Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Katibu Mkuu Chongolo yupo, hayupo?

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amefungua semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana akifungua semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam. 


Wakati Kinana akifungua semina hiyo, kitendawili kinabaki ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Daniel Chongolo yupo au hayupo kwenye nafasi yake, kufuatia kuenea kwa taarifa kwamba ameandika barua ya kujiuzulu.

Tayari, barua inayodaiwa kuandikwa na Chongolo jana Novemba 27, 2023 kwenda kwa mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, imeonekana kwenye mitandao ya kijamii.

Hata hivyo, CCM bado ipo kimya kuhusu taarifa hizo, hata Kinana hakueleza chochote kuhusu mtendaji huyo mkuu wa Sekretarieti wakati akifungua semina hiyo, aliyoielezea kwamba itawafundisha mada tofauti kuhusu uongozi, maadili na uwajibikaji kwa chama na Serikali.

Iwapo taarifa hizo za kujiuzulu Chongolo ni za kweli, CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, itakuwa na kibarua cha kumteua Katibu Mkuu mpya wa chama hicho tawala na kikongwe barani Afrika.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa(wa pili kulia), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla(wa tatu) na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dotto Biteko (wa nne) na wajumbe wengine, wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, leo Novemba 28 jijini Dar es Salaam.


Wakati hayo yakiendelea, majina ya makada mbalimbali wa CCM yanatajwa kwamba huenda mmoja akarithi mikoba ya Chongolo.

Baadhi ya wanaotajwa ni Balozi Dk.Emmanuel Nchimbi, Ali Happy, Abdallah Bulembo na Amos Makala.



Chapisha Maoni

0 Maoni