-TANCDA yataka watu wajifunze kubadilik-
-Magonjwa yasiyoambukiza huchangia asilimia 33 ya vifo
Mwandishi Wetu, daimatz@gmail.com
Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani, kuadhimisha Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza,(WMY), ambayo hufanyika Novemba ya kila mwaka, kuanzia tarehe 11 hadi 17.
Kwa mwaka huu kitaifa wiki hiyo inafanyika mkoani Dar es Salaam, huku magonjwa hayo yasiyoambukiza yakitajwa kuchangia zaidi ya asilimia 70 ya vifo vya mapema duniani.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyoambukiza (TANCDA), katika kila vifo vitatu, kimoja kinasababishwa na Magonywa Yasiyoambukiza (MY), huku yakitajwa kusababisha asilimia 33 ya vifo hapa nchini.
Hata hivyo, wataalam wa afya wanaeleza kuwa Mtindo Bora wa Maisha ndiyo suluhu ya kuepuka magonjwa yasiyoambukiza.
Mwenyekiti wa TANCDA, Profesa Andrew Swai, pichani juu, ameeleza kuwa sababu kubwa za magonjwa hayo ni mtindo mbaya wa maisha katika ulaji na kutofanya mazoezi, zikiwamo pia vinasaba vya kurithi.
Profesa Swai amesema kuwa kutokana na hali hiyo TANCDA wameandaa kitabu cha elimu kuhusu Magonjwa Yasiyoambukiza kinachotolewa bure pia kupatikana mtandaoni.
"Tunataka watu wapate elimu hii bure, wajifunze na kubadilika ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza, madhara yake na vifo," amesema Profesa Swai.
Ili kupata elimu zaidi fuatilia ukurasa huu, utapata bure nakala mtandao ya kitabu hicho au bofya:
0 Maoni