Rais ampeleka Ngorongoro Badru wa PSSSF, Dk. Doriye mhh..

 -Dk.Nyansaho bosi mpya PSSSF

Mwandishi Wetu,daimatznews@gmail.com

Rais Samia Suluhu Hassan,pichani chini ametengua uteuzi wa Dk. Elirehema Joshua Doriye aliyekuwa Kamishna wa Uhifadhi katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), huku akimteua Abdul-Razak Badru kushika nafasi hiyo.

Kabla ya uteuzi huo,Badru alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), ambapo Rais Samia amemteua Dk. Rhimo Simeon Nyansaho kuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, awali alikuwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara katika Benki ya Azania. 

                         
Dk. Nyansaho                                                 Abul- Razak Badru

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais – Ikulu, Rais amefanya mabadiliko hayo ya uongozi kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na kuimarisha usimamizi wa rasilimali katika taasisi hizo muhimu za Serikali.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Sanamu ya Bikira Maria yaonekana ndani ya Hifadhi ya Taifa Saadani

Kapteni Traole afuata huduma za afya nchini

Wawekezaji wa Oman watua nchini, wateta na NHC kuchochea mapinduzi sekta ya makazi