Miradi ya NHC Kijichi, Kawe 711, Kariakoo nguzo 3 za kipekee Dar

-Kitovu cha mapato NHC, maisha bora kwa wananchi

-Mwanzo mpya wa makazi ya kisasa Dar

-Usanifu unaoendana na Dira ya Taifa ya 2050

-Ubia sekta binafsi, ubunifu wa NHC vyafungua milango fursa mpya kiuchumi, kijamii

Mwandishi Wetu, daimatznews@gmail.com

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeendelea kuthibitisha nafasi yake kama mhimili wa mageuzi ya sekta ya makazi nchini. Kupitia miradi mikubwa ya kisasa maeneo mbalimbali nchini, NHC inaonyesha dhamira yake ya kuunga mkono ajenda ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora, salama na endelevu.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah
Katika Jiji la Dar es Salam, NHC kupitia miradi ya Samia Housing Scheme Kijichi, Kawe 711 na Mradi wa Ubia wa Kariakoo, imeleta sura mpya katika jiji hilo kupitia ujenzi wa nyumba za kisasa, matumizi ya teknolojia ya gharama nafuu na ushirikiano mkubwa na sekta binafsi, ili kuongeza kasi ya upatikanaji wa makazi ya kudumu ikibeba sifa za kipekee.


Mradi huu wa Samia Housing Scheme Kijichi unaendelea kwa kasi na ubora wa hali ya juu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuongeza wigo wa makazi bora nchini. Ujenzi wake unafanyika katika eneo la Kijichi na umeleta mwanga mpya wa maendeleo na hamasa ya kiuchumi kwa wakazi wa maeneo hayo.

 Sifa tano maalum

Mradi wa Samia Scheme Kijichi, umebeba sifa lukuki za kipekee kwa nyumba za makazi, lakini leo tunaweka hadharani sifa tano pekee ambazo ni pamoja na; mgawanyo wa nyumba za kisasa kwa familia tofauti yaani nyumba za vyumba 1, 2 na 3,vilivyopangwa katika majengo 12 ili kukidhi mahitaji ya familia mbalimbali.

Mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi kwenye Mradi wa Samia Housing Scheme Kijichi
Sifa ya pili ya kipekee ni miundombinu ya kistaarabu ndani ya mradi,  barabara za ndani, mifereji, umeme, maji na njia za watembea kwa miguu.

Sifa ya tatu ya Samia Housing Kijichi ni maegesho ya magari takribani 300, yakiwemo maegesho maalum ya ziada kwa ajili ya wageni na dharura.Hapo kila nyumba ina eneo la kuegesha gari yale ya ziada ni 40.

Mradi huo wa Samia Housing Scheme Kijichi una sifa ya nne ambayo ni kuwepo kwa jengo la huduma za kijamii likijumuisha maduka, huduma za kifedha, sehemu za burudani, na maeneo ya michezo kwa familia.

Wakati sifa ya tano ni ujenzi unaotumia teknolojia rafiki kwa mazingira, ili kupunguza gharama za ujenzi, kuongeza uimara na kuimarisha usalama wa wakazi.

Sifa hizo zote zinafanya eneo hilo la Kijichi kubadilika na kuwa la kisasa, hivyo hadhi yake na thamani kupanda hata ya maeneo nje ya mradi huo kuongezeka. Sifa hizo zinafanya mradi huo maeneo salama ya kuvutia yanayofaa kwa watanzania wenye kipato cha kawaida na cha kati kununua nyumba hizo bora na kuishi.

Mradi wa Samia Housing Scheme Kijichi utakavyooneka baada ya kukamilika
Mradi wa Samia Housing Scheme ulianza Agosti 2025 na unatarajiwa kukamilika 2027, ukiwa sehemu ya dira ya NHC ya kujenga jamii zilizo salama, zenye mpangilio na miundombinu yenye tija.  

KAWE 711


Mradi wa Kawe 711 ni moja ya alama mpya zinazoinua hadhi ya Dar es Salaam kama jiji la kisasa. Ujenzi wake wa ghorofa 17 kwa kila jengo umefikia zaidi ya asilimia 60, ukichagizwa na mahitaji makubwa ya Watanzania wanaotaka kuishi katika maeneo salama, yenye mandhari mazuri na huduma za kisasa.

 Sifa tano maalum

Sifa ya kwanza ya kipekee ya mradi huu ni kuwa na majengo marefu ya kisasa ya ghorofa 17 yaliyo na teknolojia ya kisasa ya ujenzi na usanifu wa kimataifa.

Ya pili ni kuwa na nyumba za hadhi ya juu za vyumba 2, 3 na 4 kupitia mpangilio wa nafasi uliojaa ubunifu zisizochoka zuzitazama. 

Sifa ya tatu ya Mradi wa Kawe 711 ni kuwa na maeneo ya burudani na afya ikiwemo mabwawa ya kuogelea, maeneo ya mazoezi, sehemu za watoto na bustani.

Kawe 711 pia umebeba sifa ya kipekee ya kuwa na maeneo ya huduma za kibiashara ndani ya mradi ambazo ni maduka, huduma za kibenki na maeneo ya ofisi ndogo.

Maegesho ya kutosha kwa wakazi wote ndiyo sifa ya tano inayojumuisha maegesho ya wageni na nafasi za ziada kwa magari ya familia.

Kawe 711 ni mradi unaolenga familia zinazotafuta ubora wa maisha, ukichangia pia ongezeko la thamani ya ardhi inayochochewa na shughuli za kiuchumi katika eneo la Kawe na viunga vyake hivyo kuwa eneo linalofaa kununua nyumba kwa ajili ya makazi kwa watu wenye kipato cha kati.

Mradi wa Ubia Kariakoo


Mradi huu unaotekelezwa kwa ubia kati ya NHC na wawekezaji binafsi ni mfano bora wa namna ushirikiano unavyoweza kuongeza kasi ya maendeleo ya miji. 

Kupitia mikataba 21, maeneo ya zamani yanageuzwa kuwa miradi ya kisasa yenye matumizi mchanganyiko yakivutia wafanyabiashara wengi zaidi na kuongezeka kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Sifa tano maalum                                                       Sifa kuu za kipekee katika mradi huu ni kuwepo kwa mchanganyiko wa matumizi ya majengo, yaani makazi, biashara, ofisi na huduma mbalimbali katika eneo moja.

Pili, ujenzi wake ni ule unaoongeza thamani ya Kariakoo kama kitovu cha biashara, ili kuimarisha uchumi wa eneo hilo.

Sifa ya tatu ni ubunifu wa usanifu, ambapo una majengo yenye nafasi pana ya kutosha, usalama, taa za kisasa na mfumo wa usimamizi wa taka.

Mradi wa Ubia Kariakoo ubejikita katika sifa ya kuwa na uwekezaji unaozalisha mapato mapema, taarifa za NHC kitengo cha miradi ya ubia zinaonesha kwamba  miradi inayoetekelzwa eneo hilo imeanza kuingiza mapato kabla ya ratiba. Hii ni ishara ya ubora wa usimamizi wa NHC.

Si hizo tu, bali sifa ya tano ya Mradi wa Ubia Kariakoo ni kutoa fursa kwa wawekezaji zaidi ya 100,walioonyesha nia kufanya biashara kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC). Hii inaonesha kwamba imani ya sekta binafsi kwa NHC imeongezeka.

Mradi wa Ubia Kariakoo ni chachu ya mageuzi ya maeneo ya biashara Dar es Salaam na utakuwa nguzo muhimu katika kuongeza mapato ya NHC lakini pia Serikali kupitia kodi, gawio na shughuli za uchumi.

NHC na kizazi kipya

Kwa ujumla miradi ya Kijichi, Kawe 711 na ya Ubia Kariakoo ni uthibitisho wa jinsi Tanzania inavyopiga hatua kubwa kwenye sekta ya makazi kupitia ubunifu, ushirikiano na uwekezaji wenye tija. 

Kupitia miradi hiyo na mengine inayotekelezwa nchi nzima, NHC imejipambanua kama mshirika imara wawekezaji binafsi, pia wa Serikali ikiweka msingi wa miji ya kisasa, yenye usalama, ustaarabu na fursa nyingi za kiuchumi.

Ramani inayonesha maeneo yenye miradi ya NHC mikoa mbalimbali nchini

Kwa kuongozwa na NHC ni wazi kwamba, makazi bora si ndoto tena, yanajengwa kila siku na kizazi kijacho kitaishi katika Tanzania iliyo bora zaidi, salama zaidi na yenye maendeleo ya kudumu.

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi