ZIARA YA WAZIRI DK. AKWILAPO NHC, TASWIRA CHANYA YA MAKAZI BORA
Katika hotuba yake kwa menejimenti na watumishi wa NHC, Dk. Akwilapo ametoa maelekezo ya wazi na yenye mwelekeo wa muda mrefu, akisisitiza umuhimu wa utafiti wa kina katika kubuni na kutekeleza miradi ya makazi.
Ameielekeza NHC kufanya tafiti zitakazowezesha ujenzi wa nyumba bora na za gharama nafuu, hususan kwa wananchi wa kipato cha chini na cha kawaida.
Kwa msisitizo, Waziri ameeleza kuwa unafuu wa gharama, lazima ueleweke kwa kuzingatia makundi tofauti ya Watanzania, hali zao za kiuchumi na mahitaji yao halisi.
Maelekezo hayo yameenda sambamba na wito wa kutumia teknolojia za kisasa na bunifu katika sekta ya ujenzi.

Maoni
Chapisha Maoni