeneo yeny...

JOWUTA yawasilisha maoni Kamati ya Nape

Picha
-Wataka waandishi waungane kudai na kulinda maslahi Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA), kimekabidhi maoni yake kuhusu hali ya uchumi kwa vyombo vya habari na wanahabari mbele ya Kamati ya Kupokea Maoni Kuhusu Hali ya Uchumi wa Vyombo vya Habari Tanzania. Ikiwakilishwa na Katibu Mkuu wake, Suleiman Msuya, aliyeongozana na Naibu wake, Said Mmanga na Mjumbe wa Bodi ya chama hicho, Careen Tausi Mbowe, JOWUTA ilikabidhi maoni yake leo Novemba 7, 2023 kwa  Mjumbe wa Kamati ya Kupokea Maoni Kuhusu Hali ya Uchumi kwa Vyombo vya Habari na Waandishi, Sebastian Maganga.    Katibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA), Suleiman Msuya akikabidhi maoni ya chama hicho kwa Mjumbe wa Kamati ya Kupokea Maoni Kuhusu Hali ya Uchumi kwa Vyombo vya Habari na Waandishi, Sebastian Maganga. Wengine pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa JOWUTA, Said Mmanga(Kushoto) na Mjumbe wa Bodi ya JOWUTA, Careen Tausi ...

Mazingira: Serikali kujenga ukuta fukwe za Nungwi

Picha
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Khamis Hamza Khamis akijibu maswali bungeni Dodoma kuhusu wizara yake.   .

JWT yaanza ziara kusikiliza kero za wafanyabishara Pwani

Picha
Mwandishi Wetu, Pwani JUMUIYA ya Wafanyabiasha nchini (JWT) imeanza ziara ya kikazi ya kusikiliza kero za wafanyabishara katika wilaya zote za Mkoa wa Pwani. Lengo la ziara hiyo ni kusikiliza kero za wafanyabishara, wenye viwanda na kampuni ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu na kuepuka changamoto ikiwamo migomo ya mara kwa mara. Mwenyekiti wa JWT, Hamis Livembe, akiongozana na viongozi wengine mapema leo wamewasili ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani na kufanya mazunguzo na Katibu Tawala, Rashid Mchatta kabla ya kuanza mikutano yao. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Rashid Mchatta, (katikati)akizungumza na ujumbe wa JWT walipomtembelea ofisini kwake, kabla ya ziara yao mkoani humo. Livembe amesema, Rais Samia anawapenda wafanyabishara ndio sababu amewaagiza wasikilize kero zao ili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. Amesema wafanyabishara wakiungana wanaweza kujisemea na kumaliza kero zao bila kufunga biashara wala kufanya vurugu hivyo ni muhimu kujitokeza kwenye mikutano hiyo. Naye Mchatta ameipon...

DRC yampeleka Angola Rais Dk. Samia kwa dharura

Picha