Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Waziri Mkuu akemea wathamini wababaishaji

 -Awataka kushirikiana na wathaminj binafsi kuchochea maendeleo


Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekemea tabia ya baadhi ya wathamini wanaokiuka miiko ya kazi hiyo akiwataka kuwa waadilifu, weledi na wazingatie miiko ya taaluma kwenye kazi zao za kila siku.

Majaliwa ametoa karipio hilo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Mwaka wa Wathamini unaofanyika kwa siku mbili, jijini Dodoma ambapo ameeleza kuwa wathamini ni watu muhimu katika kufanikisha mipango ya maendeleo ya Taifa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua mkutano mkuu wa Watahamini, jijini Dodoma, Novemba 10, 2023.

 “Kazi ya uthamini si ya wababaishaji au vishoka, kila mthamini hana budi kuthamini na kuheshimu taaluma yake, ninyi mnapaswa kuwa waadilifu na kuzingatia thamani halisi ya ardhi, jengo au chochote kinachofanyiwa uthamini,” amesema Waziri Mkuu na kuongeza: 

“Kuna baadhi ya wathamini  si waadilifu na kwa kushirikiana na watendaji wengine, hutoa makadirio yasiyowiana na thamani halisi, hivyo kusababisha kupoteza mapato ya Serikali, lakini pia kuwanyima haki wanaostahili kupata haki." 

Amewataka pia wathamini hao kutumia mkutano huo kufanya majadiliano ya kina kuhusu masuala ya taratibu za utwaaji ardhi na sheria zake, ukokotozi wa fidia katika maeneo ya madini, viwango vya thamani ya ardhi na mazao, changamoto za kisera za utwaaji ardhi pamoja na kupata suluhu ya malalamiko ya wananchi.

Badhi ya Watahamini, wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mkutano wao mkuu, jijini Dodoma, Novemba 10,2023


Waziri Mkuu Majaliwa, pia amewataka watendaji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi hasa wathamini kushirikiana na sekta binafsi katika kufanya kazi zao za uthamini.

 “Tumieni fursa ya uwepo wa wathamini binafsi ili kutoa huduma bora na kwa haraka, mkifanya hivyo mtakuwa mnatekeleza maagizo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ya ushirikishaji wa sekta binafsi kwa maendeleo ya Taifa,” amesema Majaliwa. 


Chapisha Maoni

0 Maoni