-Diamond, Harmonize, Kiba watajwa
-Profesa Jay, Lady Jay Dee
waibuka, Tanzania ikizoa nafasi tano,
Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Waswahili husema, biashara asubuhi, jioni ni mahesabu. Usemi
huu unaweza kuulinganisha na matokeo ya kufunga mwaka ya viwango vya maokoto
kwa wasanii wa muziki Afrika Mashariki katika mwaka 2023 unaoishia,
yakibainisha wasanii kumi bora, huku Mtanzania Diamond Platnumz, akitajwa kushika
nafasi ya pili.
Katika matokeo hayo yaliyotolewa na Jarida maarufu la Forbes, leo Novemba 27, mwaka 2023, pamoja na Diamond Plutnumz, wametajwa pia wengine wanne,
wakiwemo wakongwe Professor Jay na Lady
Jay Dee kuwa miongoni mwa wasanii wanaoongoza kwa utajiri Afrika Mashariki
kwa mwaka 2023.
![]() |
Msanii Diamond Platnumz (Picha zote kwa hisani ya Mtandao) |
Diamond ametajwa na jarida hilo kushika nafasi ya pili kwa
utajiri Afrika Mashariki katika mwaka 2023, kwa kumiliki ukwasi unaofikia Dola
za Marekani milioni 9.1. Fedha hizo ni sawa na takriban shilingi bilioni 21.84,
akiongoza pia kwa utajiri mbele ya Wasanii wengine wa Tanzania waliotajwa kwenye orodha hiyo.
Matokeo hayo yaliyotajwa kuhusisha pia mtandao wa Ugwire.com, yamemtaja Diamond Plutnumz kuwa ndiye msanii anayetafutwa na kufuatiliwa zaidi kupitia mtandao wa Google, kuwa na wafuasi wengi zaidi, akiwa pia maarufu zaidi kwenye ukanda huo.
Diamond anatanguliwa na Msanii Bobi Wine wa Uganda, ambaye pia ni mwanasiasa na kiongozi wa upinzani nchini Uganda, aliyewahi kumtikisa Rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni wakati alipowania urais nchini humo uchaguzi uliopita mwaka 2021.
![]() |
Msanii Bobi Wine |
Wine anamiliki utajiri unaofikia Dola 9.2 (shilingi bilioni
22.08), akimzidi Diamond kwa takriban shilini milioni 240 pekee.
Katika orodha hiyo, anayeshika nafasi ya tatu ni Mwimbaji
Akothee wa Kenya anayetajwa kuwa na utajiri unaofikia Dola milioni 9, sawa na
wastani wa shilingi bilioni 21.60, huku wa nne akiwa Jose Chameleon wa Uganda
ambaye kwa mwaka 2023 ametajwa kumiliki utajiri wa Dola milioni 8 (shilingi
bilioni 19.2).
![]() |
Msanii Professor Jay |
Wasanii wengine wa Tanzania waliotajwa na Forbes ni pamoja na Profesa Jay anayeelezwa kusika nafasi ya tano, ambapo anamiliki utajiri unaofikia Dola milioni 7.5 kwa mwaka huu, ambazo ni sawa na takriban shilingi bilioni 18.
Profesa Jay, amefuatiwa na
Msanii Ali Kiba aliyeshika nafasi ya sita, ambaye kwa mujibu wa Forbes,
hadi leo Novemba 27, mwaka 2023 ana utajiri wenye thamani ya Dola milioni 7.2,
sawa na takriban shilingi bilioni 17.28.
![]() |
Msanii Ali Kiba |
Nafasi ya saba katika orodha hiyo amewekwa Msanii Jaguar kutoka Kenya, anayetajwa kuwa na ukwasi wenye thamani ya Dola milioni 6.9, takriban shilingi bilioni 16.56 na nafasi ya nane pia imeshikwa na Saut Sol wa nchini humo, wenye umiliki wa Dola milioni 6.8(shilingi bilioni 16.32)
Jarida hilo la Forbes, limemtaja Mtanzania mwingine, Harmonize
kushika nafasi ya tisa kwa utajiri Afrika Mashariki katika mwaka huu wa 2023,
akimiliki ukwasi wenye thamani ya Dola milioni 6.6 ambazo zikibadilishwa kwa
fedha za kitanzania, zitakuwa sawa na takriban shilingi bilioni 15.84.
![]() |
Msanii Harmonize |
Msanii Lady Jay Dee, maarufu kama Binti Machozi au Komando ndiye aliyefunga ndimba la wasanii 10 matajiri zaidi Afrika Masharikikwa mwaka 2023, akielezwa kumiliki utajiri unaofikia Dola 6.5 ambazo ni sawa na takriban shilingi bilioni 15.60.
Lady Jay Dee ndiye msanii pekee wa kike aliyeingia kwenye
orodha hiyo, akiwa pia miongoni mwa wasanii wakongwe wa muziki wa kizazi kipya
hapa nchini.
![]() |
Msanii Lady Jay Dee |
0 Maoni