Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amefungua semina ya mafunzo kwa
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam.
![]() |
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana akifungua semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam. |
Tayari, barua inayodaiwa
kuandikwa na Chongolo jana Novemba 27, 2023 kwenda kwa mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dk.
Samia Suluhu Hassan, imeonekana kwenye mitandao ya kijamii.
Iwapo taarifa
hizo za kujiuzulu Chongolo ni za kweli, CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Dk.
Samia Suluhu Hassan, itakuwa na kibarua cha kumteua Katibu Mkuu mpya wa chama
hicho tawala na kikongwe barani Afrika.
Wakati hayo yakiendelea, majina ya makada mbalimbali wa CCM yanatajwa kwamba huenda mmoja akarithi mikoba ya Chongolo.
Baadhi ya wanaotajwa
ni Balozi Dk.Emmanuel Nchimbi, Ali Happy, Abdallah Bulembo na Amos Makala.
0 Maoni